Tag Archives: Do I have to convert?

Ni lazima nibadilishe dini au niwe mfuasi wa Ujumbe Mpya ili niweze kupokea Ujumbe Mpya?

La. Kupokea Ujumbe Mpya ni kupokea hekima yake na mafundisho yake kuhusu Knowledge, dhamira, uhusiano, umoja, ushirikiano na kuibuka kwa ubinadamu katika Jumuiya Kubwa ya waangavu katika ukimwengu.

Basi, chukua ujumbe mpya na uwapatie watu wako, taifa lako, kabila yako, dini yako, na utambue zile nguvu kubwa zinazitisha kuangamiza uwezo wa binadamu kuishi, uhuru wa binadamu na enzi ya binadamu ndani ya duniahii. Lazima kuwe na ahadi mpya ya uhuru wa binadamu, umoja na hifadhi ya dunia.Ahadi hii inaweza kutokea to kutokana na Knowledge ile Mungu ameweka ndani ya kila mtu.

Unaweza kuwa Buddhist ndani ya ufahamu na uazimaji wa Jumuia Kubwa. Unaweza kuwa Muislamu ndani ya ufahamu na uazimaji wa Jumuia Kubwa. Unaweza kuwa Mkristo ama kuwa katika dini yeyote ama njia ya kiroho yayote ile umechagua, lakini kwa mtazamo mkubwa. Kwa kuwa ni muhimu uelewe kwamba nia ya Mungu sio kuumba dini mpya lakini uelewa mpya, ufahamu mpya na uazimaji mpya. Na hizi lazima ziwe ndani ya mataifa yote ya binadamu na dini zote.

Lakini, kuna wale kwamba Ujumbe Mpya utakuwa njia yao, na watakuwa wapokeaji wake wa kwanza na watendaji wake wa kwanza. Watahisi kwamba wamepewa kile ambacho wamekuwa wanakitafuta, na hicho ni njia mpya. Kwa wote wengine Ujumbe Mpya unapatia binadamu ufahamu mkubwa uelewa, nguvu na uazimaji ule lazima uelezwe katika familia ya dunia.

Pokea basi Ujumbe Mpya. Ilete kwa Moyo wako, akili yako, familia yako, jamii yako, dini yako ya kitamaduni, taifa yako na uelewa wako wa dunia, na utakuwa umepokea Ujumbe Mpya kutoka kwa Mungu.