Miadi Takatifu

Una hatima ya kukutana na watu fulani katika maishani. Una miadi nao. Wataongozwa kukutana na wewe kama vile unaongozwa kukutana nao. Mahusiano hayana msingi kutoka ufarisi wa maisha zilizopita duniani, lakini ni sehemu ya mpango ulianzishwa kabla uje diniani, mpango ambao uliundwa kukuwezesha utambue dhamira kubwa katika maisha yako. Mungu anajua huwezi kutambua na kutekeleza dhamira hii peke yake, kwa sababu ni maalum na tofauti kuliko kitu chochote duniani. Itapinga ufafanuzi na ulinganisho, kwa kuwa inaongozwa na Nguvu Kubwa na Hekima Kubwa zaidi.

Lakini huwezi kupata dhamira hii peke yako. Unaweza tu kuandaa njia kwa dhamira hii. Unaweza tu kuandaa akili yako na hali yako ili dhamira hii kubwa zaidi ijitokeze. Na ikinaanza kujitokeza, itabadilisha jinsi unajiona na unaona ulimwengu wako.

Mahusiano ni njia, lakini pia ni thawabu. Kwa sababu hakuna kitu kinachoweza kufanywa peke yake duniani. Hata kama unafanya kazi peke yako na unaishi peke yako katika upweke, chochote unachoweza kuunda bado ni mchakato wake na wengine. Ni mchakato wa kuunganisha akili yako na akili zengine- katika kesi hii, akili ambazo ziko zaidi ya eneo inayoonekana – kutoa kitu cha maana na muhimu mkubwa.

Hii ndio mwanamichezo anataka kwa kufikia nguvu zaidi na uwezo. Hii ndio mwanamuziki anataka kwa kuruhusu mchakato wa ubunifu ujitokeze. Hii ndio kila mtu anataka kwa kutafuta maana katika dunia, utafutishi ambao unaweza tu kutimilizwa na dhamira kubwa, iliyowatuma hapa mwanzoni.

Huwezi kufanya hata maandalizi ya dhamira hii kubwa peke yako, kwa utahitaji wengine ambao wanaweza kukusaidia na kutambua thamani yake ndani yako. Haya ni mahusiano ya kipekee. Hazijaimarishwa ndio uweze kupata fursa. Hazijaimarishwa kutimiza matarajio yako au ndoto zako. Zina jukumu kubwa zaidi, jukumu ambalo ni muhimu uipate nguvu ya kuheshimu kile kilicho ndani zaidi unachokijua. Inatoa mahusiano ya muda mfupi na inayodumu.

Hapa mahusiano ya muda mfupi ni kama alama, inayopointi njia, kukumbusha kwamba una wajibu mkubwa katika maisha. Hapa watu wataingia maisha yako kwa muda mfupi kusisimsha Knowledge ndani yako, au kutoa choto muhimu ya hekima ambayo unahitaji ili uweze kuendelea. Unaweza kuwa na mahusiano mengi kama haya kwa muda fulani, na kila moja utakusaidia kutambua njia yako na kupata nguvu ya kusafiri katika mwelekeo ule, ambao ni tofauti na ule kila mtu anaufuata.

Alafu utakuwa na mahusiano ambayo ni ya muda mrefu, hasa ukiendelea na kupata ufafanuzi zaidi na nguvu, na ukiweza kupata uhuru kutoka ahadi zako za awali na wajibu na ukiweza kutambua ndoto zako na hali ya mahusiano yako.

Hapa unaanza kufikia pointi ya maidi na wale ambao watachukua nafasi muhimu zaidi katika maisha yako, lakini hata kama muna hatima pamoja haimaanishi mutapatana. Kwa sababu kuna vitu vingi vinazoweza kukuwalisha nyuma. Kuna hatari nyingi zinazoweza kuzuia musiweze kufika katika pointi ya miadi. Kuna maamzi mengi ambayo yanaweza kugeuza maisha yako iende upande tofauti.

Kwa hivyo unaweza kufika pointi ya miadi na upate wengine hawajafika. Waliitolea maisha yao huko nyuma, na hata kwa wengine, walipoteza maisha yao. Na hii ni shida kubwa mno, unaweza kuona, kwa sababu wanamiliki sehemu ya misioni, misioni ambayo pia ni yako. Na kama watu wa kutosha hawatafika, misioni yako itakuwa hatarini.

Hapa kile unachoweza tu ni kuifanya sehemu yako peke yake kikamilifu iwezekanavyo na uombe kwamba wale ambao una hatima ya kukutana nao – ama pia wale bado hawako tayari – wafuate nguvu ya Knowledge iliyo ndani yao, akili ya ndani ile Mungu ameweka ndani yao iwaongoze, iwalinde na iwalete katika miadi hii takatifu.

Watu hufikiri dhamira yao ni kitu ambacho wanaweza kujitengenezea, ile wanafikiri itawafurahisha na ile wanaamini itawapa utimizo. Lakini bila Knowledge kama kiongozi na mshauri wako, mipimo hii haitakuwa sahihi na kwa mara nyingi itasababisha maisha yako ielekee mwelekeo tofauti, mbali na pale unahitaji kuenda na mbali na miadi takatifu ile unafaa kuwa nayo na wale wako hapa kushiriki dhamira kubwa zaidi na wewe.

Mara mingi watu huoa ama huolewa na kutolea maisha yao kabla wajue ni nini wanafanya, kabla ya kuwa na hali halisi kuwa wana mwelekeo na njia kubwa ya kufuata. Na miadi yao ikikaribia, wanatukutika, wanakuwa na wasiwasi na wanachugachuga, wakihisi kuwa kuna mahali wanahitaji kuwa ambapo ni tofauti na pale walipo.

Kama haufuati njia yako halisi maishani, daima utakuwa na wasiwasi, na wasiwasi hii na kutokuwa na uhakika itarudia mara kwa mara kwa sababu moyoni wako unajua huendi mahali unahitajika, hufanyi kile unahitajika kukifanya, na maisha yako haisongi mahali inapaswa kusonga. Hapa hakuna kiasi cha furaha au vikwazo au tiba inaweza kufuta usumbufu huu, kwa sababu ni ishara kuwa maisha yako ina hatima na ni lazima uifuate hatima hii. Ahadi yako kwa hii lazima iwe kuu zaidi kuliko mapenzi au fedha. Ni lazima iwe kubwa kuliko tamaa ya mali na usalama, hata mafanikio kama vile dunia inafasili mafanikio.

Kila mtu anaitwa, lakini ni wachache tu wanajibu. Usipojibu, hatimaye utapotea duniani, na tajiri au maskini maisha yako itakuwa ya kukata tamaa- itakuwa ya kushindwa, na kuchanganikiwa itakayokuwa ya kudumu.

Ukikosa ishara nyingi, ukitia shaka kile kinachoanza kujitokeza kutoka ndani yako, hatimaye utahisi kuwa umepotea, na hata mali yako itakuwa kama janga kwako. Kile ambacho kilitakiwa kununua furaha, ridhaa na uhuru hakitaweza kukutolea chochote hapa.

Zaidi ya mahitaji ya mwili na mahitaji ya akili, kuna mahitaji ya roho. Mahitaji ya roho yanaweza tu kutimilizwa ukihitimiza dhamira kuu yako na kuhitimiza miadi yako na wale ambao wanashiriki dhamira hii na wewe na watachukua nafasi katika ugunduzi wake na uelezo wake.

Hakuna hakika kila mtu atafika. Na ni miujiza kwa wale watafika kwa sababu ilibidi wafuate kile ambacho hakiwezi kuelezwa ili wapate njia ya kufika huko. Ilibidi wawezane na shuku zao za kibinafsi na mashawishi ya wengine ili waweze kufika katika miadi hii takatifu. Ilibidi waamini kile ambacho labda hakuna mwengine katika maisha yao aliamini ama kudhamini. Ilibidi wajitolee kwa uadilifu wao na hisia ambazo ziliwashawishi ni nini ambayo ni sahihi kwao.

Dunia daima hujaribu kukushawishi ukitake kile ambacho, au ukihitaji kile ambacho na uwe yule ambaye hawakilishi asili yako ya ndani zaidi. Ushawishi huu wa kupotosha huathiri kila mtu kwa digrii mbalimbali. Hata watu waasi dhidi ya maadili ya utamaduni bado huathiriwa na maadili haya. Kwa hivyo kuwa mwaasi peke yake haitoshi, kwa kuwa mpaka wakati ule utagundua mwelekeo mkuu zaidi na sauti iliyo ndani yako, bado utadhibitiwa na hali ya kijamii yako, iwe uikumbatie ama uikatae. Hakuna uhuru hapa.

Hapa unaingia jangwani. Unaondoka ile njia nzuri ile kile mtu anasafiri, na unafuata njia tofauti na ile haiwezi kufafanuliwa katika maisha yako. Hii ndio njia ambayo walii wote na wachangiaji kwa binadamu walisafiri, na ilibidi wasafiri bila idhini ya familia na marafiki wao. Ilibidi wasafiri bila idhini ya dunia. Ilibidi wasafiri bila uadui, bila kulaani wengine na bila kukana dunia kwa jumla. Kwa sababu ni dunia hii ulikuja kutumikia katika siku zijazo na ukiikana, hautakuwa katika nafasi ya kuitumikia kwa dhati.

Miadi ndiyo kila mtu anatafuta bila kufahamu kwa tamaa yao ya ushiriki, mapenzi na mahusiano. Hapa haja za akili, na haja nyingi za akili kwa kweli sio halisi, yanashindana na yanavurugia haja ya ndani ya nafsi. Watu hawatambui kuwa haja yenyewe ni ya kweli na ni halisi. Katika eneo ya ndani kabisa, ni msingi wa mafanikio na dhamani ya maisha yako na matimizo.

Lakini watu hawana uvumilivu. Wanataka mashirikiano sasa. Wanataka kutimiza ngono sasa. Wanataka kutimiza matarajio ya utamaduni kwa kuwa na familia sasa. Hawana nia ya kungoja. Wanaogopa wakingoja, miadi haitatokea. Kwa hivyo watu wanachukua hatua mapema. Wanaoa au wanaolewa kabla kuwa tayari. Wanapata watoto kama bado hawako tayari. Wanatolea maisha yao kwa kazi bila kuwa tayari. Ule muda wanakuwa nao katika mwanzo wa maisha yao kuchunguza na kufarisi mwelekeo wa ndani katika maisha yao mara nyingi hupotea kwa shughuli nyingine, hutumiwa kufuata tamaa zingine ama hukatwa kabisa kawa sababu ya madai na matarajio ya wengine, na kwa ukosefu wa uvumilivu wao wenyewe.

Hapa watu ambao wana mchango mkubwa wa kufanya duniani huishi maisha isiowakilisha asili yao halisi. Na kwa hakika, mahalalisho yamo kila mahali. Lakini watu wakiishi maisha ambayo haiwakilishi asili yao halisi na dhamira yao, daima wataishi maisha ya uchugachuga. Na wakikosa kuanza safari ya Hatua kwa Knowledge, tabia yao itakuwa ya upotofu na uharibifu wa kibinafsi kesi ikithiri. Na washirika wao hawataelewa tabia hiyo au asili a kutoridhika kwao.

Kwa hivyo watu hukabiliana na hii kwa kutimia hobbies zao, michezo na tabia obsessive. Ama wanameza madawa ya kulevya au kunywa pombe, wakijaribu kuzuia hisia inayojitokeza kwa muda kuwa hawako pale wanahitajika na hawafanyi kile wanafaa kukifanya. Kuwa wana ahadi zengine tofauti na kuna wale wanategemea watimize ahadi hizo. Kwa hivyo mgogoro wa ndani unakua. Kama watu wakianza safari yao kwa kutafuta mwelekeo wa ndani katika maisha yao, makosa haya yatakuwa adimu na ngumu kufanya.

Kwa hivyo watu hukosa miadi yao. Na hata kama wamefanikiwa katika maisha na wamepata maadili ya utamaduni, watahisi upungufu. Watahisi hali ya kushindwa, na hali ya majuto. Huwezi kubadilisha hii kwa njia ya mazungumzo, au kwa njia ya tiba au kwa njia ya kile utakachojiambia kwa sababu asili yako ya ndani ni asili yako ya ndani. Na kwa sababu una dhamira kubwa maishani iliyo asili na ya kipekee kwako, huwezi badilisha hali hii. Mwelekeo wa ndani unaojitokeza ni kitu ambacho huwezi kukana bila kuzalisha migogoro na vivinyovinyo ndani yako.

Na haitoshi kumuamini Mungu na kumuabudu Mungu, kwa kuwa kama huwezi kufuata kile Mungu amekiweka ndani yako kukifuata, kama huwezi kufuata Knowledge iliyo ndani yako ile Mungu ameiweka ikuongoze, basi maombi yako na kusujudu wako kwa kweli sio halisi. Unaweza muomba Mungu akupe neema, unaweza muomba Mungu akuokoe kutoka shida kubwa na ndogo, lakini haukuweza kufika pointi ya miadi na Mungu. Pointi ya miadi na Mungu ni pointi ya miadi na Knowledge ndani yako, kwa kuwa hapo ndipo Mungu huwasiliana na wewe. Hapo ndipo unaungana na Chanzo cha maisha yako.

Hapa kuna shida hata kama wewe ni mtu wa dini. Hapa dini inaweza kuficha uchugachuga na ukosefu wa utimilifu. Imani katika mafundisho ya kidini, kanuni za dini au imani ya kidini inaweza kuficha na kubadilisha jukumi ya msingi ile wewe unayo ya kujibu nguvu na uwepo wa Knowledge ndani yako. Ukikosa kujibu nguvu na uwepo huu, utakuwa mtumwa wa nguvu zengine, na hisia yako ya uhuru na hisia ya ustawi na utimilifu wako utakuwa dhaifu na utatoweka.

Hatimaye hili ni swala la utenganisho. Wale ambao wanaamini utenganisho ni ya ukweli na wanaweza kujitimiza kupitia mawazo yao na imani yao na tamma zao, hawatambui kwamba wana uhusiano wa msingi na Mungu, Muumba wa maisha yote. Unaweza kubishana daima na uhusiano huu na hisia ya dhamira, lakini huwezi kuitokomeza. Itakufuapa popote utakapoenda. Daima hutaweza kuitikisa kwa sababu hauwezi kujitenganisha na Mungu. Hauwezi kujitenganisha na maisha.

Kwa hivyo kusudi yako ikizidi, ukizidi kujaribu kuyakidhi mahitaji yako ya ndani kupitia matendo ya nje na ukizidi kujitolea kwa shughuli zako, kwa hobbies zako na matarajio yako, utazidi kujiimarisha dhidi ya miadi hii ya kimsingi ambayo unayo na Knowledge ndani yako.

Hapa huwezi kufanya mpango. Huwezi kujadiliana na Mungu na kusema, “Naam, mimi nitakupa sehemu kidogo ya maisha yangu kwa kile unachotaka, kama naweza kupata ninachotaka.” Hapa hakuna majadiliano. huwezi kujadiliana na Muumba wa Ulimwengu. Huwezi kujadiliana na nguvu ya Knolwedge ndani yako. Watu wale wanaofikiria hivyo hufikiri Mungu na Knowledge ni rasilimali zinazoweza kutumika kutimiza mahitaji ya kibinafsi, zinazoitwa zikitajikana, zinazotumiwa zikitajikana, vile unavyoweza kuita idara ya polisi au idara ya moto ukiwa na tatizo.

Hilo ni kosa kubwa tena sana. Na matokeo yake ni ya kutisha kwa sababu watu hudhamini kilicho kidogo au kile hakina thamani na wanakosa kile kilicho na thamani kubwa sana. Wanachagua kuimarisha imani zao na wale ambao watathibitisha imano hao. Hivyo hata hapa mahusiano yao yanafanya kazi dhidi yao.

Huwezi kutengua ukweli kwamba ulitumwa hapa kutimiliza dhamira kubwa. Unaweza kufikiri hii ni ukiukaji wa uhuru wako, lakini uhuru ni zawadi uliopewa ili uweze kugundua kile kilicho cha kweli na muhimu ndani yako, na uweze kufanya ugunduzi huu peke yako bila ugunduzi huu ulazimishwe kwako na nguvu kubwa ya kigeni. Watu wale huamini utenganisho hawapendi hii. Wanafikiri inakiuka uhuru yao. Wanafikiri ni aina ya udikteta wa Mungu katika ulimwengu. Wao huona ni kama kulazimishwa na sio kama zawadi ya ukombozi kama vile ilivyo.

Kwa hivyo kuna tatizo za msingi katika uelewa wa watu. Lakini hatimaye swala ni, unaweza kufika pointi ya miadi na Knowledge na pia na wale walio hapa kushirikiana nawe katika dhamira kubwa inayojitokeza katika maisha yako? Hii ndiyo utatafakari wakati utatoka katika maisha hii na kurudi kwa familia yako ya kiroho, kikundi chako cha masomo. Hawatashugulika na hobbies zako ama yale uliyoshugulika nayo. Hawatashigulika na majanga yako au makosa yako, mapenzi yale uliyoyapoteza ama shuguli zako za kiuchumi ulizoshindwa nazo. Hawatashugulika na tabia zako zisio za kawaida ama tabia za kipekee za maisha yako iliyopita. Watashugulika tu na kama ulifika pointi ya miada na Knowledge na wale ambao walitumwa kukutana nawe. Watakuangalia na watauliza, “Ulifanikiwa?” Na hautaweza kuwafichia ukweli, kwa kuwa zaidi ya dunia ni vigumu sana kudanganya katika mahusiano.

Hii ndiyo itakuwa muhimu mwishoni. Mambo mengi yalio muhimu kwako sasa ama yale unayokabiliana nayo sasa hayatakuwa muhimi mwishoni. Watauliza, “Ulifika pointi ya miadi? Ulifanya kile ulichotumwa kukifanya?” Na itabidi uwaambie ukweli kwa sababu itakuwa wazi kwa wote. Na kutoka kwa mtazamo huu utaweza kuona waziwazi, bila kikwazo.

Kwa hivo ni nini kiingne unaweza kukifanya ili kurudi na kujaribu tena. Hakuna “siku ya hukumu”, pale ukishindwa katika maisha moja utaenda jehanamu ya milele. Huu ni uvumbuzi wa binadamu. Lakini matokeo ya kutopata dhamira yako na kujaribu kuishi bila dhamira hii ni ya kweli na ni dhahiri kila siku katika mawazo yako, na mwenendo wako, tabia yako na ufarisi wako. Bila dhamira hii unaishi katika aina ya jehanamu – jehanamu iliyo nzuri, lakini jehanamu ambayo huwezi kuwa na furaha, ambapo daima hauwezi kuwa katika hali ya raha kwa sababu hauheshimu asili yako ya ndani.

Knowledge iko haka kuelekeza maisha yako katika mwelekeo fulani, lakini kama haufuati mwelekeo huo, ama haujaenda katika mwelwkeo huo utakuwa katika hali ya uchugachuga. Lakini uchugachuga huu haufai kukanwa ama kuepushwa. Ni wito wa utambuzi na azimio. Hii ndio maana Mungu hahukumu. Mungu huvutia na kuajiri. Dhana nzima ya jehanamu ni jinsi binadamu anajaribu kuwaadhibu wale hawezi kuwakubali, na kutimia Mungu kama mwaadhibu. Ni ya kulipiza kisasi. Ni chombo cha akili kuwaadhibu akili zengine, au kuzilazimusha ziamini, kuzilazimisha kwa nguvu ziamini kukubaliana na makubaliano.

Una miadi takatifu na Knowledge kupitia seti ya makutano yatayobadilisha mwendo wa maisha yako na kukufunulia asili yako ya ndani na ukweli wa ndani unaozidi mawazo yako yale yanayokuhusu, utu wako na historia yako ya kibinafsi – utambuzi ulio zaidi ya eneo na ukfikia wa akili.

Alafu una miadi na watu wengine. Miadi zingine zitadumu muda kidogo, na wale watakuja maisha yako kwa muda mfupi kukukumbusha kitu fulani, kukufundisha kitu fulani ama kusemea kitu ndani yako inayohitaji nishati na upya.

Alafu una miadi na wale watachukua nafasi kubwa katika maisha yako, wale wako hapa kutumikia kwa kiasi kikubwa kile ambacho hao wenyewe wanaanza kukitambua ndani yao. Wale watakaofika katika pointi ya miadi watachukua nafasi kubwa katika maisha yako na watasimama kinyume na mahusiano yeyote uliojaribu kuanzisha.

Kama utaweza kukutana na watu hao, utaona utofauti katika maisha yako, na utagundua kwamba kile ambacho umekua ukikifuata ni cha ukweli na hautafunga safari hii peke yako. Ukipanda mlima huu – hasa ukifika sehemu za mwinuko – utahitaji mahusiani makuu. Pengine moja wa watu hawa atakuwa bwana ama bibi yako. Pengine atakuwa mtu ambaye munagawana kazi yenyu kubwa zaidi pamoja. Pengine itakuwa mwalimu aliye hapa kukutia moyo uendelee na ushinde ukiendelea. Inawezekana kuwa moja wa watoto wako, anayetambua asili yako kubwa na yule maisha yake imeunganishwa na wewe kwa kueleza kitu cha kipekee na muhimu duniani.

Mahusiano yanaweza kuchukua fomu tofauti. Lakini ukifika katika pointi ya miadi, itakuwa wazi kuwa mahusiano yako kwa kweli inahusu kitu kiingine, zaidi ya vigezo vya mahusiano ya binadamu vya kawaida. Zitasemea kile kilicho ndani na kilicho kikubwa. Ni ya ajabu. Ina maudhui zaidi na takatifu. Ni kitu ambacho kiko zaidi ya eneo ya akili, kwa hivyo kinakosa ufafanuzi. Maneno yako na majaribio yako kuyaeleza yanaweza tu kukaribia maana kamili. Haya ni mahusiano takatifu, ni takatifu kwa sababu ya nia yao na asili yao ya ndani.

Miadi hii yakitokea katika kiasi hichi, hakutakuwa na uhakika wa mafanikio kwa sababu lazima mupambane na hali yenyu ya jamii, asili yenyu ya dunia na shida zote ambazo hujitokeza katika kujiimarisha na kujidumisha maishani. Miadi sio hatua la mwisho, bali ni chanzo na uanzishaji wa hatua ya pili katika maisha yako.

Hapa mzigo ule ulikuwa ukiubeba kwa muda mrefu unaanza kupata maelezo katika maisha yako na hasa katika mahusiano haya, na utaanza kushukuru na kuhisi muinuko. Utauhisi upya na uhakikisho kuwa kwa kweli unafuata kitu muhimu, kuwa haujidanganyi na kwa kweli zina nguvu kubwa na ukweli mkubwa kwa maisha yako. Mahusiano haya yatatoa ushahidi wa jambo hili. Yatashuhudia jambo hili. Siri itakuwa nawe na kati yenyu – siri ambayo hamutaweza kufafanua, lakini ambayo lazima mujifunze kuitegemea na kuithamini juu ya vitu vyote.

Uhusiano wako na Mungu daima hautaweza kuelezeka. Hauwezi kuufunga ndani ya seti za imani, kanuni au mafundisho. Kufanya hivyo ni kuiweka ndani ya kaburi. Daima iko hai na inabadilika. Daima itakuangazia maisha yako na kukuongoza ufuate mambo fulani na kukupeleka mbali na mambo mengine, kama beacon kubwa inayokuongoza nyumbani – kutoka utenganisho, kutoka jehanamu ya utenganisho wako, kutoka migogoro yako ya zamani isiyo na suluhisho, kutoka tabia za madhara zile unashinda ukizirudia, kutoka ndoto zako, kutoka mishwasha, kutoka hatia, kutoka kushindwa.

Ni jambo la kushangaza kwamba wale ambao watajibu na kufika katika pointi ya miadi takatifu ni watu ambao wameshindwa kujitimiza duniani. Na labda watafikiri kuwa ni watu ambao wameshindwa duniani. Wameshindwa kupata mapenzi ama mali ya kutosha. Ama wameyapata haya, na kugundua kuwa hayatimizi mahitaji yao. Kwa hivyo kuna hisia ya kushindwa na disillusionment. Lakini kushindwa huku na disillusionment ni muhimu. Wakati kila mtu anajaribu kuepuka kushindwa na disillusionment, haya mawili yanatayarisha watu kugundua ukweli wa ndani unaoishi ndani yao.

Kama umeshindwa kufika katika pointi ya miadi, baadaye katika maisha, ukigundia maneno haya, kuna ukombozi wa pili. Na hii ni kuchangia kwa wengine – kuchangia mali yako, kuchangia wakati wako na kuchangia chochole unachoweza kuchangia katika huduma ya mahitaji halisi ya watu na dunia karibu na wewe. Huu ndio ukombozi wa pili. Hauna nguvu na utimizo kama wa kwanza lakini ni muhimu na utakuwa na ufanisi. Wale ambao wamekuwa na nia isiyoeleweka watapata mwishoni ya maisha yao kuwa wana fursa ya kuchangia, kuwa wafadhili – wafadhili wa mali, kama wana mali; wafadhili wa wakati, wakiwa na wakati; wafadhili wa huduma, wakiwa na nguvu ya kutoa huduma. Kwa hivyo kuna ukombozi wa pili.

Lakini kilicho muhimu kwa watu wadogo na wale walio katika umri ya kati, ni kuzingatia miadi takatifu – kuomba wafanikiwe, kuuliza wafanikiwe, kuambia Ulimwengu, “Chochote kitachohitajika kufanywa ili niweze kufika katika pointi hii ya miadi, lazima nifike pointi hii. Lazima niijue dhamira kubwa inayoishi ndani yangu.”

Ukiwa ambivalent kuihusu, ukiiogopa, ukiwa katika migogoro kuihusu, hautafika katika pointi hii ya miadi. Kwa hivyo lazima ukichague utakachokithamini. Na kama umepata hekima ya kutosha maishani – kupitia mafanikio na kushindwa, kupitia majalio na nuhusi – utajua jinsi ya kuchagua kisahihi. Utaona kuwa dunia inaweza kutoa furaha na huzuni, lakini sio utimizo.Hii lazima itoke kutoka sehemu ingine, kutoka Ukweli Mkubwa unaoishi ndani yako, ndani ya Knowledge.

Kuna sababu unatafuta katika mahusiano, lakini sio uridhike, upate mali ama kwa sababu ya tamaa. Kuna sababu zaidi. Na ingawa utashindwa mara mingi katika mahusiano, kamwe hautakata tamaa kwa sababu unatafuta miadi takatifu yanayokusibiri na yalio muhimu katika utimizo na mafanikio katika maisha yako.

Hatima

Ujumbe Mpya umo hapa kuagiza ubinadamu na kuhifadhi utamaduni wa binadamu. Ni jibu ya maombi isiohesabika kwa uongozi wa mtu binafsi na kuleta ushirikiano mkubwa, nguvu na ubunifu wa familia ya binadamu kwa wakati wake wa haja kubwa na taabu.
Ni kubwa sana, kiasi watu hawataweza kuielewa, ingawa watafikiri wameielewa. Na hata hivyo ni rahisi kiasi watu wanaweza kuitumia leo, katika kila hali, na kwa kila mtu ambaye watakutana naye, katika kila seti ya mazingira.
Ujumbe Mpya ni wa kuandaa binadamu ili aweze kuishi katika dunia mpya na kuandaa binadamu katika mahusiano na maisha iliyo nje dunia hii, ushiriki ulio sehemu ya hatima yenyu na mageuzi.
Wakati huu sasa, ubinadamu hauko tayari kukabili pointi hizi kubwa za mageuko – vizingiti hivi vikubwa ambavyo vitahitaji nguvu zaidi, utambuzi mkubwa zaidi na huruma mkubwa kutoka kwa watu kila mahali.
Ni wito mkubwa wa mtu binafsi awe na hekima na awajibike, awe na uwezo na uelewa. Ni zawadi ya watu wote na mataifa. Ni zawadi ya wakati huu na nyakati zijazo. Unajibu maswali ambayo bado hamujaweza kujifunza kuyauliza. Unatatua matatizo ambayo watu bado hawajafahamu.
Unaleta hekima ya Muumba. Umetumwa na uwepo wa Malaika, ambao unatafsiri mapenzi ya Muumba katika maneno, mawazo na maombi.
Ujumbe Mpya unatoa ufafanuzi wake na mazoezi. Kwa kuwa hauwezi kuachwa kwa watu na watu binafsi, hata wasomi na wataalamu, kuamua maana yake na jinsi mazoezi yafaa kufanywa. Ujumbe Mpya wenyewe unazungumzia mambo haya na unafafanua mambo haya ili upunguze kwa kiasi kikubwa uvumi wa binadamu na tafsiri ya binadamu. Dhumuni ya kufanya hivyo ni kupunguza uwezekano wa makosa ambayo yanajitokeza wakati watu wanashughulika na jambo kubwa ya aina hii.
Tahadhari kubwa inafanywa kutoa mafundisho haya, mazoezi na ufafanuzi- ikisemwa kwa njia nyingi tofauti, ikitumiwa katika hali tofauti, ikionyeshwa tena na tena ili ufafanuzi wake uweze kuwa wazi na kusiwe na ukosefu wa udhahirifu unaohusiana nao.
Kwa mara ya kwanza, Ufunuo Mpya unaotolewa kwa ubinadamu unao uwezo wa kusoma na kuandika, kwa dunia ya mawasiliano ya dunia nzima, dunia ya biashara na kwa baadhi ya watu wengine wanaoanza kufahamu dunia.
Unaotolewa sasa katika kina kubwa na ufahamu ili uweze kuunganisha watu wa tamaduni, temperamenti, raia wa nchi na rangi tofauti ndio uweze kupatikana na kueleweka na mtu binafsi, bila kutegemea wasomi wakubwa au taasisi kuamua nini maana yake, nini inasemwa na jinsi mtu anatakiwa kujibu.
Ujumbe Mpya unatoa wito ili nguvu ya Knowledge iliyo ndani ya mtu binafsi itokee-nguvu iliyo ndani zaidi ya mazingira ya akili, nguvu isiyoweza kueleweka na bado ni sehemu ya ufarisi wako.
Kwa baadhi kadhaa ya watu, hii itakuwa ngumu sana kushughulikia. Wao huangalia kila kitu duniani kama ni rasilimali ya akili zao. Lakini Knowledge ni kubwa sana na haiwezi kutumika kama rasilimali ya akili. Watu ambao wanadai wanafuata Knowledge watakuwa wakifuata mawazo yao. Watu ambao wanaodai wanaongozwa na Knowledge wataongozwa na hali zao za kijamii au na tamaa zao. Na hivyo kwa baadhi ya watu hii itakuwa ngumu sana kuelewa. Hii ni kwa sababu ya jinsi wanavyojiona wenyewe na dunia.
Si kila mtu atakuwa na uwezo wa kufahamu ukweli mkubwa kwa wakati huu. Lakini kama watu wa kutosha wataweza, itatoa ahadi kubwa kwa siku zijazo, na kwa usalama na uhuru wa binadamu.
Dunia mpya itakuwa hatari zaidi kuliko dunia ambayo umezoea. Na Jumuiya Kuu ya maisha ni ya tatanisho na ngumu.
Ni lazima mujifunze kuihusu. Ni lazima mujifunze Hekima na Maarifa kutoka Jumuiya Kuu. Na hiki ni kitu ambacho Mungu pekee  anayeweza kuwafunza. Hata mataifa mengine hayawezi kufanya hivyo, kwa kuwa hawajui akili ya binadamu na roho ya binadamu cha kutosha ili waweze kufanya hivyo na hawadhumuni uhuru, isipokuwa mataifa chache tu.
Umezaliwa katika wakati huu. Umezaliwa kwa sababu ya wakati huu. Ni hatima yako kuwa hapa, kujifunza kuhusu mambo haya. Ni hatima yako kupokea maneno haya. Ni hatima yako kugundua Ufunuo Mpya.
Watu wengi duniani hawajaweza kujitolea katika dini za utamaduni za binadamu kwa sababu kuna kitu katika roho yao kilichowaambia wasubiri. Labda wanahalalisha hii kwa ajili ya mapungufu au matatizo yaliyopo ndani ya mila fulani. Lakini hiyo siyo suala, unaweza kuona, kwa kuwa hatima yao ni kitu kiingine, na ilibidi wasubiri Ufunuo. Si ati kwamba mila yao ni duni kwa jinsi fulani. Ukweli ni hatima yao ni kitu kiingine kwa sababu ya asili yao na vile walivyoumbwa, kwa sababu ya dhamira yao, kwa sababu ya hatima.
Hii ni nguvu kubwa kuliko akili ya binadamu, na inaleta changamoto zake zenyewe na baraka zake kubwa na fursa.
Njia ya kurudi kwa Mungu sio ya kiakili. Huwezi kuja kwa Mungu kwa njia ya madai yako. Ukweli na uumbaji havipo kulingana na uelewa wako au tathmini. Mawazo yako hayana madhumuni mbinguni, ni ushiriki wako peke yake.
Hatima si kitu ambacho unaweza kuagiza mwenyewe, wala kitu unaweza kufafanua na kusema, “Hii ni hatima yangu kwa sababu nilalipenda wazo hilo.”
Hatima inahusu pale ulipotoka na pale utaenda na sababu yako kuwa hapa duniani na pale dunia inaenda-mambo yalio zaidi ya mazingatio na ufahamu wa watu.
Hatima itakuongoza, kwa kuwa ni sehemu ya Knowledge iliyo ndani yenu-akili kubwa ambayo Mungu amewapa, iwaandae na iwalinde, iwafafanulie njia yenu na iwashiriki na hatima yenu.
Watu wa Ufunuo Mpya ni sehemu ya kizingiti mpya cha maelewano kwa binadamu kwa sababu binadamu anaingia katika dunia mpya- ulimwengu wa mabadiliko ya mazingira; ulimwengu wa ukosefu wa utulivu wa kisiasa na kiuchumi; ulimwengu wa rasilimali utovu; dunia ambapo hatari ya mgogoro ushindani, na vita itakuwa kubwa sana; dunia ambayo inahitaji ushirikiano mkubwa na hali ya hatima moja pamoja na wengine.
Bila umoja, ubinadamu utashindwa katika Jumuiya Kubwa na kuanguka chini ya ushawishi wa nguvu za kigeni, kama vile ilivyojitokeza mara mingi katika historia ya ulimwengu. Hiyo ni hatari kubwa kwenyu.
Hata hivyo, ni nani ambaye anayatambua haya? Ni nani ambaye anayawaza mambo haya? Ni nani ambaye ana wasiwasi kuhusu haya? Yale watu wanayafikiri na, wanaamini na wanatarajia ni tofauti sana yale Mungu anajua, na hapa ndipo lazima daraja ijengwe. Hii ndio maana Mungu ameiweka Knowledge ndani yako-ili uweze kupata uelewa huu mkubwa na kubainisha ukweli mkubwa.
Mungu ametoa Hatua kwa Knowledge kushiriki akili yako ya juu – akili ya jamii, akili ya dunia- na akili iliyo ndani yako ya Knowledge. Hapa ndipo unakuwa moja katika sehemu zako zote. Hapa ndipo unaanzisha ufarisi wa uadilifu wako.
Hii ndio inakupatia nguvu na uwezo wa Mbunguni ukisafiri hapa duniani. Hii inakupatia madhumuni, maana na mwelekeo kwa kuwepo yako hapa na inatoa wito kwa watu fulani ambao watakuwa na jukumu muhimu katika ugunduzi na kuelezea lengo kubwa zaidi ambalo limekuleta hapa kwa wakati huu, katika hali hii. Hii ni hatima yako.
Usilalamike kuhusi dunia. Usiwe na uchungu au uchovu katika mtazamo wako wa dunia, kwa kuwa hii ndio dunia umekuja kutumikia. Ni kamilifu kwako. Hii ndio sababu umekuja.
Usiikane ama utakana dhamira yako kuwa hapa. Usiihukumu, ama utajihukumu pamoja nayo. Usijitenganishe kutoka kwake, ama utapoteza uhusiano na asili yako ya ndani.
Hatima imo nawe. Wito mkubwa unaenda nje. Mtume anatayarishwa kuongea duniani. Ufunuo Mpya umo hapa.
Ni baraka kubwa kuwa duniani katika wakati huu – wakati wa Ufunuo! Ni baraka kubwa kuwa unaweza kujifunza kuhusu haya. Ni baraka kubwa kuwa na hatima, kujifunza kuihusu na kuwa na unyenyekevu na hekima ya kuipokea.
Watu huwa na shida na mambo haya kwa sababu ya kiasi ambacho hao wanahusisha imani yao, malalamiko yao na mawazo yanayo wahusu, ambayo kwa mara nyingi hayana kitu chochote cha kufanya na swala linalotamkwa, ni nani hao kibinafsi na sabau yao kuwa duniani.
Mabadiliko ni magumu kwa watu, hasa mabadiliko ya ndani, lakini ni asili na lazima au huwezi kuishi maisha makubwa au ya lengo kubwa zaidi. Na huwezi kupatikana kwa mahusiano zaidi na muungano mkubwa na wengine.
Hii ndio malipo ya kiingilio. Hii ndio inamaanisha kupata jibu kwa maombi yako. Kwa kuwa maombi yako yakijibiwa inammanisha mlango umefunguliwa, na ni lazima uupitie. Sio safari ya maamuzi yako na haitatokea kulingana na maneno yako, mawazo na matarajio.
Ukitaka Mungu akusaidie, lazima basi umuwache Mungu akukusaidie na akuongoze. Mungu anakuongoza na anakusaidia kwa njia ya nguvu na uwepo wa Knowledge.
Lakini ni lazima uwe katika mahusianio na Knowledge, ukuchukue Hatua kwa Knowledge, ufarisi ukweli wake, uwezo wake kamilifu na kuendeleza ujuzi wa uvumilivu utaokuwa muhimu kwako kwa safari hii katika mikoa ya maisha na ufarisi ule kwa sasa hauko katika ya dhana zako au uelewa wako.
Mungu anakijua kile chakuja katika upeo wa macho. Swali ni, watu wanaweza kujibu na kujiandaa, na wanaweza kupokea maandalizi yale Muumba wa uhai wote ametuma duniani?
Ubinadamu hauwezi kijitayarisha. Haujui kwa nini unajitayarisha. Haujui hali ya maisha katika ulimwengu. Haujui jinsi ya kujitayarisha. Hautarajii kukabiliwa na dunia mpya.
Kwa hivyo haujajiandaa na hauna fahamu, unafikiri kuwa siku zijazo zitakuwa kama zamani, unaishi katika siku zilizopita, na kujihusisha na siku zilizopita, bila kuona hali ya mabadiliko ya dunia- mazingira ya inayobadilika na mabadiliko makubwa yanayokuja katika upeo wa macho.
Hamuna muda wa kutosha wa kutitayarisha kwa haya yote, kwa maana yako katika mwendo, na hamuwezi kuyazuia. Hamuwezi kuzuia kuingia katika dunia mpya. Hamuwezi kuzia dunia yenyu iibuke Jumuiya Kuu ya maisha katika ulimwengu. Maingilio tayari yameanza duniani kupitia jamii zilizo janja ambazo zipo hapa kupata faida kwa sababu ya ujinga wa binadamu na matarajio ya binadamu.
Hamuwezi kutoroka hatima yenyu, munaweza kuona, na hatima hii itawainua, au itwashinda, kulingana na jinsi mutajiandaa na uwezo wenyu wa kujibu – uwajibu wenyu.
Huu ndio wakati. Hamuna wakati wa kuwa wadhaifu. Hamuna wakati wa kujificha katika hisia kinzani. Hamuna wakati wa kujipoteza katika hobbies zenyu, mapenzi yasio ya dhamira na tafrija haribifu.
Dunia yabadilika. Inasonga chini ya miguu yenyu. Inatetemesha miji yenyu. Inanyima watu wenyu. Inabadilisha jinsi mutakavyoishi duniani. Inabadilisha hali ya anga duniani, hali ya hewa, mazingira,  uwezo wa kuzalisha chakula na rasilimali mutakazohitaji kudumisha utamaduni.
Ni nzito. Ni kubwa. Lakini watu bado wanalala, wanaota, wamepotea, hawaajibiki, wako obsessed, preoccupied, aliwasihi, na wanaamini kile wanachoambiwa na viongozi wale wanajua kidogo tu kuliko kile hao wenyewe wanajua kuhusu yale yajao katika upeo wa macho.
Lakini watu hawezi kuwa wajinga kabisa kwa sababu Knowledge inaishi ndani yao, na Knowledge inatoa ishara la onyo. Hii ndio maana watu wana wasiwasi. Hii ndio maana watu wanahisi ukosefu wa uhakika kuhusu uimara wa mustakabali wa binadamu. Hii ndio maana watu wana wasiwasi.
Wasiwasi hii ndio inakupatia kidokezo kwamba katika kiasi fulanu unakabiliana na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko yajayo duniani na badiliko la nafasi ya binadamu katika ulimwengu.
Ni ishara ya mabadiliko makubwa. Hauielewi. Hauwezi kuifafanua. Lakini uko hapa kukabiliana nayo kwa sababu ni hatima yako.
Kutoka upande mkubwa zaidi, kutoka upande wa Uumbaji, hatima ni kila kitu. Lakini sio hatime ile wewe mwenyewe umejiamulia. Ni hatima ile Mungu amekupatia. Ndio maana uko hapa. Ndio maana nafsi yako iko vile ilivyo. Ni kamilifu kwa wito wako wa kweli katika maisha, wito ambao una uwezekano bado haujautambua.
Hii ni hatima. Hii inaishi zaidi la eneo ya akili. Zaidi ya eneo la filosofia na theolojia, zaidi ya upendeleo, zaidi ya hofu, zaidi ya vivinyovinyo, zaidi ya uhakika wa binadamu- singizio la uhakika wa binadamu- zaidi ya imani ya dini, zaidi ya nafasi ya kisiasa, zaidi ya nadharia ya uchumi ni hatima.
Akili yako haitaelewa lakini katika sehemu ya ndani utaanza kujibu kwa sababu katika sehemu ya ndani, umeunganishwa na hatima.
Una hatima ya kukutana na watu fulani kama unaweza kuhitimiza mkutano huo, kama hautapotea njiani kwa  mkutano huu mkubwa na wengine.
Ni hatima kwamba lazima mukabili dunia mpya na ukweli wa Jumuiya Kuu ile Mungu atawafunilia kutumia Ufunuo Mpya.
Ni hatima kwamba unayasikia maneno haya. Ni hatima imeleta Ujumbe Mpya kwako na imekuleta kwa Ujumbe Mpya.
Hatimaye, utaelewa mengi ya mambo haya. Lakini kwa sasa, ni swala la kuwa na imani kubwa kwamba nguvu ya Knolwedge inaishi ndani yako, kwamba ni safi na ni uumbaji wa Mungu.
Ni unyenyekevu na utambuzi utakaoleta utakuwezesha kutambua tofauti kati ya Knowledge na mawazo, hofu na matarajio yako na mawazo, hofu na matarajio ya wengine.
Hapa ndipo unakuwa mjuzi. Hapa ndipo unaweza kutambua. Hapa ndipo hauko kama mtoto yule lazima aongozwe, bila kujua, kwa maana hii haitakuwa sahihi katika dunia mpya.
Ubinadamu lazima upevuke. Raia wake lazima wafahamu na wawe macho, watayarishwe na waimarishwe. Wacheni watoto wawe watoto, lakini kama wazima, lazima mupate mtazamo mkubwa na muwajibike.
Hizi sio nyakati za kale. Hauambiwi uwe kama kondoo. Unaambiwa ukabiliane na haya, na uchukue hatua kwa Knowledge na uruhusu Knowledge ifanye mabadiliko kwa maisha yako na ikufunulie hatima yako kubwa.
Hii ndio Nia ya Mbinguni, na sas lazima iwe nia ya binadamu.

Ujenzi wa Daraja ya Maisha Mpya

Wakati fulani utakuja kutambua kwamba Ufunuo huu Mpya huko hapa ili kukupatia maisha mapya. Hauko hapa kuboresha maisha yako kwa kutia maana ya kiroho au kusamehe mawazo yako na imani na matendo yako ya zamani kupitia aina ya baraka kutoka juu.
Wakati fulani utakuja kutambua kwamba maisha unayoishi kwa kweli si sahihi kwako. Ni maisha ya kuafikiana. Na maafikiano yamekuwa makubwa mno. Kwa hakika yamekuwa makubwa mno. Ni maafikiano kuhusu vile unajiona, kuhusu vile unawaona wengine, kuhusu vile unaiona dunia. Na ingawa labda utapinzana na utambuzi huu, labda utaukana, na maafikiano mengine yatatafutwa, katika ukweli unawakilisha mwanzo wa matumaini makubwa kwako.
Kwa maana Mungu anajua kwamba bila Knowledge, akili zaidi ile imewekwa ndani yako, basi utaishi maisha ya maafikiano. Utatafuta maafikiano ili upate usalama, ili upate idhini, ili upate mali na faida. Utatafuta maafikiano ili uepuke kejeli au upinzani au hukumu au hata kukataliwa na jamii. Maafikiano yatapenya kila kitu, kuanzia imani yako, mitazamo yako, matarajio yako, shughuli yako, mipango yako, malengo yako. Na hii itaongezeka hadi pale ambapo kwa kweli utapoteza mawasiliano na asili yako.
Sasa umekuwa bidhaa ya jamii yako, bidhaa ya matarajio ya jamii, bidhaa ya mawazo yako binafsi, lakini umepoteza mawasiliano na asili yako ya undani na maana ya maisha yako. Na hata kama utafanikiwa na kufikia malengo yako, yatakuwa tupu, na furaha yako itakuwa ya muda mfupi, na itakuja kwa bei kubwa ya muda, nishati, juhudi, na Manufaa yake yatakuwa ya muda mfupi na itakukimbia.
Ugunduzi huu, ambao hukanwa na kuepukwa, ni mwanzo wa ahadi kubwa zaidi kwako. Usipingane nao. Usibishane nao. Usilalamike kuwa lazima ubadilishe maisha yako kwa kiasi kikubwa. Bila shaka lazima ubadilike! Kwa sababu unapewa maisha mpya – sio maisha bora kidogo kuliko ya zamani, si tu scenery mpya au nyuso mpya au aina mpya ya kusisimua. Haya sio mabadiliko ya mapambo. Haya ni mabadiliko ya umuhimu mkubwa sana na wa kina kikubwa cha maana kwako. Haya ni aina ya mabadiliko ya moyo wako uliokuwa unautamani kwa muda mrefu. Kwa muda mrefu umekuwa ukifanya kazi.
Na sasa inaonekana kuwa umeshindwa. Inaonekana umeshindwa kutimiza matarajio ya utamaduni wako. Hata labda unajisikia kuwa umeshindwa, kuwa hujatimiza malengo na matarajio ya familia yako, utamaduni wako na hata dini yako. Lakini katika maono ya kushindwa huku kuna ahadi ya mafanikio makubwa zaidi. Maisha yako ya zamani lazima ikushinde au lazima uiwache ndio uweze kuwa na nafasi mpya, ufunguzi huu katika maisha yako, huu ni mwanzo mpya.
Watu wengi wanataka tu kuwa na ufunuo kama kuwa ni aina fulani ya kitambi ya maisha yao ya zamani, kama kiroho ni kama kitoweo kwa udufu wa maisha yao. Ni kitu ambacho wataongeza. Sasa watakuwa watu wa kiroho na watafanya mambo ya kiroho na kufikiri mawazo ya kiroho na kufanya shughuli ambazo zitaonekena kuwa ni za kujenga na kuinua, Lakini tena, hii yote ni ya idhini. Hii yote ni ya kutafuta radhi zaidi, faraja zaidi, usalama zaidi. Motisha huu hauna tofauti na motisha wa kuongoza watu kutafuta mali na furaha na kuepuka maisha. Hii sio halisi. Na matokeo yake, hauzai matokeo halisi. Tunaongea kuhusu kitu tofauti sana hapa.
Na maisha haya mapya, bado haujui maana yake. Bado huwezi kujua vile itakavyokuwa kwa sababu ni mpya. Haitakuwa uvumbuzi wako. Haitakuwa kama ile umezoea. Kwa hivyo unaanza kugeuka kona hii polepole sana. Hata kama kuna matukio makubwa katika maisha yako yaliyokuleta katika ufahamu huu, sasa , safari ina hatua nyingi, ndio ikuruhusu uwe na muda wa kujifunza na kukabiliana na kupata msingi zaidi wa kujiamini ndiyo maisha yako iweze kuongozwa na kilicho ndani badala ya vilivyo nje, ndiyo upate kuwa mtu wa uwezo na nguvu na uadilifu, badala ya mtu ambaye ananakala maadili ya tamaduni yao.
Hapa lazima mambo mengi yafunzwe tena. Lazima yachunguzwe tena. Mawazo yako mengi yatabidi yachunguzwe tena. Dhana zako za imani ulizoimarisha zitabidi zichunguzwe na kwa baadhi ya kesi ingine itabidi ziwekwe kando. Hii ni bei ya uhuru. Hii ndiyo bei ile watu hulipia ndio wawe na fursa ya kuishi maisha makubwa, maisha halisi, maisha ambayo inalingana na Knowledge ndani yao, maisha yale yanatimiza hatima ile walitumawa duniani kukamilisha.
Mpaka hatua hii ifikwe, unaishi nusu ya maisha. Ndiyo, moyo wako unapiga, na damu inapitia mishipa ya damu yako, na akili yako ni inatoa taarifa ya dunia karibu nawe, na unaenda kwa miendo ya maisha yako, unatimiza majukumu na wajibu wa maisha yako na unajaribu kutafuta baadhi ya fomu ya furaha. Lakini uwepo huu ni tupu. Bado hujagundua maana halisi na thamani ya maisha yako. Hadi hatua hii, Knowledge, akili kubwa ile Mungu ameweka ndani yako ikuongoze na ikulinde, itajaribu kuwalinda dhidi ya madhara, itajaribu kukushika na kukushikilia ili usifanye makosa makubwa na ya muda mrefu na kujitolea kwa ahadi ambazo zitakuwa katika upinzani na uwezo wako wa kugundua na kuishi maisha  makubwa katika siku zijazo.
Hapa katika hatua hii ya kwanza Knowledge itaonekana latent ndani yako, lakini kwa kweli bado inajaribu kukuweka nje ya taabu na kuzuia uitolee maisha yako kwa wengine au kwa hali au mahali, kwa watu, kuweka maisha yako iwe wazi. Watu wengi bila shaka wako katika hatua hii ya kwanza. Uibuka bado haujatokea kwao. Wakati utatokea, na jinsi utatokea na hata kama utatokea ni kitu wewe haujui. Ni fumbo.
Unaweza kuona, kabla ya uibuka huu, kwa kweli unajenga msingi wa kuwa mtu anayeweza kuishi duniani. Unajenga stadi za maisha. Unahisi raha na maumivu ya dunia hii. Unatafuta radhi na unaepuka maumivu na kupata yale yanayokata tamaa njiani. Maandalizi haya ya mapema yanaweza kuwa muhimu sana kwa kile ambacho unachoweza kukitambua, kukikamilisha na kushirikisha na wengine katika siku zijazo. Hata makosa yale ya ujinga zaidi utayofanya katika hatua hii ya mwanzo yanaweza kuwa muhimu sana katika kukupatia hekima, kukufundisha yaliyo ya kweli, kuthamani yale ya kweli, kukusaidia uweze kutambua kile kinachonekana ni kizuri kutoka kile kilicho kizuri, kukusaidia kutambua kile kilicho kizuri kutokana na kile tu kinaonekana ni kizuri, kukusaidia kutambua mwelekeo wako halisi kutokana na impulses zinazowakilisha udhaifu wako na ukosefu wa usalama.
Pengine katika hatua hii ya kwanza utahisi kuna uwepo unakuangalia mara kwa mara. Utahisi uwepo umo nawe. Na utadhani mara kwa mara kuwa kuna kitu kikubwa unafaa kukifanya katika maisha, lakini utambuzi bado haujatokea. Bado haujateketeza msingi wako. Ni kitu tu unakifikiri katika eleo la akili yako. Bado haujapenya moyo wako.
Kushindwa kwako na kukata tamaa hapa itashikilia ahadi kubwa kwako. Kukata tamma katika nafsi yako na wengine na katika furaha kubwa ambayo umelipa bei kubwa, kweli, hii ita banar njia kwa utambuzi huu. Na utambuzi huu hautadumu wakati mfupi. Itakuwa ni kitu ambacho kitabadilisha mwelekeo wa maisha yako, na hutaelewa kilichotokea kwako au asili na dhamira ya mabadiliko ya mpaka usafiri katika hatua ya pili ya safari yako.
Miongozo ya kuishi yatayotolewa hapa yanahusiana na hatua hii ya pili ya safari ya maisha yako. Hayahusiki na watu ambao hawajavuka kizingiti hiki kikubwa, ambao hawajafarisi hatua hii ya kugeuka. Kwao yataonekana kuwa ya manufaa lakini ya utata. Yataonekana ni kama yatwarudisha watu nyuma. Yatakuwa ni changamoto kwa mawazo yao ya uhuru. Yataonekana yanahitaji juhudi kubwa na wajibu kwa sababu hawako tayari kufanya juhudi hii au  kuchukua jukumu hili. Bado wanajaribu kupata kutoka kwa maisha kile wanachotaka, zaidi ya mahitaji yao ya msingi. Wanajaribu kupata kutoka kwa maisha wanachotaka. Hawatambui kwamba walitumwa duniani kwa dhamira. Hawana kumbukumbu ya Nyumba yao ya Kale, kwa hivyo wanafikiri maisha haya ndiyo muhimu sana, ni kila kitu. Wanataka kuishi kwa muda, kwa wenyewe. Kwa hivyo mtu huanza kupata baada ya kizingiti hiki kikubwa uelewa tofauti. Na miongozo ya ya kuishi hapa sio tu ya kusaidia lakini ni muhimu kwa mafanikio.
Matakwa ya kwanza ni kukubali mabadiliko makubwa yanayotokea na kuwacha maelezo yawe wazi. Hutaweza kuwa na uwezo wa kuelewa. Akili yako inajua tu maisha yako ya hapo awali na ya zamani. Haiwezi kuakaunti linalojitokeza kwako, na impulses ambazo unahisi, na mwelekeo ambao polepole unaojitokeza ndani yako. Akili yako itajaribu lakini itashindwa katika kufahamu maana ya hii.
Baadhi ya watu hujaribu kurudi nyuma hapa. Wanataka kurudia kile walidhani kiliwapa hali ya usalama na utulivu na uhakika wa kibinafsi, lakini kwa bahati mbaya wameenda mbali sana sasa, majaribio hayo yataonekana kuwa tupu, yatawarudisha tu kwa maisha yao ya zamani iliyopatikana kuwa inakosa utimizo – inakukosa dhamira, maana na thamani. Sasa wanajiingiza katika safari ya aina mpya, na hawawezi kuifafanua.
Kwa hiyo, ruhusu mabadiliko hayo yatokee. Usijaribu kuyafafanua. Usitumie hata mawazo kutoka tamaduni zengine za kiroho kujaribu kuyafafanua. Ruhusu yawe ni ya fumbo, kwa kuwa kwako yatakuwa ni ya fumbo. Fumbo imo zaidi ya eneo la akili. Iheshimu. Ikubali. Fumbo sasa imeanza kujitokeza katika maisha yako, ambapo hapo awali ilikuwa imefungwa. Hapo awali, hapakuwa na mahali katika maisha yako ijitokeze, ikuongoze, ikubariki na ikukuandae. Sasa fumbo zimeanza kujitokeza. Basi wacha ijitokeze.
Utachanganyikiwa kuhusu kile unafaa kukifanya kuhusu mahusiano yako na watu, kimsingi, na pili, uhusiano wako na pale unapoishi, kazi unayofanya, shughuli zako, hobbies zako, maslahi yako na kadhalika. Wacha uchanganikio huu uishi. Ni wa afya. Ni wa kawaida. Ni sehemu ya mpito, unajenga daraja ya maisha mapya. Bado huishi maisha mapya kikamilifu. Unajenga daraja. Uko katika kipindi cha mpito. Mabadiliko huchanganisha kwa sababu unasonga kutoka uelewa mmoja hadi mwingine, kutoka kwa ufarisi mmoja wa maisha hadi ufarisi mwengine wa maisha. Mabadiliko ya maanisha kwamba huwezi kurudi nyuma, na  hujaenda mbali kutosha ili ufike mbele, kwa hivyo lazima uwe juu ya daraja hii, kupitia mabadiliko haya.
Wacha mustakabali uwe wazi. Weka kando mipango zaidi ya yale lazima uyafanye ili uweze kudumisha maisha yako duniani. Hapa lazima uwe na imani kwamba uhakika utakuja, na uhakika utakuja utakapoona uko tayari kusonga mbele na uko tayari kusonga mbele katika wilaya mpya. Lakini ukisita, basi, uhakika hautakuja. Ukijadiliana na kujaribu kufanya kazi nje ya mpango ili uweze kuweka kitu kutoka maisha yako ya awali, uhakika hautakuja. Uhakika hautakuja kwa sababu bado hujageuka hiyo kona. Ni kama jibu limo upande wa mlima, na lazima uzunguke ulima huo ndio uupate.
Hii inachanganya akili, lakini sasa akili lazima itumikie nguvu kubwa ndani yako, nguvu ile Mungu ameweka ndani yako ikuongoze na ikubariki na ikuandae kwa maisha haya makubwa. Bado lazima uwajibike kwa kile unachofanya na kile unachotumikia, kwa kile utajitolea katika maisha, katika jinsi ya unataumia muda na nguvu yako na kadhalika, lakini kuna kitu kikubwa kinachosonga ndani yako sasa.
Halafu, usiende kuwaambia marafiki wako wote na familia, kwa kuwa hawatafahamu. Isipokuwa mmoja wao amegeuka kona hii, watadhani umekuwa mjinga au watafikiri kwamba kitu kimbaya kimetokea kwako au umeshawishiwa na kitu ambacho ni tuhuma. Wanaweza hata kufikiri umekuwa wazimu! Kwa hivyo, lazima usiutangaze ufarisi wako vile iwezekanavyo. Kama una bahati, kutakuwa na mtu mmoja, iwe ndani ya familia yako kwa sasa au mtu utakutana naye atayekupa ishara usonge mbele.
Utataka kushiriki ufarisi wako mpya, na ugeni na uajabu wa mawazo hayo na dhana ambayo yatakuja kwako, na mabadiliko yale unahisia yanakukomboa kutoka siku zilizopita, lakini lazima uwe makini haswa kuhusu wale ambao unashiriki nao mambo haya, kwa kuwa wengine hawatafahamu, na ukosefu wao wa kufahamu na upinzani wao na hukumu itakuumiza na itafanya usijiamini.
Kutoka kuwa mtu anayeongozwa na kilicho nje kuwa mtu anayeongozwa na cha ndani ni mabadiliko makubwa, na mara ya kwanza utahisi una wasiwasi. Hutahisi kuwa una nguvu. Hutakuwa na hakika kuhusu unachokifanya. Utakuwa kama mmea mdogo zabuni katika msitu kubwa ambao lazima ulinzwe mpaka upate nguvu ya kutosha kusimama peke yake. Hivyo kuna hatari katika hatua hii ya mwanzo, katika sehemu hii ya kwanza katika sehemu hii ya mwanzo wa safari yako – mahitimisho ya mapema, indiscretion na watu wengine, kujishuku, jaribio la kujaribu kufafanua maisha yako – haya yote yana hatari kwa sababu yanaweza kuzuia uendelee, na wakati safari hii inaanza, lazima uendelee. Hii ni muhimu sana! Fikiria kuwa unapanda mlima mkubwa, basi, ukianza kupata mwinuko kidogo, basi, hutaki kurudi nyuma. Unahitaji kwenda mbele.
Knowledge ile Mungu ameweka ndani yako itakusihi uendelee, kuwa macho, kusikiliza kwa makini, kuwa mwaangalifu sana, kutia makini sana. Usidhani kuwa Mungu atakulinda kutoka kila namna ya madhara na kuzuia uumie na usikate tamaa na upate janga. Lazima utie makini sana. Hii ni sehemu ya kupata uelewa mkubwa. Hapo awali, haukutia makini. Ulikuwa reckless. Ulikuwa mpumbavu,na impulsive. Sasa ni lazima uwe mwaangalifu, mutambuzi, mvumilivu, makini. Katika kufanya hivyo, utaona jinsi umekuwa ukipoteza maisha yako, muda wako, nguvu yako, kwa shughuli zisio na maana na kwa mafikiro ambayo kamwe hayatasababisha azimio – kujishuku, kujihukumu, kuwahukumu wengine – mazungumzo makubwa ya juu juu yale watu wengi huendelea kudumisha karibu nawe.
Halafu, lazima ukukusanye rasilimali yako na kuhifadhi nguvu yako ili upate muda wa kuwa peke yako, ujifunze kutulia na kusikiliza. Unatafuta utulivu sasa zaidi ya sisimua. Utakuta kwamba shughuli za kijamii karibu nawe zitakukera, kwa maana unahitaji kitu kingine sasa. Unahitaji kusikiliza. Unahitaji kuwa na utulivu. Unahitaji kupata uhusiano mkubwa na nguvu hii inayojitokeza kutoka ndani.
Hii itabadilisha vipaumbele vyako. Hii itabadilsha tamaa yako. Hii itaathiri maamuzi yako. Na utakuta kwamba utakuwa tena hauna nia ya kufanya mambo na watu wengine ambayo hapo awali uliyafanya. Mambo yale kwa kweli kamwe hayatakupa utimizo, sasa utataka kuiepuka. Utaona utupu wao, na hautayataka, na yatakukera. Na utoto na purukushani ya mazungumzo ya watu, na hukumu yao ya mazoea dhidhi watu wengine, utakuta kuwa yanakukera. Hii ni asili.
Hii ndio inamaanisha kuja nyumbani kwako, kupata maadili yako halisi, vipaumbele vyako halisi, mwelekeo wako asili badala ya yale yote ambayo umeshawishiwa kuaamini. Utatafuta muda mbali na watu wengine. Utatafuta muda peke yake. Hautataka kuwa na kusisimua mara kwa mara. Unahitaji ujasiri wa kufanya hivyo. Watu wengi hawawezi kukaa zaidi ya sekunde tano kabla ya kuendeshwa nje yao. Hapa lazima ukukae na usikilize. Nadhari katika asili. Sikiliza sauti ya dunia, dunia ya kawaida.
Utaona hapa jinsi nishati yako yako – nishati ya akili na mwili wako – imekuwa ikitumiwa vibaya hapo awali, na utataka kuihifadhi, maana sasa unaihitaji. Sasa unakusanya nguvu yako. Unakusanya rasilimali yako. Hautupi maisha yako mbali. Unataka kuziba mashimo yote ambapo meli yako inavuja, ambapo  unapoteza msimamo wako kwa wengine au kwa hali-kwa njia ya tabia au kwa njia ya miundo ya wengine.
Ujumbe Mpya utakuzungumzia hapa, kwa maana una nguvu na ufumbo wa Mungu. Na ni nguvu hii na fumbo hii inakuvuta sasa, kwa kweli kinachotokea katika maisha yako ni Mungu anasonga ndani yako. Mungu anakusongesha. Lakini msongu huu ni uhuru kutoka kwa mambo yote ya awali. Lazima udisengage. Huwezi kuchukua maisha ya zamani katika maisha mpya, kwa hivyo ni unaendelea kwa njia ya kudisengage hatua kwa hatua. Sehemu ya kudisengage ni ya kimwili. Inahusu shughuli na mahusiano yako na wengine, lakini kwa kiasi kikubwa inahusu mambo ya ndani. Ni mawazo yako. Ni compulsions zako. Ni kile unafikiri lazima ukikufanyae Ni kile unafikiri lazima uwe au unapaswa kuwa nacho au jinsi unapaswa kuwa na watu wengine. Kwa kuwa hapa ndipo mashawishi ya kijamii kweli hufanyika.
Na kila siku unasonga mbele, unavunja minyororo. Mamlaka yake kwako inapunguka. Ukipanda mlima, mvuto wa tambarare unapunguka, na unapata uhuru na unahisi u mwepesi kutoka kwa mzigo na matarajio ya wengine na kwa mahitaji yako yale hayakuwa halisi kuanzia.
Wakati huu, punguza wakati ule unaotumia kwa  vyombo vya habari. Usisome vitabu vingi. Usiende sinema isipokuwa sinema hiyo ni inspirational, kwa maana unakusanya nguvu yako. Unaita nguvu kwako. Unahifadhi nishati yako. Unakisikiliza kwa makini kilicho ndani yako zaidi ya vile vilivyo nje. Unasonga mbali na Racket ya dunia. Iruhusu hii itokee. Ifuate. Iimarishe. Kwa maana hii ni mwendeko asili.
Kama urafiki wa dhati na hauwezi kukufuata sasa, itabidi uuwache, kwa upendo. Urafiki wenyewe utajitenganisha nawe, kwa sababu marafiki hao bado hawawezi kwenda nawe juu ya mlima huu. Unaenda mbali kuliko vile hao bado wanaweza kwenda. Umegeuka kona mabayo hao bado hawajageuka.
Jambo ngumu sana katika hatua za mwanzo ni wajibu kwa watu wengine, kwa marafiki wao, familia zao. Isipokuwa tu kwa wajibu wa kulea watoto wako, ambao ni lazima ufanye mpaka wawe watu wazima. Lakini kwa wengine wote, uhusiano wako sasa utakuwa katika mashaka. Pia itahitajika utoe huduma kwa mzazi wazee au mgonjwa, na hii ni sahihi. Lakini zaidi ya hii, unajenga utii wako kwa Mungu, na hii itatia utii wako kwa wengine na ngome kwako kwa mashaka. Kwa watu wengi, hii ni changamoto ngumu sana, Kizingiti kikubwa cha kwanza katika maandalizi yao.
Usijieleze kwa wengine. Sema tu kuwa kuna mikondo ya ndani zaidi katika maisha yako na unajaribu kuyafuata. Kuna mwelekeo ndani ya moyo wako na wewe unajaribu kuufuata. Waambie kwamba unahitaji muda peke yako, wakati wa utulivu, wakati wa faraghani, wakati wa utathmini. Usihisi kwamba lazima ujibu maswali. Sio lazima uwape majibu. Jipuri kutoka uchungu wa kujaribu kufanya hivyo.
Katika hatua ingine, itakuwa muhimu kwako ujifunze kuhusu njia ile Ujumbe Mpya umeutoa, kwa kuchukua hatua kwa Knowledge, kwa kusoma Hekima kutoka Jumuiya Kubwa, kujifunza juu ya Kiroho kutoka Jumuiya Kubwa. Hii itakuwa kama chakula kwako, chakula kwa moyo wako, chakula kwa nafsi yako. Utahitaji hii sasa kwa sababu itakupa nguvu na kuthibitisha mwelekeo mkubwa wa maisha yako. Itawapa uwazi zaidi, ufafanuzi mkubwa, na itakuonyesha kwamba kona hii uliopiga inawakilisha hatima yako na sio ajali katika maisha yako. Ni maisha yenyewe inayosonga ndani yako sasa. Na Ujumbe Mpya utaresonate na asili yako ya ndani zaidi, asili ambayo inayojitokeza polepole. Na hii italeta watu wapya katika maisha yako, watu ambao pia wanageuka kona na wameanza safari kubwa zaidi.
Ni muhimu hapa kuwa usiwe na imani imara. Huna haja ya kukubali imani imara. Unatafuta ufarisi wa ndani sasa. Ufarisi utakuwa msingi wako, sio imani imara. Unajitoa kutoka imani imara. Unaingia ndani ya eneo kubwa zaidi ya ufunuo na ufarisi wa asili. Kila mtu chini ya mlima anafuata imani imara, lakini imani imara haitakuwezesha kuupanda mlima huu, wala kupata mwinuko wa juu ambapo unaweza kuona ukweli wa maisha iliyo karibu nawe kama itakuwa dhahiri. Usifuate imani imara. Kama unahisi wasiwasi, kama huna uhakika, ni sawa, ni asili. Wacha maelezo yawe wazi. Usijiambatisha kwa seti nzima mpya ya imani. Hiyo ni sawa na kutoka gereza moja na kwenda kwa ingine. Oh, hapa ni mahali mpya! Lakini ni hali kama ya zamani. Oh, ni mpya na ya kusisimua na kutuliza, lakini ni hali ile ile ya zamani.
Ruhusu hatua zikufunulie kwa kweli safari hii. Sio safari ambayo inaeleweka kwa theorists au pundits au wanafalsafa, idealists, wasomi au wananchi kwa ujumla. Ni njia ya fumbo, safari ya ndani zaidi. Aya zake kitatokea zaidi ya eneo ya akili, kwa maana si safari ya kitaaluma. Akili yako itakomaa ili iweze kuelewa kwa kiasi. Na utajifunza kwa muda kupata mtazamo mkubwa na hekima kubwa kuhusu mambo mengi. Lakini sio safari ya kiakili, kwa kuwa akili ni uvumbuzi wa binadamu. Kile kilicho kuumba na kukuleta ndani ya dunia si uvumbuzi wa binadamu. Kile kitachokufunulia maisha makubwa ile unafaa kuishi na kutimiza si uvumbuzi wa binadamu. Lakini kinahitaji ushiriki wa binadamu, hekima ya binadamu, uwezo wa binadamu, imani ya binadamu, utambuzi wa binadamu ili kiweze kujitokeza.
Hapa hutoi nguvu yako yote kwa Mungu, kwa kufikiri kuwa Mungu atakuongoza katika kila kitu. Hiyo ni ujinga! Hapa unajitolea kwa mamlaka kubwa ndani yako ile sio ya uvumbuzi wako, lakini mamlaka hii inahitaji uwajibike, uwe mwaaminifu, uweze kuamua maisha yako. Itahitaji ufuate mambo ya fumbo, lakini mara nyingi utakuwa ukifanya mambo ya kawaida.
Kama uko katika uhusiano na una watoto, usifanye hatua yoyote kwa ghafla katika maisha yako. Kwanza jenga nguvu hii. Jenga uhusiano na Knowledge ndani yako. Jifunze kusikiliza. kuwa na wakati wa faraghani. Fuata mwelekeo wa asili yako. Shiriki sehemu tu ya fumbo na mume wako au mke, kwa maana labda hawatakuwa na uwezo wa kuelewa. Waulize wakupe wakati huu na imani hii, kwa kuwa kuna mambo yanayojitokeza ndani ya moyo wako. Dumisha wajibu wako na majukumu, lakini chukua muda wa kuwa pamoja na Knowledge ndani yako. Chukua muda wa kuchukua hatua kwa Knowledge, wa kujifunza Hatua kwa Knowledge na kujiweka katika nafasi ambapo hatua zitaweza kufunua ukweli wao mkubwa kwako.
Waambie watoto wako kwamba kuna nguvu kubwa ndani yao ambayo itawaongoza na itawalinda kama wataisikiliza. Shirikiana nao katika ufahamu wako. Lakini usijaribu kushiriki kila kitu, kwa maana unajenga nguvu, ukijaribu kushiriki kila kitu, unapeana nguvu yako. Usijaribu kutunza watu wengine zaidi ya watoto wako au mzazi mzee hapa, kwa maana unapata nguvu ndani yako. Unajifunza kuhifadhi nishati yako. Unajishikilia usijitolee kila mahali, unajishikilia ndio usipeane nguvu yako.
Usifanye maamuzi yoyote kwa ghafla kuhusu mahusiano yako ya msingi kama umeoa au umeolewa na watoto, kwa kuwa katika kesi nyingi itakuwa mapema. Ndoa hapa itakuwa katika changamoto. Mambo mengi ndio yataweza kuamua kama ndoa itaweza kuendelea, na huwezi kuwa na uwezo wa kuyajua mambo haya katika wakati huu.
Kazi yako ni kufuata uibuka wa Knowledge ndani yako, kuitumikia, kuipokea, kujivuta ndani, kuchukua muda unaochukua hadi uibuka mkubwa utokee ndani yako. Na usiwe na papara, kwa maana utaibuka wakati wake mwenyewe. Bado hutambui ukubwa wa kile kinachotokea au ukubwa wa uwezekano kwa nyakati zijazo.
Punguza mvuto ulio karibu na wewe. Kuwa kimya na wale wanajitembeza au wale wanahukumu dunia. Usijadili na wengine katika hatua hii. Usishindane na wengine. Usibishane kuhusu masuala. Usitetee mawazo yako. Kwa maana kwa sasa haya sio muhimu na yatakuwa counterproductive kwako.
Nguvu na uwepo wa Knowledge unajitokeza kwako. Hii ndio jambo la muhimu sana. Unajifunza kuwa na nguvu na kufuata mwelekeo wa ndani. Hii ndio jambo la muhimu sana. Dumisha majukumu yako. Jitolee kwa watoto wako. Lakini shikilia hii kama jambo la muhimu zaidi, hatimaye uhusiano wako mkubwa ni uhusiano wako na Mungu. Wajibu wako mkubwa ni kwa Knowledge ile Mungu ameweka ndani yako uijibu, uifuate na uieleze. Hii ndio uhuru usiyoweza kulinganishwa, lakini unahitaji nguvu kubwa ya ndani na uvumilivu.
Hizi ni miongozo za hatua za mwanzo. Zaidi ya hii, lazima ujifunze kujenga nguzo nne za maisha yako-Nguzo ya Mahusiano, nguzo ya Kazi, nguzo ya Afya na nguzo ya Maendeleo ya Kiroho. Lazima ujifunze kuhusu Jumuiya Kubwa. Lazima ujifunze kuhusu Mazingira ya Akili. Lazima ujifunze kuhusu mahusiano na madhumuni ya dhamira kubwa. Haya yote yanakusubiri. Lakini kwanza ni lazima ujenge msingi, bila msingi huu, huwezi kuwa na uwezo wa kupenya maana zaidi, umuhimu na matumizi ya Ufunuo hizi zilizomo ndani ya Ujumbe Mpya kutoka kwa Mungu.
Msingi ni muhimu sana na unahitaji uvumilivu mkubwa na forbearance. Ni uvumilivu huu na forbearance ambao utahamisha utii wako kutoka kwa akili yako na maonyo ya wengine kwa Nguvu Kubwa ndani yako – nguvu ya Knowledge, nguvu ya Mungu. Kamwe hutaweza kuielewa nguvu hii kikamilifu. Kamwe hutaweza kuidai kwako mwenyewe. Kamwe hutaweza kuwa sahibu wake. Kamwe hutaweza kuitumia kwa kujaribu kuwa bora kuliko wengine. Huwezi kuitumia kukipata unachotaka . Huwezi kuitumia kupata utajiri na nguvu na radhi. Unaweza tu kujifunza kuifuata na kujifunza kufunga safari kubwa juu ya mlima uliotayarishwa kwako.

Kushuhudia Ufunuo

Mtume yuko dunia. Yeye ameuleta Ujumbe mkubwa kwa binadamu, Ujumbe ambao amekuwa akiupokea kwa zaidi ya miaka 25, ujumbe wa kina la kutosha kuongoza ubinadamu katika hatua ya pili kubwa ya mageuzi yake na maendeleo.
Yeye ni mtu wa kawaida, lakini katika muonekano tu. Kwa maana yeye anabeba mbegu ya uelewa mkubwa na Ukweli Halisi Kubwa – ukweli halisi wa maisha katika ulimwengu; ukweli halisi wa dimension kubwa ya kiroho cha dunia na kwingineko; ukweli halisi wa dhamira, maana na mwelekeo, ukweli halisi wa uwasiliano na uwepo wa Malaika, ambao uwajibu wao ni ustawi na maendeleo ya familia ya binadamu.
Watu wengi watajaribu kumukana. Watu wengi watamhukumu au wataanza kumdhihaki. Ni nani atamusimamia? Ni nani miongoni wenyu atashuhudia Ufunuo? Nani kati yenu ana nguvu ya kutosha, ni jasiri kutosha na mwaaminifu wa kutosha kufanya hii?
Uwepo wa Mtume ni wa thamani kubwa duniani. Yuko katika mazingira magumu. Kutakuwa na makundi mengine na watu binafsi ambao watajaribu kumwangamiza Tangazo yake ikitambuliwa zaidi na kugunduliwa zaidi duniani.
Ni nani atashuhudia ufunuo?
Watu wanataka mambo mengi kutoka kwa Muumba wa maisha yote. Na watu wanataka mambo mengi kutoka kwa Mtume aliye tumwa, Mtume peke yake katika dunia ya leo na siku mingi ijayo.
Watu wanataka miujiza. Watu wanataka kuokolewa kutoka mazingira yao. Watu wanataka kupewa neema na dispensations. Watu wanataka kutumikiwa. Watu wanataka kutiwa na nguvu. Watu wanataka ushindi katika vita na ustawi kwa amani.
Wataleta matarajio haya kwa Mtume, hasa kwake. Lakini anaweza tu kupointi kwa Ufunuo, ambayo ni ya kina na ya uelekevu zaidi kuliko vile watu wengi wanatambua na itahitaji ushiriki mpana na utambuzi, mazoezi zaidi na matumizi iliyo aminifu.
Ni nani anaweza kuzungumza kwa niaba yakei? Ni nani anaweza kusahihisha makosa mengi ambayo hutokea kwa sababu ya tangazo hilo? Hata miongoni mwa wale ambao watajibu vyema, kutakuwa na matarajio isio sahihi. Kutakuwa na madai hazitaelezwa.

Kutakuwa na laumu na hukumu kuwa Ujumbe na Mtume hatimizi matarajio ya watu. Ni nani atazungumza kwa niaba yake?
Ujumbe na Mtume zinahitaji mashahidi wengi. Zinahitaji mwelezo mkubwa wa utambuzi na dhamira. Kwa wale ambao hii ni hatima yao, ni jambo muhimu mno katika maisha yao.

Wakati wataondoka dunian na kurudi kwa familia zao za kiroho, watauliza, “Je ulizungumza kwa niaba Mtume? Je, ulimutambua Mtume? Je, ulimusaidia Mtume?”
Itakuwa ni tukio kubwa na nafasi muhimu zaidi katika maisha yao. Ni nani anaweza kujibu hii? Ni nani anaweza kutambua hii? Ni nani anaweza kuwajibika hapa, tukio kubwa ile wataweza kuwa nayo?
Watu wanataka mambo mengi, lakini kinachotakiwa kutoka kwao ni kitu kingine. Wakati wa Ufunuo, vipaumbele hubadilika. Hii ni tukio ambalo hufanyika tu kila milenia, na wewe sasa uko duniani katika wakati huu.
Utaona Mtume ananyanyaswa na kudharauliwa na kuudhiwa. Ni nini atawaambia, ambao ni walengwa wa Ufunuo Mpya kutoka wa Mungu? Ni nini itakiita mbele kilicho ndani yako, ambaye amepewa heri na heshima ya kupokea Ujumbe Mpya kwa binadamu na kuwa miongoni mwa wale wa kwanza na wapokeaji wa mwanzo?
Kama huwezi kuhisi na kuona mambo haya Sisi tunasemea, basi akili yako inaenda wapi? Ni nini inaweza kuwa muhimu zaidi kuliko hii? Furaha yako? Usalama wako? Idhini yako kutoka kwa watu wengine? Msimamo wako kwa kijamii? Hili ni swali na mtanziko kwa kila mtu ambaye anaweza kujibu.
Kama wale wanaopinga Mtume watakuja kwenu na kusema, “Ni nini unaamini? Msimamo wako uko wapi?” Ni nini utasema? Kama Mtume anakanwa au kupuuzwa au kuudhiwa, utasema nini hapa?
Watu wana nia ya kupokea baraka na faida ya Ufunuo, lakini faida hii iko pamoja na jukumu, uwezo wa kujibu. Unawaita wawe mashuhudi na sio tu wapokeaji – kufanya mazoezi peke yao kwa siri, kwa siri kama wamejificha mahali duniani.
Ni nani anaweza kuutetea Ufunuo wakati changamoto itakuja? Ni nani atazungumza wakati Ujumbe na Mtume wanashambuliwa na wale walioonekana kuwa wana heshima na august katika jamii wakilaani mteule wa kuleta ufunuo wa Mungu duniani?
Ni nini utahisi na kufikiri wakati unaona wale ambao unawaajabia, wale ambao unawaheshimu, wakigeuka Ufunuo? Je hii itakutia katika shaka na fujo? Je itafanya ujisikie u mdhaifu na asiye na matumaini?
Angalia historia. Kuna Mitume yeyote mkubwa ambaye amewahi kukumbatiwa nchini katika wakati wao au kama wale walio karibu nao wakaelewa kwa mafanikio?
Kama Mtume angepata madaraka ya kisiasa, oh, bila ya shaka kungekuwa na visasi vingi. Oh, bila ya shaka, kungekuwa na mipango mengi. Oh, bila shaka, ingeonekana kama wengi wanamfuata, wakitaka kuwa upande wa kushinda katika migogoro. Naam, wengi wangefika, wakimsifu na kumutabua Mtume, kwa maana wangekuwa wanatafuta faida kutoka kwa uwepo wake na nafasi yake. Naam, mawaziri waaminifu wangeonekana. Naam, watu wangeweza kuamka na kushauku.
Na hiki ni kitu gani kwa Mtume, kuwa na ufuatia mkubwa wa watu ambao hawaelewi, ambao matarajio yao sio sahihi, ambao visasi vyao sio aminifu, ambao heshima na urai ni ya uongo na unaharibiwa kwa urahisi na wengine? Ni nani atashuhudia kulingana na nguvu ya Knowledge, akili zaidi ndani yao?
Katika hatua hizi za mwanzo za tangazo, Mtume atapuuzwa. Yeye atahukumiwa wazi, watu watamukosoa kwa ukali – ataitwa ibilisi na kuitwa mpumbavu, ataitwa mpotovu, ataitwa mambo mengi na wale ambao hawawezi au hawataki kujibu, atahukumiwa na wale ambao tu wanatafuta kulinda na na kuhifadhi nafasi yao ya sasa na uwekezaji wao wa awali, na wale ambao hawana ujasiri wa kuhoji visasi vyao, imani yao au mawazo.
Na, oh, Wataalamu hawatakuwa bora, wale wametia juhudi kubwa sana kwao wenyewe na kulipwa bei kubwa na wamefanya maafikiano mengi kupata nafasi yao ya mamlaka katika jamii. Je, watahatarisha haya yote na kutambua mtu ambaye ana utambuzi mdogo, mtu ambaye ana ufuataji mdogo sana, mtu ambaye Ujumbe wake unaonekana ni wa ajabu na ambaye matangazo yake yanakataliwa na yanaleta chuki?
Je Wataalam hawa watahatarisha sifa zao, nafasi yao ya kijamii, ajira yao, kushuhudia Ufunuo? Je wanasiasa watahatarisha uwekezaji wao – msimamo wao, mafanikio yao – kwa kutambua Mtume?
Hapana, unaweza kuona, mzigo huu uko juu yako na wengine, wengine wengi. Usiangalie wasomi au wenye heshima kuhatarisha nafasi yao ili washuhudia Ufunuo. Usidhani kwamba Mtume tu anhitaji kuwa katika mahusiano na baadhi ya watu wenye nguvu, maana utacheza role ya Judas – kwa nia njema, pengine, lakini kwa upofu na ukweli wa hali hii.
Mtume ana kifunguo cha mustakabali wa ubinadamu na mafanikio ya siku zijazo. Ni nani atashuhudia hii? Ni nani atashikilia nafasi hii, nafasi ambayo dunia haiheshimu au haitambui?
Watu wengi watakuja, wakitaka vitu vingi. Kutakuwa na nodi ya vichwa na nyuso za kutabasamu, lakini ni nani ambaye atashahudia hii?
Wewe ambaye unatafuta dhamira na maana katika maisha yako budi uelewe kuwa hatimaye hii ndio maana yake –  kwamba lazima usimamie kitu kikubwa zaidi kukuliko, kubwa kuliko maslahi yako binafsi au faida, kubwa kuliko inurement yako ya kibinafsi. Lazima usimamie kitu kikubwa ukikabiliwa na upinzani, ukikabiliwa na ujinga na upumbavu na kukataliwa.
Hii itakuita nje ya vivuli. Hii itakuita nje ya kujinyima kibinafsi. Hii itawaita wengine kutoka kwa kuwepo yao duni, na ya siri. Hii itatoa watu nje ya kukosa kujithamini. Hii itatoa watu  nje ya kujishuku kibinafsi na kujikana kibinafsi, wito sasa wa kushahudia kitu kikuu, kitu kikubwa, kitu cha kina na cha ufanisi, kitu ambacho ubinadamu unahitaji lakini hauwawezi kukitoa kwao wenyewe.
Kwa wale wote ambao wanaweza kupata baraka za Muumba sasa, hatimaye,lazima wakabiliwe na maswali haya. Hawawezi tu kuwa katika sehemu ya kupokea – wakitaka zengine, wakitarajia zengine na kushukuru – hao pia lazima wapande katika nafasi ya kujieleza kibinafsi. Hao pia lazima watetee kile ambacho kinawahudumia. Hao pia lazima wahatarishe hofu yao na mashaka yao ya kibinafsi kufanya uelezo mkubwa kwa wengine. Hao pia lazima wakabiliane na kukataliwa na kijamii.
Ni asili ya wito wao. Hakuna wito au kusudi ambayo haihusiki na baadhi ya mambo haya. Huwezi tu kutangaza madhumuni kwako mwenyewe na kuishi kwa furaha milele kwa milele. Huwezi tu kujibu wito wako na halafu kila kitu kinaenda njia yako.
Kutumikia dunia, lazima ukabiliane na dunia. Lazima uwe na ujasiri wa kukabiliana na dunia na hali halisi yake. Lazima ujenga nguvu ndani yako ya kufanya hivyo na kuchanga kitu duniani ambacho dunia haiwezi kujichangia, kitu ambacho ni muhimu ambacho hakipatikani, jambo ambalo watu wengine hawawezi kufanya au hawataki kufanya. Usiahirishe kwa wengine hapa, kwa maana ni wewe ambaye unaitwa.
Hii ni maana ya wito – dhamira na wito. Kuitwa ni kuitwa nje ya yale ya kawaida, nje ya maeneo unaishi, nje ya kile kila mtu anafanya, anafikiri na ana wasiwasi nacho, ni hatua nje ya mstari, ni kuitwa mbali na maisha yako ya kawaida kwa kutosha ili uwe na uwezo wa kupata hekima kubwa na ufunuo.
Dhamira kubwa basi ni nini ila kuchukua nafasi kubwa zaidi ya shughuli zako za kawaida na kutumikia kitu ambacho kimo zaidi ya maslahi ya kibinafsi na kujiinua kibinafsi? Kujibu Ufunuo basi ni maandamano kamili ya mambo haya.
Kwa kuwa wale ambao hawawezi au hawataki kushuhudia Ufunuo, vile ikuavyo hawana nguvu kubwa  wanayohitaji na hawana nguvu ya kutosha ya Knowledge, au wanaogopa kukivuka kizingiti ili waweze kuwa wawasiliana wa kweli duniani badala ya kuwa mtu ambaye amejitoa katika dunia na ana hofu kwa duniani na ni anajaribu kuyalinda yale aliye nayo kutoka duniani.
Sio kila mtu aliye tayari kufanya hivyo katika wakati huu, lakini hii ndio njia ambayo kila mtu ataifuata. Unasimamia kitu fulani. Na maandamano yako lazima yawe ya kweli na siyo tu ya kisaikolojia. Ni lazima ikamatike na si tu katika eleo ya mawazo. Lazima ufanye kafara kwa sababu yake. Lazima uwache mambo kwa sababu yake. Lazima uhatarishe  mambo kwa sababu yake. Na hii ndiyo inatofautisha wale ambao wito wao ni wa kweli na wenye nguvu kutoka kwa wale ambao wanajifanya au ni dhaifu mno kuweza kutoa jibu kikamilifu.
Mtume yuko duniani. Ni nani atamushuhudia, kulingana na nguvu ya utambuzi wao? Ni nani atachukua nafasi ya kuzungumza na wengine? Ni nani ataruhusu maisha yao iwekwe katika fomu ingine na Knowledge, ataruhusu vipaumbele vyake vibadilike kwa kawaida, ataruhusu mawazo yake yawe sare, ya nguvu na ya kupenya? Ni nani ataruhusu maisha yake ibadilishwe na apitie vipindi hivyo vya kutokuwa na uhakika kwa kuwa hiki kitahitajika njiani?
Hakika sio  mtu yule ambaye lazima ahisi kwamba lazima awe katika udhibiti wakati wote, ambaye uhakika wake una msingi kutoka kwa nguvu ya imani yake na mawazo na uimara wa maisha yake. Hana imani au uaminifu wa kibinafsi wa kupitia mchakato wowote halisi wa maandalizi, ambayo itawaleta katika hali ya kutokuwa na uhakika na kuvunja regimentation yake ya uongo na madhara.
Waroho hawatafanya kazi hii, kwa maana inhatarisha mambo yale wanajaribu kuyapata. Watajaribu kutumia ufunuo wa Mungu kujitajirisha kisiasa, kijamii, kiuchumi, hata kiroho. Lakini hawatakuwa watetezi wa kweli. Hawatamushuhudia Mtume kwa sababu wanataka kila mtu awashuhudie.
Hii sio hamu au nia ya Mtume, kuvuta nadhari ya watu kwake. Yeye ni mtu mnyenyekevu. Hatafuti utambuzi kama huo, na hii ni sehemu moja ya sababu yeye alichaguliwa kuwa mwakilishi wa Mungu katika enzi hii ya maendeleo ya binadamu.
Watamani na waroho kamwe hawachaguliwi, kwa maana hao sio waaminifu. Hawana utambuzi au uaminifu wa kibinafsi kwa kuchukua uwajibikaji mkubwa. Unyenyekevu ni matunda ya uaminifu na huruma, mambo mawili ambayo waroho bado hawamiliki.
Kweli lazima Mtume achinjwe katika mikono ya upinzani wakati wafuasi wake wa kweli wanabaki bubu, wanakimya na ni wadhaifu? Je Ufunuo Mpya utaharibiwa na utakanwa wakati wale ambao wanachaguliwa kuwa mashahidi wake wanakaa kimya na kuwa withdrawn, wanajihofia?
Kufikiri Mtume anaweza kuwasiliana kila kitu na kujibu kila kitu ni kuuweka mzigo ule hauwezekani kwake, kwa kuwa yeye ni lazima awe na washahidi wengi katika sehemu nyingi. Na ni lazima wawe makini kama wanaishi katika nchi ambazo zina ukandamizaji wa kisiasa au kidini. Lazima wafanye mazoezi ya utambuzi mkubwa na busara pale ambapo wanashiriki Ufunuo.
Kifodini sio mkazo hapa. Ni mawasiliano. Ni uhusiano. Ni kueneza Ufunuo – juu ya ardhi au chini ya ardhi, kutegemeana na mazingira ya kisiasa, kijamii na kidini ambapo wanaishi.
Lakini mawasiliano na uhusiano lazima iongezewa na ipanuliwe. Haitoshi kuwa muumini wa dhati, kwa kuwa lazima itafsiriwe kwa vitendo, sio tu kwa kufanya maisha yako upya na kuichunguza tena, lakini pia na kuwa ushahidi kwa yale ambayo ni chanzo cha marejesho ya ajabu ya mtu.
Hii itatenganisha washiriki wa kweli kutoka kwa watu wengine ambao ni wadhaifu mno na hawezi kuepuka wasiwasi wa kibinafsi.
Basi wacha hii iwe msingi wa uelewa wako wa wengine ambao wanaojibu. Kitu muhimu ni kile ambacho wanakifanya, sio kile wanachokisema au kukitangaza katika wakati fulani. Wataruhusu maisha yao kwa kweli ibadilishwe, itengenezwe kulingana na Ufunuo na kwa nguvu ya Knowledge ndani yao? Watashuhudia Mtume kama kitendo cha mchango wa papo kwa papo na asili? Ama watabaki nyuma wakipanga jinsi wanaweza kufaidika bila kulipa bei yoyote au kuchukua tahadhari yoyote?
Hii ni sehemu ya mzigo wa Mtume, maana hata miongoni mwa wale ambao wanaonekana wanajibu vyema, bado kuna hatari. Mmoja ambaye atamsaliti Mtume atatoka kwa safu ya wafuasi wake. Mwanafunzi asiyeguswa au aliyeshindwa, badala ya kuchukua jukumu kwa matatizo na mapungufu yao wenyewe, watamukana au kupunguza Ujumbe na Mtume. Hili hutokea mara yote katika wakati wa Ufunuo. Utaona hili likitokea.
Jibu lako kwa Ufunuo ni jibu kwa maisha na Chanzo cha maisha. Linaonyesha uwezo wote wako na udhaifu wako. Linaonyesha mvuto ule wa maisha yako ulio wa faida na wa hatari, katika kukabiliana na Ufunuo, hakuna ardhi neutral. Hii inapolarize watu, kama vile inafaa, kama vile ni lazima, kwa sababu lazima kuwe na matokeo. Kwa mtu ambaye anaonekana hajaguswa au hana haja na Ufunuo basi, huo sio msimamo ulio neutral.
Fikiri wale ambao walishindwa kujibu wakati wa Mitume wakubwa katika siku za kale. Nini walikuwa wakifikiri? Ni kwa namna gani ambayo hawakuweza kuona yaliyo mbele yao? Ni kwa namna gani kuwa hawakuweza kutambua mmoja ambaye aliwaletea ahadi ya maisha makubwa? Ni kwa namna gani waliweza kusimama na kuruhusu Ujumbe na Mtume wawe denigrated?
Aidha neutrality yao ni uelezo wa woga mkubwa, au hao ni wafu kwao wenyewe na kwa dunia, na hawawezi kujibu. Hawawezi kuwajibika, kwa maana hao hawawezi kujibu.
Mtume lazima atangaze ujumbe Mpya na lazima atambua kile ambacho kinaharibu ustaarabu wa binadamu na mustakabali wa binadamu na uhuru. Mengi ambayo atayasema yatakuwa changamoto sana. Ni yatakutia wasiwasi kwa sababu hivyo ndivyo Ufunuo hufanya; inakutia wasiwasi.
Ufunuo huleta uthibitisho na wasiwasi kwa sababu unahitaji ubadilike. Unahitaji ufikirie maisha yako, ahadi yako na shughuli zako upya. Ni changamoto, sio tu faraja.
Shinikizo iko kwa mpokeaji, sio vile atajibu mara moja, lakini vile atajibu. Jinsi atajibu itasema kila kitu kuhusu mazingira yake, hali yake ya akili na jinsi anajithamini.
Hebu kuwe na mashahidi wengi wa Ujumbe na Mtume. Hebu kuwe na wengi ambao wanaweza kujibu na kupokea zawadi ya maandalizi na kuiitia katika maisha yao na dhamira ya kweli na huruma.
Hebu dunia isikie kile Ufunuo unasema. Waache wasikilize Sauti ya Ufunuo. Wajibu Mtume kwa njia yoyote ambayo wanaweza.
Kuwa gari ya hii, na maisha yako itakuwa adilifu, na dhamira yako itatimizwa, na matunda ya mateso yote na mafanikio yako yote yatakuwa na maana kubwa na thamani kubwa kwa dunia.

Mungu anaongoza binadamu katika mwelekeo mpya

Mungu anaongoza binadamu katika mwelekeo mpya, mwelekeo ambao binadamu hajawai kuupitia. Kwa kuwa dunia imebadilika na binadamu anakabili Jumuiya Kubwa ya waangavu ulimwenguni – mabadiliko makubwa, kizingiti kikubwa katika evolution ya binadamu, wakati wa mageuzi makubwa na wasiwasi, wakati wa hatari kwa familia ya binadamu, wakati ambao utasonga kwa haraka na matukio yatayojitokeza kwa haraka.

 

Mungu anaongoza binadamu katika mwelekeo mpya, katika mwelekeo wa jamii ya dunia ambayo ina uwezo wa kuendeleza dunia na kukabiliana na hali halisi ya maisha katika ulimwengu, ambayo itabidi mukabiliane nayo na hata kwa sasa munalazimishwa kukabiliana nayo.

 

Ni mabadiliko makubwa ambayo watu wengi wanayahisi lakini hawayaelewi. Harakati ya dunia inatokea kwa kasi, ambapo maisha ya watu itakuwa ya kuzidiwa na ya kushindwa katika mabadiliko makubwa ya mazingira ambayo yanajitokeza kwa njia ya mageuzi ya kisiasa na kiuchumi.

Haya yote sasa yako katika mwendo na hayawezi kupunguzwa, inaweza tu kuwa tu kuwa mitigated. Hapa watu wanaweza tu kukabiliana nayo.

Ni katika kizingiti hiki kikubwa katika historia ya binadamu kuwa Ufunuo Mpya umemtumwa duniani, na Mtume ametumwa hapa kuupokea, kuuandaa Ujumbe huu na kuueleza. Kwake, safari hii ilikuwa ndefu, safari ndefu na ngumu.

Ujumbe wa ubinadamu sasa ni mkubwa, ni mpana zaidi na ni kamilifu zaidi kuliko Ujumbe wowote uloyowahi kumtumwa duniani, kamili na mafundisho na ufafanuzi ili hekima yake na Knowledge yaweze kuonekana na kutumiwa ipasavyo na si tu kuachwa kwa utafsiri wa binadamu.

Watu hawaoni, hawasikii. Hawajijui wenyewe. Na ujuzi wao wa asili wa kutambua mazingira, kwa wengi, umepotea na haujakuzwa.

Hii inafanya kazi ya Mtume iwe ngumu zaidi. Yeye lazima abebe fumbo, kwa kuwa Ufunuo umo zaidi ya eneo la akili na kwa hakika hailinganishwi na matarajio ya watu, imani au ufahamu.

Mungu anaongoza dunia katika mwelekeo mpya. Ni mwelekeo ambao ulikuwa ni hatima ya binadamu, lakini utakuwa mpya kwa watu wa dunia. Utakuwa mpya kwa uelewa wao.

Mafunuo yote kutoka kwa Muumba daima huwa kama hii. Yote huwasilisha ukweli mpya, mwamko mpya, mwelekeo mpya na ahadi kubwa zaidi.

Giza inaongezeka duniani, na ahadi hii kubwa zaidi inahitajika sasa. Ni mwangaza wa Knowledge peke yake, akili kubwa ile Muumba ameitoa kwa familia ya binadamu na kwa jamii zote ulimwenguni, inaweza sasa kuwawezesha muelewe na mujibu.

Kwa kuwa unarudi kwa Mungu kwa masharti ya Mungu, Ujumbe wa Mungu lazima ueleweke, kama vile ulivyo na vile lengo lake liko.

Kutakuwa na mapambano na ubishi kuhusu haya, na Mtume na wafuasi wa Mtume lazima wakabiliane na ugumu huu, kuchanganyikiwa huku na wawe na uvumilivu mkubwa.

Ufunuo kama huu hautakubaliwa hapo awali, na ni wachache tu watakuwa na uwezo wa kujibu kabisa. Lakini wakati ukiendelea na dunia ikizidi kuwa na matata, Ujumbe Mpya utapata kivutio kikubwa, utambuzi mkubwa na umuhimu mkubwa.

Unayajibu maswali ambayo bado hamujajifundhisha kuyauliza. Ni maandalizi ya mustakabali na pia tiba ya wakati wa sasa.

Wanafalsafa na wanateolojia wenyu hawatajua cha kufanya na ujumbe huu. Watakuwa na masuala na Ujumbe huu. Hautaendana na uelewa wao, ule ambao wamewekeza wakati yao.

Viongozi wa dini watateta dhidi yake kwa sababu inaongea kuhusu ukweli ambao hawajatambua.

Mungu anaongoza bunadamu katika mwelekeo mpya.

Mtume yuko hapa kutoa Ufunuo. Imemuchukua miongo kuupokea. Itachukua miongo kadhaa kutambuliwa duniani.

Lakini tatizo ni wakati. Binadamu hana muda mrefu wa kujiandaa kwa dunia mpya na kwa Mawasiliano na maisha katika ulimwengu – Mawasiliano ambayo tayari yanatokea, Mawasiliano ya kusudi na nia hatari.

Watu wako obsessed na mahitaji yao, masuala yao, tamaa yao na matakwa yao. Hawaoni harakati ya dunia.

Kwa kua dunia imebadilika, lakini watu hawajabadilika nayo. Na sasa munakabiliwa na seti mpya ya ukweli.

Ni nini Mungu atasema kuhusu haya watu wakihisi kuzidiwa, kama unabii wao wa mustakabali hautatokea, kama kurudi kwa mwokozi wao hakutafanyika, kama wanaamini kuwa Mungu anajenga matatizo haya yote kwao?

Ufunuo unasemea haya yote, lakini lazima muwe wazi kwa Ufunuo, na lazima mukabiliane na matarajio ya mabadiliko makubwa, kwa kuwa mabadiliko haya tayari yamo kwenyu na kwa dunia, na yatazidi kuendelea.

Hamuwezi kurudi nyuma maelfu ya miaka na kujaribu kutafakari yanayotokea leo, kwa kua mageuzi ya binadamu yamehama katika sehemu mpya, sehemu ya kuhodhi duniani na sehemu ya mazingira magumu ulimwenguni.

Mafundisho ya kutayarisha binadamu kukabiliana na dunia mpya na Jumuiya Kubwa yataanza wapi – matukio mawili ambayo yatabadilisha mwelekeo wa historia ya binadamu na kuathiri kila mtu?

Serikali haijui. Viongozi wa dini hawajui. Wataalam hawajui. Vyuo vikuu haviwezi kuandaa watu.

Ufunuo lazima utoke kutoka kwa Muumba wa maisha yote, na tukio hili ndilo linatokea sasa, kwa kuwa munaishi katika wakati wa Ufunuo na Mtume yuko duniani.

Kama bado yuko duniani muna fursa ya kujitayarisha.

Akitoka duniani, hali itakuwa tofauti. Itakuwa ngumu.

Kwa haya, yeye ni mwangaza duniani.

Yeye ni mtu mnyenyekevu na hana madai yoyote ila kuwa Mtume, kwa kuwa hii ndio ile kazi aliyopewa.

Lazima atayarishe ubinadamu kukabiliana na dunia mpya kupitia njia ya Ufunuo.

Lazima atayarishe ubinadamu kukabiliana na Jumuiya Kubwa kupitia njia ya Ufunuo.

Lazima azungumze kuhusu mabadiliko makubwa yanayokabili binadamu na tayari yanakabili watu kila mahali kupitia njia ya Ufunuo.

Mungu anaongoza binadamu katika mwelekeo mpya.

Je, ubinadamu unaweza kusonga?

Je, ubinadamu unaweza kujibu?

Je, unaweza kujibu?

Unaweza kukubali kuwa unaishi katika wakati wa ufunuo na kufikiri maana ya hii kwa maisha yako na changamoto ambayo inaleta kwa maisha yako?

Watu hawatambui kiasi ambacho hali ya maisha na mazingira yao inategemea hali ya dunia na harakati ya dunia.

Ni katika mataifa maskini ambapo haya yote yamo wazi.

Katika mataifa tajiri, utajiri unawalinda kutokana na ukweli wa maisha kwa kiasi fulani na kwa muda fulani. Lakini utajiri huu utaisha, na ukweli mkubwa tayari umo nanyi.

Uamuzi utatokana na jinsi ubinadamu utajibu.

Uamuzi utatokana na kile ambacho kitatoa taarifa kwa watu binafsi.

Ni sauti gani ambayo wataisikiliza, kama itakuwa sauti ya nguvu na uwepo wa Knowledge ile Mungu amewapa iwaongoze na iwalinde, ama kama itakuwa sauti ya utamaduni wao ama sauti ya hofu au sauti ya hasira au tamaa.

Uchaguzi ni msingi kwa mtu binafsi, na kwa kile watu watachagua kitaamua hatima na mustakabali wa binadamu.

Kwa hivyo uwajibika ni wa kila mtu na sio tu viongozi na taasisi.

Hii ndio sababu Mungu anatoa Ujumbe Mpya kwa watu na sio kwa viongozi wa mataifa.

Kwa kuwa viongozi hawana uhuru. Wamefungwa na ofisi zao na wale ambao wamewachagua, na matarajio ya wengine.

Hii ndio maana ufunuo unakuja kwako wewe na kwa watu. Ni uchaguzi wao na uwezo wao ambao utatoa uamuzi.

Watu wanataka vitu vingi. Hawataki kuyapoteza yale wanayomiliki. Wanaishi kwa wakati wa muda mfupi. Hawana mtazamo wa kuona mahali maisha yao inaenda.

Ufunuo utakuwa wa mshtuko mkubwa na changamoto kubwa kwa kila mtu, lakini mshtuko huu na changamoto ni mshtuko wa Ufunuo. Na changamoto hii inakabiliwa ni mapenzi ya Muumba. Na changamoto ni kuona kama unaweza kujibu na asili ya majibu yako.

Huwezi kusimama mahali upo, kwa kuwa dunia inabadilika, na itazidi kubadilika. Inasonga na lazima usonge nayo.

Hii ndio kutungamana na maisha.

Hii ndio kutoka kwa utenganisho.

Hii ndio kujikomboa kutoka kwa distractions na obsession.

Hii ndio kujifunza kusikiza, kuona, kutuliza akili yako ndio uweze kuona.

Hii ndio kuyawacha malalamiko yako ili upate kuelewa pale ulipo.

Nii ndio kuchukua Hatua kwa Knowledge ndiyo uwepo na nguvu ya Mungu izungumze kukupitia na ikuzungumzie.

Huu ndio Ufunuo unaoongoza ubinadamu katika mwelekeo mpya.

Je, watu wako tayari kwenda, ama watakaa nyuma – wakikabiliana na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko, kama wamelala katika pwani wakati Mawimbi Makubwa yanapata nguvu, wanaishi katika ufukwe na kufikiri kwamba yote yamo salama, na wakiishi kwa muda, wakiwa hawawezi kukabiliana na ishara za dunia, wakiishi kulingana na mawazo ambayo hayafuatani na hali halisi ya maisha?

Ni nani anayeweza kujibu?

Ni nani ataagalia?

Ni nani atasikiliza?

Ni nani atakayeweka kando dhana zake na imani yake na mapendeleo yake ndio aweze kukiona kitu, kukisikia kitu, kukijua kitu?

Hii ndio Mtume atakuuliza uifanye.

Hii ndio Unfunuo unahitaji kutoka kwako.

Hii ndio maisha katika dunia mpya itahitaji.

Hii ndio uibuka katika Jumuiya Kubwa ya waangavu inahitaji.

Je, binadamu atakuwa mjinga na dole, chachili na asiyewajibika, akili yake kubwa ikose kutambuliwa na kutumiwa?

Haya ndio maswali.

Majibu yeke hayako wazi, kwa kuwa bado hayajaibuka. Bado hayajakabiliana na jaribio la kweli ambalo limo katika familia ya binadamu.

Lakini Muumba wa maisha yote anaipenda dunia na anapenda ubinadamu na ameituma nguvu ya ukombozi duniani – kukomboa mtu binafsi na kurejesha nguvu yake na uadilifu, ili aweze kukabiliana na changamoto ya maisha inayoibuka katika upeo wa macho.

Mungu anaongoza binadamu katika mwelekeo mpya.

Huu ndio wakati wa kujitayarisha, kupokea na kusaidia ufunuo.

Watu watateta, Watalalamika. Watapinga. Watamulaani Mtume. Watakemea Ufunuo. Hawawezi kujibi, hawatataka kuwaza maisha yao na dhana zao upya. Watapinga Ufunuo.

Haya yote hufanyika wakati wa Ufunuo.

Wale walio na uwekezaji mkubwa katika siku za nyuma watapinga dunia mpya na kila kitu ndani yake.

Hawaoni. Hawataweza kujua. Hawana ujasiri wa kifikiria msimamo wao upya. Hawana unyenyekevu wa kusimama wakikabiliwa na Ufunuo.

Ni nini Mungu anaweza kuwafanyia?

Wanauliza vitu vingi kutoka kwa Muumba, lakini hawawezi kujibu jibu la Muumba.

Ni nini Mungu anaweza kuwafanyia?

Kuwa miongoni mwa kwanza kujibu ili zawadi zako kubwa katika maisha ziweze kuwa imara na kuwa na nafasi kujitokeza katika siku na miaka ya maisha yako.

Hii ndio nguvu ya Ufunuo – kutoa hekima na Knowledge ambayo binadamu mno anahitaji sasa kwa kujitayrisha kwa mustakabali ambao utakuwa tofauti na siku zilizopita.

Baraka ziko nanyi. Nguvu ya ukombozi iko ndani yenyu, kwa Knowledge ndani yenyu.

Lakini ni jambo gani ambali linaloweza kuignite Knowledge hii na kuiita na kukuwezesha uikaribie, uielewe na uifuate kwa mafanikio?

Ni lazima iwe ignited na Mungu, na ufunuo uko hapa ili kuweka katika mwendo ukombozi mkubwa wa watu binafsi katika maandalizi ya dunia mpya na kwa hatima ya binadamu ulimwenguni, ambayo bado haijatambuliwa na haijatimizwa.

Sasa ndio wakati wa kujibu.

Ni wakati wa kuwa mwaminifu kwako mwenyewe, bila kulingana maisha yako na mapendekezo yako, lakini kwa utambuzi wa kweli ndani yako.

Kukabiliana na Ufunuo kutaleta changamoto ya kujibu kwa uaminifu huu mkubwa.

Kukabiliana na Ufunuo kutaleta changamoto ya uaminifu huu mkubwa.

Ni changamoto kubwa ya maisha yako.

Ni changamoto muhimu zaidi ya maisha yako.

Ni tukio muhimu ya maisha yako.

Mungu anaongoza ubinadamu katika mwelekeo mpya.

Upendo Mkubwa

 

Upendo dunia unadhaminiwa sana, kama mnara wa ufarisi wa binadamu. Upendo huimbwa katika nyimbo, huandikwa katika mashairi. Hudhaminiwa katika maandiko makubwa. Huzungumzwa katika mazungumzo ya kawaida. Watu wanadai kuwa wamo katika upendo, kuwa upendo ndiyo ufarisi wa mwisho, kuwa kile mtu anahitaji duniani ni upendo tu na vengine vyote vitakuwa na matokeo mazuri. Lakini watu wachache tu ndio wanaelewa ukweli wa upendo. Na watu wachache tu ndiyo wana ufarisi wa upendo katika eneo ya ndani zaidi – zaidi ya mvuto, zaidi ya ghururi na mahaba. Watu wachache wana ufarisi wa nguvu halisi ya upendo.

Aidha, watu wengi hulinganisha baadhi ya aina ya tabia, imani na mitazamo kama upendo – upole, uwasilisho ni huhusishwa na upendo. Amani na utulivu huhusishwa na upendo. Lakini kwa kweli upendo huu wa ndani zaidi ni nini, sio upendo ambao tu ni mvuto , ama ghururi au mahaba, lakini aina ya upendo wa ndani ambao ni ukombozi, ambao huanza kutoka mahali ya undani ndani ya mtu binafsi.

Na zaidi ya haya, upendo wa Mungu ni nini? Ni ghururi, mvuto au mahaba? Watu wengi watasema hapana, lakini hawajui maana asili ya upendo wa Mungu na jinsi upendo huu unajieleza na jinsi unaweza kutafsiriwa katika dunia kwa ufanisi.

Hivyo leo tunazungumza kuhusu Upendo, upendo mkuu ambao unaishi ndani ya kila mtu na upendo mkuu wa Mungu, ambao ni jumla ya upendo wote Ulimwenguni, na ni chanzo cha upendo wote wa kweli kila mahali – katika dunia hii na katika Jumuiya Kubwa ya ulimwengu. Na hapo tutazungumza kuhusu kile Ujumbe Mpya kutoka kwa Mungu kwa dunia kinafundisha kuhusu upendo, kwa maana kuna Ujumbe Mpya kutoka kwa Mungu duniani, na upendo ni sehemu ya ujumbe wake.

Ni lazima hapa kuanza kwa kusema upendo sio nini. Upendo sio mvuto. Upendo sio ghururi. Upendo sio mahaba. Upendo si romance ambapo unavutiwa au kuchukuliwa na uzuri wa mtu mwingine au baadhi ya nyanja ya utu wake. Sio ibada ya sanamu, ambapo unaidolize mtu, unaabudu mtu, hata Uungu, hata Mtume, hata Mungu. Lakini haya hayawakilishi uhusiano halisi, uhusiano wa mafanikuo, uhusiano wa umoja.

Upendo sio tabia, mtazamo, staili. Sio etiquette. Sio mkataba. Upendo unaweza kujieleza katika njia tofauti – kwa upole au kwa kulazimishwa. Upendo unaweza kuonekana mpole. Upendo unaweza kuonekana imara. Upendo unaweza kuwa changamoto. Upendo unaweza kukukosoa. Upendo unaweza kufichua Illusions zako, fantasies zako na udanganyifu wako binafsi. Upendo sio kile watu humaanisha wakati wanajadiliana kuhusu upendo, katika karibu hali zote.

Upendo ni nguvu zaidi ambayo huongoza watu kufanya mambo ambayo ni tofauti na mawazo yao, imani zao na hisia zao za lazima. Upendo ni kitu kilicho zaidi ya upendo ambao unasikia katika mazungumzo. Kwa kweli, ni bora kuonyesha upendo kuliko kuzungumza kuhusu upendo, kwa kuwa upendo wa kweli huonyeshwa. Ni kile ambacho kinaongoza watu kubadilisha maisha yao, kubadilisha vipaumbele vyao, kwa kushirikiana na kile kilicho ndani zaidi na kubwa zaidi ndani yao. Ni kitu ambacho kina uwezo wa kuenda kinyume cha tamaa ya binadamu, ubinafsi wa binadamu, kero za binadamu na imani zote za mapendeleo na mitazamo, itikadi za kidini.

Kwa kuwa upendo haufungwi na mambo haya. Huzuliwa tu na haya, hurudishwa nyuma au hufichwa na haya. Lakini upendo husonga kwa hiari yake mwenyewe, kwa kuwa inahusishwa na Knowledge ambayo Mungu ameweka ndani ya kila mtu. Kwa kuwa, ulizaliwa na akili mbili – akili ya kufikiri na akili na kujua. Akilin ambayo unafikiri nayo ni bidhaa ya ushawishi wote kutoka jamii yako. Ni bidhaa ya kuwa duniani. Ni mkusanyiko wa mawazo ya vyama, na mwelekeo wa fikra ambazo umejifunza tangu siku uliyozaliwa. Fikra mengi ni muhimu, na baadhi yake ni madhara na hatari kwako. Hakika, umekuwa na ukijifunza jinsi ya kuishi duniani – jinsi ya kuishi kimwili, jinsi ya kuishi kijamii, namna ya kushiriki katika mazingira ya familia, katika utamaduni au labda ndani ya muundo wa kidini. Umekuwa ukijifunza jinsi ya kuwasiliana na mawazo yako na hisia. Umekuwa ukijifunza kile jamii imekuambia ni lazima ujifunze. Kama tulivyosema, baadhi ya haya ni mazuri na muhimu sana na baadhi ya haya ni hatari na hayana maslahi bora kwako.

Lakini ulizaliwa na akili ya ndani, akili ya Knowledge. Akili hii haifikiri kama akili yako ya kimwili inafikiri. Inaona na inajua. Sio ile watu wanadhani wakati wanazungumza kuhusu subconscious. Subconscious huhusishwa na akili yako ya kidunia, au uwekevu. Hii ni akili ya ndani na haiwezi kushawishiwa na dunia. Haifuati mfano au ushawishi wa dunia. Haiogopi au kutishwa na dunia. Akili hii ya ndani zaidi inaitwa Knowledge katika Ujumbe Mpya sababu inahusiana na ufarisi wa moja kwa moja wa kujua, ni ufarisi wa mshikamano, ni ufarisi wa utambuzi wa kweli na ufarisi wa uhusiano wa kweli.

Upendo wa kweli huanza kutoka uwepo wa Knowledge. Kwa asili ni uelezaji wa Knowledge. Wakati Knowledge inakuongoza kufanya jambo lolote – labda kitu kamwe haukuwa na mpango wa kukifanya, kitu ambacho haukielewi, kitu ambacho kinaenda kinyume cha mipango yako na malengo na matarajio. Hili linaonyesha upendo kwa sababu unaonyesha mapenzi ya Mungu, ambayo ni upendo wa Mungu. Kwa kuwa upendo wa Mungu hauko tofauti na nia ya Mungu. Mungu hafikiri kama vile akili yako hufikiri – ina furaha siku moja, na huzuni siku ijayo, inafurahia hiki, na kukasirikia kingine, ina ukatili na inawaadhibu wale waliofanya makosa au ambao wanaishi katika makosa. Hii si Mungu! Hii ni akili ya binadamu inahamisha akili ya binadamu kwa Mungu na kuhamisha kwa Mungu hisia na malalamiko ya binadamu. Haya ni matarajio yote ya akili ya binadamu. Lakini Mungu yumo zaidi ya haya yote. Na upendo na mapenzi ya Mungu yamo zaidi ya haya yote.

Hivyo kama unaishi katika akili ya kibinafsi au kile unakiita “ubapa wa akili,” basi, fikra zako zote kuhusu Mungu zinahusishwa na akili yako ya kibinafsi. Unafikiri kuwa Mungu ni kama utu mkubwa, akili kubwa mno, lakini akili ambayo inaweza kudhibitiwa na hofu na wasiwasi, chuki na mashtaka, hukumu na adhabu, mawazo ya kudumu, haki na uzushi. Huyu ni Mungu ambaye watu wanadhani anafikiri kama hao, anatenda kama hao, ana tabia kama zao.

Lakini ukifikiri Mungu kwa kweli ni nini, basi, Mungu wa Jumuiya Kubwa, Mungu wa maisha yote ya akili katika Ulimwengu, bila shaka Mungu wa Ulimwengu, wa Jumuiya Kubwa, hawezi kushawishiwa na imani za binadamu, mitazamo ya binadamu, hisia za binadamu, mikataba ya jamii ya binadamu na mambo yote ndogo ambayo yanaweka ubinadamu katika hali iliyo primitive na haijaendelea.

Kama Mungu ni Mungu wa Jumuiya Kubwa, basi Mungu ni mwandishi wa aina mingi ya maisha ya kiakili isiyohesabika, ya dunia zisizohesabika ambapo maisha ya kiakili inaishi. Mungu ni mwandishi wa mageuzi. Mungu ni mwandishi na chanzo cha upanuzi wa Ulimwengu. Mungu ni mwandishi wa ukweli wote ya kisayansi. Mungu ni muumba wa jamii zisizohesabika ya viumbe ambavyo havilingani nawe, havifikiri kama unavyofikiri au kuwa na mfumo wa thamani kama wako. Mungu ni mwandishi wa asili, ambayo inafanya kazi ndani ya dunia hii na kwingineko na ndani ya dunia zote katika Ulimwengu na zaidi ya Ulimwengu – katika eneo zote za udhihirisho. Huyu ni Mungu mkubwa sana na anapita mawazo yote ya kiteolojia, mifumo ya dini ya imani, mashirika ya dini. Ni bora kuweka kando mawazo yako kuhusu Mungu na kukifuata kile Mungu ameweka ndani yako ukifuate, na ukione kile Mungu amekiweka ndani yako ukione, ukisikie kile Mungu amekiweka ndani yako ukisikie.

Hapa tu ndipo unaweza kuwa na ufarisi wa Mungu na ufarisi wa uhusiano wako na Mungu, na hatimaye, ukifanikiwa katika kufuatia nguvu na uwepo wa Knowledge ndani yako, utaugundua mapenzi ya Mungu kwako katika maisha haya, katika dunia hii, kwa wakati huu.

Kwa sababu huwezi kuelewa Mungu, ina maana huwezi kuelewa mapenzi ya Mungu. Ina maana huwezi kuelewa upendo wa Mungu. Lakini unaweza kuhisi mambo haya kwa sababu Mungu amekupatia akili ya ndani, akili kubwa zaidi, akili ya Knowledge. Unaweza kubashiri, unaweza theorize, unaweza kuanzisha mifumo ya kufafanua ya mawazo, mifumo ya kufafanua ya akili, lakini kama huwezi kuwa na ufarisi wa harakati ya Knowledge katika maisha yako, hekima ya Knowledge katika maisha yako, ambayo inatoa shauri wakati wote – shauri ambayo huwezi kusikia, shauri ambayo hujibu kwa sababu mawazo yako yapo katika ubapa, katika akili yako ya kibinafsi na katika mtazamo wako wa dunia. Kama huwezi kuhisi harakati hii kwa undani, basi, Mungu ni wazo la kigeni kwako. Mungu ni wazo ambalo unaweza kukubali au kuweka kando.

Mungu ameweka uelezaji wa mapenzi ya Mungu na upendo ndani yako, zaidi ya eneo la ubapa, zaidi ya eneo la akili, mapenzi na upendo ambao huwezi kuidhibiti, huwezi kuitawala, huwezi kuitumia kupata utajiri, nguvu au ushawishi. Unaweza tu kuwasilisha nayo. Unaweza tu kuifuata na kujifunza kuihusu na kufanya kile ambacho kinakupa ukifanye ili uweze kuanzisha upya maisha yako, kujenga upya mawazo yako, kujenga afya yako, kubadilisha maisha yako, kuanzisha tena seti kubwa ya vipaumbele vyako na pamoja nazo nafasi kubwa zaidi katika mahusiano na wengine.

Ni upendo huu mkuu ambao umo mbali zaidi na tofauti na upendo unaousikia katika mazungumzo. Watu wanasema, “Ninakipenda hiki. Ninamupenda yule. Ninapenda chakula hii. Ninapapenda mahali hapa. Ninayapenda mavazi yako. Ninapenda asili. Ninapenda miti. Ninapenda bahari.”

Upendo wa kweli uko zaidi ya haya yote. Upendo wa kweli ambao unakuongoza ujitolee katika huduma, ambayo inabadilisha maisha yako, ambayo inakuambia kuwa uko katika upotovu, inakuambia ukweli kuwa maisha yako imekuwa ufujaji na unajaribu kuchukua mwelekeo ambao sio mwelekeo wa kweli, hii ni upendo!

Upendo ambao unaendelea kukuongoza katika dhamira yako kubwa ya kukuja duniani bila kujali mipango yako na malengo yako, upendo ambao haubadiliki, upendo ambao hauendani na matakwa yako, hii ni upendo!

Mara kwa mara, inaleta changamoto, na unaona kuwa unashindwa na huwezi tena. Na mara kwa mara, inafaraja na inatuliza, na unaikaribisha na kuwa na furaha ipo, kuwa ni ya kweli.

Huu ndio Upendo Mkuu – upendo wa Mungu na upendo wa Mungu uliowekwa ndani yako, kwa Knowledge ndani yako, katika akili yako ya ndani. Akili hii ya ndani iko hapa kwa misioni. Iko hapa kwa dhamira, kwa maana umekuja duniani kwa kutimiza misioni, kwa dhamira, kufanya mambo maalum na watu maalum. Na Knowledge ndani yako inajaribu kukuongoza ufike hapo, kukuongoza katika mwelekeo sahihi ndio uweze kufika pointi ya mihadi yako na wale ambao una dhamira ya kukutana nao na kupata hali na mazingira ambapo dhamira yako kubwa zaidi inaweza kujitokeza, inaweza kuwa activated. Wakati watu bado wanafanya mipango yao na kuimarisha kile wanakifanya na kile wanaamini, Knowledge ndani yao inajaribu kuwaongoza mahali fulani.

Kwa hivyo, kamwe usifikiri kuwa watu daima wako mahali wanafaa kuwa, wanafanya kile wanafaa kukifanya. Hio sio ukweli. Hio ni kisingizio tu. Ni aina ya njia ambayo watu husema ili mambo yawe sawa, ili kufanya mambo yote yawe haki, lakini kwa kweli, maisha yao yamo katika upotovu. Hawapo mahali wanahitaji kuwa. Wanafanya kazi katika eneo ambayo haiwakilishi dhamira yao kubwa zaidi ya kukuja duniani, au wamefungwa na umaskini au ukandamizaji wa kisiasa, au wamefungwa katika nafasi yao na hawawezi kupata njia nyingine.

Lakini upendo wa Mungu bado unaishi ndani yao. Kamwe upendo huu hautakata tamaa. Upendo huu sio kama akili yako ya kufikiri, ambayo haina msimamo katika tamaa yake, imani yake inayoshinda ikibadilika na vivivnyovinyo vyake, katika mawazo yake ya pinduani, ukali wake. Kitu pekee kwa kweli ni kile cha msingi ndani yako ni Knowledge kwa sababu hicho ndicho kitu pekee ambacho kitadumu. Na Knowledge hii haijafungwa na itikadi za kidini au kwa mapendeleo ya taifa. Haiwezi kutumika kama silaha. Haiwezi kutumika kuonea wengine. Haiwezi kutumika kwa kugawanya na kushinda wengine. Knowledge inaweza tu kufuatwa. Haiwezi kutumika. Akili lazima itumikie Roho. Sio kwa njia nyingine.

Watu wanataka Mungu afanye mambo mengi kwa maisha yao, kama Mungu ni mtumishi wao. Watu wanataka Mungu awalinde kutoka hatari au janga. Wanataka Mungu awapatie kile wanachotaka, kama Mungu ni aina ya, ni kama mtumishi. Hii ni akili inataka Roho itumikie akili. Akili inataka Mungu aitumike na aiimarishe. Huu sio mpango halisi. Hii ni kichwa chini. Kwa kweli, mwili wako unafaa kutumikia akili, na akili yako inafaa kumtumikia Roho, au Knowledge. Na Knowlegde hapa inatumikia Mungu. Huu ndio uongozi wa kweli wa kiumbe chako. Huu ndio mpangilio peke yake ambapo uadilifu wako unaweza kuwa na ufarisi na kuwa imara, ambapo unaweza kupata umoja ndani yako mwenyewe.

Hatimaye hapa, kila kitu ni mtumishi wa Mungu kwa sababu kama mwili ni mtumishi wa akili, na akili ni mtumishi wa Roho, na Roho ni mtumishi wa Mungu, basi, kila kitu ni mtumishi wa Mungu. Lakini ili kupata uadilifu, ili kupata maelewano ya ndani, muungano huu wa masuala yote ya maisha yako, inahitaji maandalizi makubwa – maandalizi ambayo huwezi kuyaumba mwenyewe, maandalizi ambayo si aina fulani ya mfumo wa mchanganisho ambapo unachukua kile unakipenda kutoka mila hii na kile unakipenda kutoka ingine alafu unayaunganisha, kulingana na mapendekezo yako. Hii ni kutumia Roho kuimarisha akili. Hii siyo sahihi kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Knowledge itakuongoza pale ambapo hungeweza kujipeleka mwenyewe. Knowledge itakuongoza kutoka kwa hofu yako na mapendekezo yako kwa sababu mapendekezo yote yanatokana na hofu – hofu ya kukosa, hofu ya kuwa na makosa, hofu ya kupoteza, hofu ya kifo.

Katika dunia hii, kuna mengi ambayo yamekamilika katika dini na katika kiroho. Kama unaweza kuelewa mageuzi ya maisha katika dunia zengine, basi utaona kiasi ambacho ubinadamu umeendelea, licha ya makosa yake mengi. Ungeona kuwa dini katika dunia hii kwa kweli imeendelea sana. Ungeona kuwa mataifa mengi yalioendelea kiteknolojia yamewacha dini zao zote, uelewa wao wote wa kiroho. Wamekuwa kama mitambo, kama mashine, kulingana na mawazo yao, kulingana na sayansi yao, kulingana na dikteta ya kisiasa na muundo wa kijamii.

Musidhani kuwa dini katika dunia hii ni kosa kubwa. Kwa kweli ni dini pekee yake ambayo binadamu anaweza kuchangia katika Jumuiya Kubwa kwa hatua hii. Kile ambacho kimekuwa na mafanikio katika suala la uhuru wa mtu binafsi na ufahamu wa kiroho kwa kweli ni kizuri sana kulingana na nafasi ya binadamu katika ulimwengu kwa ujumla. Na huu ni uelewa muhimu kwa sababu mustakabali wa binadamu utakuwa katika Jumuiya Kubwa, na kama mutabaki kama taifa iliyo huru na inayojitegemea itaamuliwa na mahusiano yenyu katika Jumuiya Kubwa.

Upendo ni nini? Upendo ni harakati ya Knowledge. Au ikisemwa kwa maneno mengine, upendo ni mapenzi ya Mungu yanayojieleza yenyewe kukupitia. Hapa upendo unahusishwa na inspiration, ambapo akili inaunganishwa na Roho, ambapo akili inatumikia Roho, ambapo akili inaongozwa na Roho. Wakati mwingine hii hufanyika mara moja yenyewe. Wakati mwingine hutokea wakati umekata tamaa sana, na unahisi kitu ndani yako ambacho inatoa matumaini wakati unajisikia kuwa unakata tamaa.

Lakini kupata faida ya Knowledge, kuchukua hatua kwa Knowledge, inahitaji mbinu inayotekelezwa kwa makini. Na mbinu hii inatakiwa itolewe na Mungu kwa sababu Mungu tu ndiye anajua jinsi ya kuunganisha tena mawazo yako na akili kubwa ya Knowledge ndani yako.

Kuna mengi ambayo akili yako inafaa kufanya na kuzingatia, na hata ujuzi wake mkubwa haujakuzwa kikamilifu ndani ya watu, lakini katika suala hili, lazima upokee neema ya Mungu, ambayo ni upendo wa Mungu. Maisha yako imepotea. Hujijui mwenyewe au kile unachokifanya na hatimaye unakuja katika pointi ya kukata tamaa ambapo unatambua kuwa huu ni ukweli wa hali yako na hali hii daima ilikuwa hali yako. Na Mungu anakutumia Hatua kwa Knowledge. Unaweza kutaka Mungu akupe kazi mpya, uhusiano mpya, mwili nzuri, au Mungu ayaondoe matatizo yako. Haya ndio yale watu wanataka Mungu awafanyie. Mungu anatuma kile kitawakomboa, sio kile wanachokitaka. Kile wanachokitaka kitaendeleza tu hali yao, utenganisho wao, kitazuia watu kuweza kupata fursa ya kupata Knowledge. Kwa hivyo Mungu kwa upendo wa Mungu anakitoa kile kinachohitajika kwa ukombozi.

Ni wakati tu unatambua kuwa kukipata kile unachokitaka haitatoa tofauti kwa maisha yako ndio utarejea Knowledge. Ni wakati itakapokuwa dhahiri kuwa mipango yako ya kujitimiza duniani ni dhaifu na hayatatimiza matarajio yako ndio utarejea kwa Knowledge. Hapa disappointment kubwa ni muhimu sana na inamiliki nafasi kubwa kwako. Lakini dissapointment ndio kila mtu anataka kuepuka, kwa hivyo watu wanaendelea kujaribu kupanga na kuzingatia maisha yao ili kwa wapate wanachotaka. Tatizo lao linazidi tu. Knowledge inawashauri, lakini hawawezi kusikia. Hawako wazi ndio waweze kupoea Knowledge. Wanakitaka kile wanachokitaka. Wanaendeshwa na hofu na upendeleo wao. Na hivyo hawaujui upendo.

Upendo ndio unawapatia wanachokitaka. Upendo ni kitu ambacho kinaonekana ni kizuri. Upendo ni kile ambacho wanachohisi kuwa ni kizuri katika wakati huu. Na matokeo yake ni, dhana ya watu kuhusu upendo inakuwa chanzo cha addictions zao. Na upendo unakuwa aina ya dawa la kulevya. Lazima uwe na mtu huyu. Lazima uishi katika eneo hili. Lazima uwe na chakula hiki. Lazima uwe na radhi hii. Lazima uwe na madawa haya ya kulevya.

Upendo wa Mungu ni harakati ya Knowledge ndani yeko, kwa sababu harakati hii inakuongoza kwa ukombozi wako na utimizo wako duniani. Kupata ukombozi na utimozo huu, ni lazima uwe huru kutokana na mahusiano na majukumu yanayokufunga katika maisha yako. Ukombozi si kitu tu ambayo unaongeza juu ya maisha yako, Sio kitu kingine ambacho unasimamia katika maisha yako. Si tu kitu cha kuongeza. Ni maisha yako. Kila kitu ambacho Knowledge inakuongoza ukifanye, kama inakuongoza kuepuka kitu au kukuongoza ukifuate kitu, yote yana lengo la kukuongoza kwa ukombozi wako. Na ukombozi wako una maanisha kuwa umelinganisha akili yako ya kufikiri na Knowledge, huu ndio ukombozi. Huu ndio mwanzo wa ahadi ya kweli kwako. Hukombolewi kwa Mungu. Hujawahi kutengwa na Mungu. Mungu hajakukasirikia. Umejiweka mwenyewe katika uhamishoni. Umeingia katika mazingira ambapo Mungu hajulikani, ambapo Mungu amesahaulika, ambapo Mungu ni ibada ya sanamu, imani na kiibada. Kile kinachokukomboa ni kuchukua hatua kwa Knowledge, kuunganisha akili na Roho, akili ya kufikiri na nguvu halisi ya Knowledge ndani yako – siyo na imani yako kuhusu Roho au kiroho au dini, lakini na ukweli.

Watu wengi hawawezi kutofautisha kati ya imani yao na hali iliyo halisi. Wanafikiri kuwa imani yao ni ukweli. Wanasema, „Kile ninachoamini ndio cha kweli.“ Wanasema , „Kile ninachoamini ndio ukweli.“ Wanasem, „Kile ninachoamini ndio mapenzi ya Mungu.“ Na bado vile wanazidi kuyazingatia mawazo yao inaonyesha kuwa bado hawajashikamana na Knowledge. Bado hawajaokolewa.

Akili lazima itumikie kile Mungu amekiweka ndani yako. Kile Mungu amekiweka ndani yako ni mapenzi na mpango wa Mungu kwa maisha yako, ambayo inashikamana na mapenzi na mpango wa Mungu kwa maisha yote ndani ya dunia hii, nje ya dunia hii, katika Jumuiya Kubwa ya dunia zote ulimwenguni ambapo unaishi. Kubwa sana! Baada ya kuuona ukubwa wake, utatambua kuwa mawazo yako kamwe hayataweza kuyaelewa na kuyafafanua. Lakini Knowledge inalingana na kila kitu. Iko katika maelewano na Knowledge ndani ya wengine. Na kuwa Knowledge ndio mpatanishi mkubwa duniani. Amani yoyote ya kweli ambayo imekuzwa na kuanzisha imetokana na Knowledge. Vinginevyo, makubaliano ya amani ni mipango ya kiuchumi au kisiasa ya kuzuia vita na migogoro. Hakuna amani hapa imeanzishwa. Amani ni matokeo ya watu kutambuana na kuwasiliana, si tu biashara ya mipaka, si tu kuangaliana kwa mbali, lakini kujifunza kutambua na kuwasiliana na kuhusiana pamoja.

Idadi ya watu duniani ikizidi kuongezeka, muna fursa kubwa ya kuanzisha umoja wa binadamu, umuhimu mkubwa wa kuanzisha umoja wa binadamu. Katika dunia ya rasilimali ambazo zinapungua, idadi hii ya watu ambao wanaoongezeka lazima iungana kimarisha uwezo wake wa kuishi. Hali halisi ya uhaba ambayo munaijenga inaleta msukumo mkubwa wa umoja wa binadamu. Hii ni kazi ya Knowledge.

Mungu hataki ubinadamu uishi katika dunia ambayo ina idadi ya watu wengi, dunia ya rasilimali zinazopunguka. Lakini Knowledge itaendelea kuongoza watu kwa ukombozi wao bila kujali hali ya dunia! Hata kama mutajenga mazingira ya ndoto mbaya katika dunia, Knowledge ndani yenyu na wengine itawaongoza katika ukombozi. Mungu basi sio mwandishi wa yale unayoyafikiri na unayoyafanya. Mungu ni mwandishi wa ukombozi wako. Mungu ndiye chanzo cha dhamira kubwa zaidi ambayo imekuleta na kila mtu duniani. Na yule ambaye ataweza kupata Kumbukumbu ya Kale atafarisi nguvu na mamlaka ya Mungu. Na yule ambaye anaweza kuchukua Hatua kwa Knowledge na kuleta Knowledge katika ufahamu wake atakuwa na ufarisi wa upendo wa Mungu.

Upendo ni kama hewa unayopumua. Hauidhamini. Kamwe hauiwazi. Lakini unaihitaji kila wakati. Upendo ni kama hewa. Unaweza kufarisi? Knowledge iko ndani yako. Imetulia. Inatoa ushauri. Unaweza kuihisi? Unaweza kuisikia? Uko tayari kwenda kwake kwa mikono iliyo wazi, bila madai, bila imani, kuenda kwake tu? „Ninaenda kwa Mungu.“ Enda kwa Mungu. „Nia ya Mungu kwangu ni nini? Nifanye nini katika hali hili? Ninafaa kuwa na mtu huyu? Ndiyo au hapana? Ninafaa kuenda mahali hapa? Ndiyo au hapana? Ninafaa kushiriki katika shughuli hili? Ndiyo au Hapana? “

Kila kitu ni rahisi. Hakuna mikataba. Hakuna maafikiano. “Naam, nitafanya kitu kudogo kuhusu haya kama Mungu anatoa kitu kidogo kwangu. Nitafanya mpango na Mungu. ” Hakuna mikataba. Utafuata uongozi ama hautaufuata. Uko tayari kukishuku kile unajitakia, au hauko tayari. Hii haimaanishi kuwa unajisalimisha kwa Mungu. Hii itatokea labda baadaye. Huu ni ufunguzi mdogo, utayari mdogo, mwanzo. Unaanza kama mwanagenzi. Huwezi tu kuruka katika hali ya kukomaa katika uhusiano wako na Mungu. Lazima uchukue hatua. Na Mungu ndiye anatoa hatua.

Upendo ni harakati ya Knowledge ndani yako. Knowledge ni akili ya ndani ile Mungu ameweka ndani yako, ikuongoze, ikulinde na ikuongoze kwa ugunduzi wa dhamira yako kubwa katika dunia hii kwa wakati huu. Kitu kiingine kinachojiiita upendo ni uonyesho tu. Haina staamani ndani yake. Haina hekima ndani yake. Na haina dutu. Maisha haitaitekeleza. Hii ndio maana watu huwa katika upendo, wanaanza uhusiano, na kisha wanajua katika uhusiano kama wanaweza hata kuwa katika uhusiano, na kwa mara nyingi hawawezi kuwa katika uhusiano. Kwa hivyo upendo uko wapi hapa? Upendo ni nini hapa? Ghururi ya awali? Mvuto wa kitu ambacho unafikiri kitakuokoa au kufanya uwe kile unataka kuwa?

Watu huzeeka. Wanapoteza uzuri wao wa kimwili. Wanapoteza mvuto wao. Maishani wanakabiliana na matatizo na mahitaji. Lazima wazalishe. Lazima wafanye kazi. Lazima wakabiliane na shida. Ni nini kilichotokea kwa upendo wao ule huko mwanzoni ulikuwa wa furaha na ajabu? Basi kile watu walidhani kuwa ni mapenzi inakuwa aina ya mkataba wa kuishi au ustaarabu.

Kuna upendo mkubwa. Kuna Upendo Mkuu, upendo ambao Mungu ameuweka ndani yako, ndani ya kila mtu, unaosubiri kugunduliwa, unaosubiri kuonyeshwa na ufarisi. Upendo huu hauna njia moja tu ya kujieleza. Haihusiani na aina fulani ya tabia au etiquette. Sio mkataba wa kijamii. Upendo huu utakuvuta mbali na hatari. Upendo huu utatoa changamoto kwa mawazo yako na mtazamo wako. Upendo huu utakuonyesha kuwa maisha yako haiendi popote. Upendo huu utakuongoza uelekee njia moja wakati unataka kupitia njia nyingine. Upendo huu utakuzuia. Upendo huu utakuelekeza upya. Huu ni Upendo Mkuu. Hiki ni kitu halisi! Hata kama uko peke yako maishani, kama unaweza kuhisi harakati ya Knowledge, utahisi upendo wa Mungu. Hutaielewa. Hutakuwa na hakia mahali ambapo utakuongoza. Hutakua na uhakika kuhusu maana yake. Lakini kama utaifuata, basi utakuwa na ufarisi wake. Na hatua kwa hatua, na nyongeza kwa nyongeza, itaongoza maisha yako katika nafasi tofauti na kufungua fursa kubwa kwako.

Hapa lazima ufanye mazoezi ya uvumilivu na forbearance. Lazima uahirisha hukumu na uchelewesha mahitaji yako ya kuwa na hitimisho kwa sababu unahitaji kupokea kutoka kwa Mungu. Kabla uweze kutoa kile ambacho Mungu amekupa utoe, lazima upokee kutoka kwa Mungu. Lazima basi Mungu aikomboe maisha yako.

Baadhi ya watu wanadhani kwamba kukombolewa ni kuchukua mfumo wa imani: „Nimekombolewa kwa sababu sasa ninaamini“ Lakini huu sio ukombozi. Imani ni dhaifu na inakosa uhakika. Daima lazima ishinikizwe. Haina nguvu ya Knowledge. Ni uvumbuzi wa binadamu! Ni lazima Uwe na imani kwa Knowledge ndani yako, lakini hata hapa unatambua kuwa Knowledge ni kubwa kuliko ufahamu wako. Na pale ambapo Knowledge inakuongoza ni mbali na ufahamu wako wa sasa.

Kama unaweza kufuata, unaweza kupata. Kama unaweza kupata, unaweza kutimiza. Kama unaweza kutimiza, unaweza kueleza.

Huu ndio Upendo Mkuu. Na haja ya Upendo huu Mkuu ni mkubwa. Angalia dunia inayokuzunguka. Kuna watu wengi. Kuna shida mingi. Kuna hatari mingi, na hatari kubwa ya kutishia katika upeo wa macho. Upendo Mkuu uko wapi? Katika maisha yako yote, kwa kazi na shughuli zako, preoccupations zako na wasiwasi, malalamiko yako, mivuto yako, Upendo Mkuu uko wapi? Upendo Mkuu ambao unakusisimua na unakuongoza na unakujumuisha? Huu ndio lazima uupokee, ni upendo wa Mungu, ambao ni harakati ya Knowledge. Hivi ndivyo Mungu atakukomboa. Umekuwa ukijaribu kujikomboa, lakini hivi ndivyo Mungu atakukomboa.

Unachukua kila kitu unachokifanya maishani, na kujiuliza, „Kimsingi, hiki ni kile ambacho ninahitaji kukifanya?“ Katika mahusiano yote, „Je, uhusiano huu unanisaidia? Je, ni muhimu kwangu wakati huu ?“ Kila kitu! Na utakuwa na maana zaidi ya hayo itakayotoka kwa Knowledge, ndani yako kabisa. Labda itakuwa hisia. Labda itakuwa picha. Pengine jibu litakuja wiki moja kutoka sasa. Lazima uendelee kuuliza na kusikiliza. Unaomba Upendo Mkuu ukukomboe, ukuungane, na ukuweke katika nafasi ambapo zawadi zako kubwa zinaweza kufikiwa na kuchangiwa duniani. Na hii inahitaji uwe katika baadhi ya mazingira fulani, uwe katika mahusiano na baadhi ya watu fulani, katika mazingira fulani. Kama hauko katika mazingira fulani na watu fulani, basi, ugunduzi hautatokea. Pale ambapo uko kimwili ni muhimu sana katika suala hili. Wale ambao unahusiana nao ni muhimu sana katika suala hili.

Kama utambuzi wako utatokea katika mji fulani kuhusu baadhi ya watu fulani walio pale na hauko katika mji huo, basi, ugunduzi utafanyika aje? Hata kama uko katika mahali sahihi, utaweza aje kuwapata watu halisi ambao una dhamira ya kutimiza pamoja nao? Huwezi kujua. Hii ni kubwa mno kwa akili. Ni Knowledge peke yake ambayo inaweza kukuongoza uende huko. Knowledge inaweza kuleta watu wawili kutoka sehemu za kinyume za dunia kwa kutimiza dhamira kubwa zaidi. Hiyo ni nguvu ya Upendo Mkuu. Na Upendo Mkuu ndio ambao dunia inahitaji sasa.

Mapenzi ya Mbinguni

Watu wengi duniani wanasubiri mwokozi wao, Maitreya wao au Imam wao arudi. Lakini Mungu ametuma Ujumbe Mpya duniani, Ujumbe wa kuandaa ubinadamu kwa mabadiliko makubwa ambayo yatatokea na kwa mawasiliano na ulimwengu wa waangavu, Mawasiliano ambayo yatakuwa ya hatari zaidi kuliko vile watu wengi wanatambua.

 

Kiroho cha binadamu kinamomonyoka duniani, asili ya kweli ya kiroho cha binadamu. Asili ya ndani ya kila mtu polepole inaanza kuwa baidi jamii yenyu ikizidi kuwa ya kiteknolojia na ya kidunia. Mgawanyiko kati ya dini ni kubwa sana na ya kuharibu, hata mgawanyiko ndani ya dini, yataongeza kwa migogoro na mateso ya binadamu katika siku zijazo, kama vile zivyo sasa.

 

Ukiangalia dunia kwa uaminifu ni utatambua kwamba matatizo yake yamezidi kushinda uwezo wa binadamu na uelewa wake. Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko yanayokuja duniani yanazidi yale watu binafsi na taasisi zinaweza kufahamu na kujadiliana nazo.

 

Ubinadamu umefikia katika kizingiti kikubwa cha mageuko. Hauwezi kurudi katika hali yake ya zamani. Hauwezi kurudi nyuma katika historia yake. Na hauwezi tu kuthibitisha imani zilizogawanywa na zina matata katika mila zake za kidini, ambazo zilianzishwa na Mungu.

 

Ufunuo wa Mungu lazima sasa uje tena na umekuja tena, na Mtume ametumwa duniani – mtu mnyenyekevu, mtu asiye na cheo kikubwa katika kijamii, mtu asiye na madai makubwa za kibinafsi na mafanikio, mtu ambaye maisha yake imehifadhiwa na kuelekezwa kwa dhamira hii peke yake.

 

Watu watabishana kuhusu haya, bila shaka, hawatataka au hawataweza kufikiria upya msimamo wao na kuwa wazi kwa Ufunuo Mpya. Wanafikiri kuwa wanaelewa mapenzi ya Mungu na dhamira yake kwa watu wa dunia hii. Wanafikiri wanaelewa maana ya Ufunuo na wakati unaweza kutokea.

 

Wanafikiri wanaelewa. Lakini ni nani anaweza kuyaelewa haya kikamilifu? Nani mwenye hekima na upana na uwezo wa kuyaelewa haya kikamilifu? Hakika haya lazima yazidi ufahamu wa mwanadamu. Na hakika lazima kuwe na unyenyekevu na uaminifu wa kutosha wa kutambua kwamba watu hawawezi kutabiri wakati na jinsi Muumba wa Ulimwengu wote atazungumza katika sayari hii moja ndogo.

 

Ujinga na kiburi cha binadamu unaungana hapa na kufomu mchanganyiko wa hatari, mchanganyiko wa ukali na ukandamizaji. Wa uchovu na kirahi. Wa upendeleo na utaoendelea kugawanya familia ya binadamu, mgawanyiko ambao unaweza kuwadhoofisha mkikabiliwa na mabadiliko makubwa ambayo yanakuja duniani.

 

Ujumbe Mpya uko hapa katika fomu safi, na kwa mara ya kwanza mutakuwua na uwezo wa kusikia Sauti ya Ufunuo. Ilikuwa ni sauti kama hii iliyonena na Musa na Yesu, Buddha na Muhammad na Walimu wengine wakuu ambao hawajulikani katika mwenendo wa historia ya binadamu.

 

Hakuna wakati wa makosa sasa. Hatari ni kubwa mno. Kila kitu kinachofanywa na Ufunuo Mpya kinafanywa ndio uwe wazi kabisa. Unatoa Ufafanuzi wake mwenyewe, Mafundisho yake yenyewe, kwa kuwa haya hayawezi kuachwa kwa utafsiri wa binadamu.

 

Hamuna wakati wa kutosha na ubinadamu haujajiandaa ndio uweze kukabiliana na dunia mpya ya rasilimali zinazopungka, kwa kukabiliana na hali halisi na matatizo ya kuibuka ndani ya Jumuiya Kubwa ya maisha ulimwenguni.

 

Muko katika kizingiti kikubwa, na kwako wewe kama mtu binafsii ina maanisha kuwa maisha yako inaharakishwa kukabiliana na kizingiti hiki, kujiandaa ili uweze kukabiliana na kizingiti hiki, na kushirikiana na kizingiti hiki.

 

Lakini hii inawezekanaje bila Ufunuo Mpya kutoka kwa Mungu? Hakuna mtu duniani aliye na hekima, uwezo na uelewa wa kuyatatua yale yote binadamu atakabiliana nayo akipita katika kizingiti hiki na kuingia katika dunia mpya na ya changamoto.

 

Ni nani duniani anayeweza kutayarisha binadamu ili aweze kukabiliana na ulemwengu, Ushiriki mkubwa, ushiriki ambao hata saa hizi unatokea, kwa siri, unafanywa na vikundi ambavyo viko hapa kupata faida kupitia ujinga na ushirikina wa binadamu?

 

Kama wewe kwa kweli ni mwaminifu, lazima ugundue kuwa hakuna aliye na upana wa uelewa huu, uwezo huu. Hakuna yeyote duniani anayeelewa Jumuia Kubwa ya maisha. Na kile watu wanafikiri ni makadirio ya hofu zao, fantasies zao, na haya yote hayatoi picha sahihi kuhusu yale ambayo mtakabiliwa nayo.

 

Asili ya kweli ya kiroho cha binadamu sasa imefumbwa, imepotoshwa, imeshikiliwa na mila na desturi na tafsiri kwa kiasi kikubwa hadi mila kuu ya dunia, ambayo inaweza kutoa hatua zile lazima muchukue, zinahitaji mwalimu wa kipekee na myenye vipawa aweze kupitia kila kitu kingine kilichoongezwa katika miongo na karne.

 

Dini imekuwa palliative. Imekuwa distraction badala ya mwangaza. Imekuwa kitu ambacho watu [hutumia] kutoroka dunia ya kutafuta faraja badala ya maandalizi ya kushiriki duniani kwa njia kubwa.

 

Muumba anayajua haya yote, bila shaka. Ufunuo umo zaidi ya mjadala katika eneo la juu. Umo zaidi ya uvumi. Umo zaidi ya itikadi. Umo zaidi ya teolojia ya dini moja inayoshindana na teolojia ya dini ingine. Mashindano haya ni tatizo la binadamu lililoumbwa na kutokuelewana kwa binadamu na kikomo cha uwezo na kikomo cha hekima ya binadamu.

 

Unaweza kupinga hoja dhidi ya Ufunuo, lakini huu ndio Ufunuo ambao umetolewa, na utakuwa ni Ufunuo ambao umetolewa. Ukubaliwe au ukataliwe, huu ndio Ufunuo.

 

Mungu hashuguliki tu na dunia hii, lakini Mungu anajua kuwa dunia hii iko – mahali padogo katika ulimwengu mkubwa.

 

Uwepo wa Malaika unayosimamia dunia hii unatafsiri Nia ya Muumba katika maneno na matendo, Mafundisho na Ufafanuzi ambao watu wa dunia wanaweza kuelewa na kufanya leo na kesho na siku zijazo.

 

Munaulizwa mupokee, sio muhukumu.

 

Munaulizwa mujiandae kwa dunia, sio mtumie dini kama aina ya kutoroka dunia.

 

Munaulizwa muheshimu asili yenyu ya ndani na muchukue Hatua kwa Knowledge ndio ukweli wake uwe wazi kwenyu.

 

Munaulizwa muwache migogoro yenyu yasioisha na musifikiri kuwa munaweza kuwa na vita duniani kwa jina la Mungu, kwa kuwa hilo ni chukizo. Hakuna majeshi takatifu. Hakuna kitu takatifu kuhusu vita.

 

Munaulizwa mujifundishe na mujitayarishe kukabiliana na dunia mpya na kukabiliana na ukweli wa changamoto na fursa ya kuibuka katika eneo kubwa la waangavu ulimwenguni.

 

Hamuwezi kujifunza haya yote, kwa kuwa hamujui ya kutosha. Na kubishana na haya ni kuonyesha kikomo chenyu na kutoelewa kwenyu.

 

Ujumbe Mpya umeletwa kwa watu – sio wataalamu, sio viongozi, kwa kuwa wamewekeza mengi katika cheo chao na matokeo ya haya ni, hawawezu kuyaona yanayokuja au hawawezu kushiriki ukweli kwa wale wanawafuata.

 

Ufunuo unampa mtu binafsi nguvu kubwa sana, lakini pia wajibu mkubwa sana. Kama munaongozwa na nguvu ya Knowledge ndani yenyu, akili kubwa ile Mungu ameiweka ndani yenyu, basi hakuwezi kuwa na vurugu, vita na migogoro. Kutakuwa tu na juhudi ya kuanzisha mipango chanya ya faida kwa wengine.

 

Hii ndio kazi ya akili. Hii ndio changamoto kubwa kwenyu, changamoto cha kiasi kikubwa kuwa itachukua nishati yako yote kama unataka kuifanya kwa mafanikio.

 

Ufunuo umo zaidi ya eneo na fikio la akili. Umo zaidi ya eneo na fikio la imani na itikadi. Mungu haumbi itikadi. Mungu anawapa hekima na uwazi na kiwango cha juu cha kuishi. Munaweza tu kuamua kuyafuata ama kuyakana.

 

Amua kuyafuata, na muyafuate kwa rehema, bila kuyatumia kama silaha ya kudhulumu wengine au kulaani wengine. Kulaani wengine kwa kuzimu na hukumu ni kutoelewa Ufunuo wa Mungu wa sasa na wa kale.

 

Kutangaza kuwa hakuwezi kuwa na Ufunuo mpya ni kutangaza kiburi na ujinga wako na kufikiri kuwa unajua mengi kuliko Muumba. Kwa kuwa hakuna aliye duniani anayejua kile Mungu atafanya tena. Hata Uwepo wa Malaika haujui kile Mungu atakifanya tena, hivyo ni nani anayeweza kutangaza hivyo? Hakika huu ni mfano wa kiburi na ujinga!

 

Hakuna mtu duniani anayeweza kutangaza kuwa Jesu ndiye njia ya kipekee kwa Munngu kama Mungu ametoa njia zingine! Wewe ni nani wa kuyasema hivyo? Huku ni kutoelewa na kuchanganyikiwa. Hivyo ni kujaribu kuweka imani yako juu na zaidi ya imani za wengine, kufanya mwalimu wako, mwakilishi wako, kuwa mkubwa na wa kipekee wa kufuatwa. Haya sio mapenzi ya Mbinguni. Huu ni ujinga wa binadamu

 

Dunia ambayo itawakabili itahitaji ushirikiano mkubwa wa binadamu, huruma na mchango, ama itakuwa uwanja wa vita kuhusu nani atakuwa na rasilimali zilizobaki duniani. Nani ambaye anaweza kulinda mali yake wakati mataifa mengine yanashindwa na kuanguka?

 

Madai kwa binadamu yatakuwa makubwa mno kiasi cha itachukua huruma na hekima kubwa ili watu waweze kujibu. Lakini watu wamegawanyika sana. Dini zimegawanyika sana. Kikundi hiki kinapinga kikundi kile kwa jina la utawala wa taifa yao, au kwa mapenzi ya Mungu, na ubinadamu utatumbukia katika vurumai.

 

Hii ndio maana Ufunuo Mpya umo duniani. Hapa haumusifu Mtume kama Mungu. Unamuheshimu kama Mtume. Hapa hautangazi mawazo yako juu ya mwengine, lakini unatambua kwamba mawazo ni chombo tu cha kutumiwa na nguvu kubwa ndani yako na kwamba ukweli wa kweli, ukweli mkubwa, unaishi zaidi ya eneo la akili, akili ambayo kamwe haikuundwa kuelewa hali halisi zaidi ya maisha.

 

Mapenzi ya Mbinguni ni ubinadamu uungane na ujiandae ili uweze kuishi katika Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko na ujiandae kwa mahusiano yake na maisha katika ulimwengu kwa njia ambayo uhuru wa binadamu na uwezo wake wa kujitawala katika dunia hii unaweza kulindwa.

 

Kwa kuwa munakabiliwa na ulimwengu ambapo viumbe havifanani na binadamu kwa tabia au mawazo na ambapo uhuru ni nadra na ambapo mataifa na watu walio huru lazima zitumie busara kubwa na tahadhari kubwa kati ya uwepo wa mataifa mengi ambapo uhuru umezuliwa ama ambapo kamwe haujawahi kufahamika.

 

Mahitaji ya Jumuiya Kubwa yatakuwa makubwa. Hamuwezi kuwa mukihusika katika migogoro ya mara kwa mara hapa duniani na kuwa na uwezo wa kuishi kuwa dunia iliyo huru katika uwanja huu mkubwa wa maisha. Hili sio suala la mtazamo au imani. Ni jambo la lazima.

 

Ndiyo mataifa yaweze kuishi katika mazingira ya rasilimali zinazopunguka duniani na mageuzi ya kisiasa na kiuchumi na shida inayoongezeka, Itakuwa ni lazima mushirikiane na wengine kati yenyu. Badala ya vita, lazima mutafute njia za kutoa chakula cha kutosha, maji na nishati kwa watu wa dunia. Hiyo ndio haja ya kuhodhi itakayokuwa hapa duniani katika mustakabali.

 

Watu ambao wanafikiri venginevyo wanaishi kwa mtazamo wa siku zilizopita, Dhana zao zina msingi katika siku zilizopita. Hawawezi kuyaona yale yanayotokea kati yao. Hawawezi kuyajua yale yanayokuja katika upeo wa macho. Wanaishi katika shell yao ya imani na dhana zao na ni kama vipofu kwa ukweli wa dunia wa leo na kesho. Wanafikiri kuwa ushiriki wa ulimwengu utakuwa ni matokeo ya uchunguzi wa binadamu, lakini kesi hii ni nadra ulimwenguni. Maingilio hutokea wakati mataifa yanapata nguvu na yanaungana. Hapa ndipo changamoto ya uhuru na uwezo wa kujitawala wa mataifa huanza.

 

Mafundisho yenyu kuhusu ulimwengu na matayarisho ya kuishi katika dunia mpya ni makubwa sana, yanahitaji Ufunuo Mpya kutoka kwa Mungu. Uwazi wa asili, dhamira na umoja wa kiroho cha binadamu sasa lazima yasisitizwe zaidi ya mambo yote, ama binadamu hatapata nguvu ama umoja wa kujibu mabadiliko makubwa yalio juu yake.

 

Ufunuo Mpya unaleta usahihi na ufafanuzi mkubwa, ambao ni muhimu sasa kama dini zote za kitamaduni za dunia zitaongeza hekima kwa familia ya binadamu na sio tu kuongeza migogoro, ubaguzi na ugomvi. Kila mmoja ina mchango wa kufanya. Zote ni muhimu. Dini moja sio kuu zaidi kuliko ingine. Kufikiri hivi ni kutoelewa Mapenzi ya Mbinguni, kwa kuwa ni binadamu tu iliyo na umoja ambayo itakuwa na uwezo wa kushindana na changamoto za maisha katika dunia mpya na changamoto kubwa ya kuhifadhi uhuru wake na uwezo wa kujitawala mbele ya vikosi ulimwenguni.

 

Huu ndio wakati munaishi, katika wakati wa Ufunuo. Ni wakati muhimu. Ni wakati wa ugumu. Ni wakati wa machanganikio. Ni wakati wa matokeo makubwa.

 

Nyinyi ndio miongoni wa wakwanza kujibu Ufunuo Mpya. Na hii ni kwa sababu ya dhamira. Sio ajali kuwa hivi ndivyo ilivyo. Wewe ambaye bado unajaribu kupanga utimizo wako maishani bado haujagundua kuwa una dhamira kubwa hapa, dhamira itakayoelezwa kwa kipekee katika maisha yako, lakini ni dhamira unayoshiriki na wengine, kwa kuwa hakuna aliye duniani kwa ajali sasa.

 

Kila mtu alitumwa hapa kushindana na hali ya dunia. Lakini maandalizi hayo hutokea katika eneo la ndani zaidi ya akili, katika eneo la Knowledge. Hii ndio sehemu yako ambayo haijawahi kutenganishwa na Mungu. Ni sehemu yako ambayo ilikuwa, na bado, ni utambulisho wako wa kweli. Knowledge ndiyo ilikuleta duniani. Ni Knowledge ambayo itakuongoza ukichukua safari yako duniani. Itakuwa Knowledge ambayo itaibuka nawe nje ya dunia.

 

Waliojitenga wanakombolewa kupitia Knowledge. Waovu huokolewa kupitia Knowledge. Wajinga hufanywa wa hekima kupitia Knowledge. Hivi ndivyo Mungu huokoa, sio tu familia ya binadamu, lakini uumbaji wote ambao unaishi katika utenganisho, unayoishi katika ulimwengu wa kimwili ambao unaweza tu kufikiria.

 

Ni Mapenzi ya Mbinguni ujibu Ufunuo Mpya. Ni Mapenzi ya Mbinguni uchukue Hatua kwa Knowledge, kwa uvumilivu, bila dhana, ukiweka imani zako, mapendeleo yako na hofu zako kando ukiendelea ndio uweze kushiriki na nguvu kubwa, uadilifu mkubwa na dhamira kubwa ndani yako.

 

Ni Mapenzi ya Mbinguni kuwa muweze kushiriki uwazi na maandalizi haya kwa wengine na muwe

kama gari la kushiriki Ufunuo huu, kwa kupointi kwa Ufunuo Mpya.

 

Ni Mapenzi ya Mbinguni kwamba ubinadamu upevuke, uibuke kutoka ujana wake ulio reckless na wa utata kuwa mawakili wa hekima wa dunia hii, ulinde rasilimali zake za uzima za dunia hii na uwe taifa iliyo na huru katika ulimwengu ambapo uhuru ni nadra na huthamaniwa na wachache tu.

 

Ni Mapenzi ya Mbinguni muwache migogoro yenyu isiyoisha, kwa kuwa sasa hamuwezi kuharibu watu wenyu na miji yenyu . Mutahitaji rasilimali zote za dunia, rasilimali zote zile munazo, kushindana na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko yanayokuja.

 

Hamuishi katika wakati wa siku zilizopita. Dunia ya kale imepita. Munaishi katika dunia mpya – dunia ya hali ya hewa isiyotabirika na mabadiliko ya hali ya mazingira, dunia ya rasilimali zinazopunguka, dunia ya udhaifu mkubwa, ya wasiwasi kubwa , ambapu tamaduni ya binadamu imo hatarini.

 

Lakini nani atayaona haya? Nani atayasikia haya, sio kwa dhana zake, au maoni yake au imani yake, lakini kwa undani, undani zaidi? Ni nani aliye na ujasiri wa kukabiliana na haya? Ni nani aliye na unyenyekevu wa kukabiliana na Ufunuo Mpya? Ni nani anayeweza kukubali kuwa Mungu ana mengi ya kusema kwa binadamu na awache ubinafsi, na kukemea na maazimio yanayofuata.

 

Mapenzi ya Mbinguni na nia ya binadamu bado ni tofauti sana. Lakini giza inaingia duniani, Hakuna wakati wa kutosha, na hakuna wakati wa upumbavu na kukana.

 

Ni wakati wa Ufunuo. Ni zawadi ya binadamu, ipokewe au ikanwe. Ni mustakabali wa binadamu, utimizwe au uharibiwe. Ni ahadi ya binadamu, igunduliwe na ielezwe au iharibiwe na itupwe. Huu ni uchaguzi mkubwa, sio wa watu wengine mahali pengine, lakini wako mwenyewe, ndani yako.

 

Kila kitu kinalingana na uchaguzi wa mtu binafsi, na hiyo ndio sababu Ujumbe Mpya kutoka kwa mungu unazungumza kuhusu swala hili. Hautoi tu mfumo mpya wa imani, nira mpya ya itikadi ambayo kila mtu sasa lazima aifuate na akandamizwe. Watu lazima watengeze maelezo kikamilifu. Lakini motisha lazima iwe ya kweli. Ufahamu lazima uwe hapo.

 

Lazima kuwe na uwazi mkubwa kuhusu yale munakabiliana nayo na yale mutakabiliana nayo katika mustakabali, na hii itarudisha nyuma tabia zenyu za udhaifu na uharibifu. Hii itafanya uwaze kabla ulaani ama ushambulie watu wengine au taifa zingine. Hii itarudisha nyuma extremesim na ukali na kiburi na ujinga wote unaojitokeza kwa uharara na ufasaha duniani.

 

Lazima uyasikilize maneno haya kwa roho yako. Usisubiri, kwa kuwa kila siku ni muhimu sasa. Wakati hauwezi kupotezwa sasa. Mtume yupo hapa. Hatakua hapa milele. Umebarikiwa kumusikia na kukutana naye kama inawezekana. Anabeba Ufunuo, zaidi ya kile ambacho kinapatikana katika kitabu au rekodi.

 

Mupokee, Musikilize. Na maisha yako itaonyesha ushahidi wa ukweli ambao unakaa naye na ndani yake na kupitia kwake.

Zawadi ya Maisha Mpya

 

Ujumbe Mpya kutoka kwa Mungu hauko hapa tu kuongeza thamani kwa maisha yako ya sasa ama kuhalalisha mawazo na shughuli zako za sasa. Haiko hapa kuhalalisha dini za dunia ama kuendana na imani au matarajio yao, kwa kuwa Mungu hajafungwa na haya yote. Haiko hapa kuhalalisha matarajio yako, kwa kuwa Muumba wa Ulimwengu yote hajafungwa na haya.

Kwa kweli, Ujumbe Mpya kutoka kwa Mungu uko hapa kutoa maisha mapya kwa wale ambao wanaweza kujibu kwa kweli, kuwapatia msingi mkubwa ambapo wanaweza kujenga maisha ya maana – maisha ya kutia moyo, maisha inayoongozwa na Knowledge, maisha ya mahusiano ya kweli na ya ushiriki wa maana na dunia.

Hapa majukumu hayapewi, lakini watu wanapewa msingi ndio Knowledge ndani yao, Nguvu kubwa ile Mungu amewapatia iwaongoze, iweze kuwa wazi kwao, ndio waweze kwa wakati kujufunza kuiamini na kuifuata, wakipitia hali ngumu ya maisha na hali ngumu ile itabidi wakabiliane nayo katika dunia mpya ya rasilimali ambazo zinapunguka na hali kubwa ya ukosefu wa utulivu.

Watu wanakuja kwa Ujumbe Mpya kuona kama inaendana na imani yao, mawazo yao na matarajio yao. Bila Shaka, haifanyi hivyo.

Watu wanakuja kwa Ujumbe Mpya kutoka kwa Mungu wakitaka kuitumia kama rasilimali ya kupata kile wanachokitaka kwao wenyewe, lakini Ufunuo Mpya una mpango mkubwa na ahadi kubwa kwao.

Watu wanakuja kwa Ujumbe Mpya wakitarajia kuwa watapata hekima wanayohitaji kurekebisha makosa yao na kufanya uwekezaji wao uwe na mafanikio na maana, lakini Ujumbe Mpya uko hapa kuwapa maisha mapya – sio tu wazo mpya iliyowekwa juu ya maisha yao ya zamani, sio tu asali ya kufanya ladha ya uchungu ya maisha yao ya sasa iweze kuwa nzuri na kukubalika. Watu wana matarajio madogo na wanataka kidogo, na matarajio yao hayalingani na maana na nguvu ya Ufunuo.

Watu wanakuja kwa Ufunuo wa Mungu wakitaka kuona vile wanaweza kuitumia kwa sasa, kama Ufunuo tu ni mfululizo wa vyombo ambavyo watu wanaweza kutumia kuboresha maisha yao. Lakini hawawezi kuboresha maisha yao kwa sababu hawajui wanachofanya. Hawapajui wanapoenda, na mawazo yao na imani yao, kwa mara nyingi, hayalingani na dhamira yao kubwa na mwelekeo wao wa kweli maishani.

Watu wanaweza kufikiri kuwa Mungu ni mkubwa na haeleweki, lakini wanajaribu kutumia Mungu kama aina ya mtumishi, kijana wa kutuma ujumbe wa tamaa, matarajio na shida zao. Wanasema, „Basi, ni nini Mungu anaweza kufanya kwangu? Ufunuo Mpya wa Mungu unaweza kuniletea nini?“

Unaweza kuona kutokana na maswali haya kuwa mtazamo na matarajio yao sio halisi. Hakuna mnyenyekeo. Hakuna heshima. Hakuna uelewa kuwa wanajadiliana na kitu kikubwa mno kuliko uelewa wao, kinachozidi matarajio yao, maadili yao na mapendeleo yao. Kwa hivyo ni nini Mungu anaweza kuwafanyia ila kuwatia moyo kupitia mabadiliko na disappointents za maisha ili waweze kukuja kwa ushiriki huu mkubwa na nia safi na mwelekeo wa unyenyekevu?

Ujumbe Mpya uko hapa kuokoa binadamu kutoka kwa msiba na kutiishwa katika ulimwengu mukianza kuibuka ndani ya Jumuiya Kubwa ya waangavu, Jumuiya Kubwa ambayo mumekuwa mukiishi na ambapo sasa itabidi mujifunze kukabiliana nayo.

Lakini uko hapa kuwapa watu binafsi ufarisi mpya, msingi mpya na fursa ya kurejesha maisha yao, kujikomboa na kutumia uwezo wao na nguvu ya Knowledge ndani yao ili waweze kutumikia dunia ambayo mahitaji na shida yake yanaaza kuzidi kila siku.

Watu wengi wamekata moyo katika utafuti wa maana kubwa, ama bado hawajauzalisha kabisa. Kwao Ufunuo Mpya utakuwa wa udadisi au kitu cha kuhukumu., kitu ambacho wanakitolea hofu yao, hukumu yao na malalamuko yao bila hata kuelewa kile wanachokitazama.

Kutakuwa na aina mingi ya majibu kwa hii, bila shaka, lakini itakuwa muhimu kwa wale ambao wanajibu kwa nia nyenyekevu na aminifu na safi watambue kuwa nguvu na uwezo wa Ufunuo wa Mungu na kile Ufunuo unaoweza kufanya kwao – kuwarejesha kuwapa dhamira na mwelekeo mkubwa, ambao tayari unaishi ndani yao.

Huvumbui dhamira na mwelekeo, kwa kuwa tayari umo ndani yako, unaweza kuona. Ni sehemu ya blueprint ya asili yako ya ndani, zaidi ya eneo ya akili. Zaidi ya majadiliano na uvumi. Unaweza kujadiliana nayo milele na milele, lakini inamanisha tu kuwa haujaelewa.

Ni muhimu kuwa watu ambao wanakuja kwa Ufunuo kwa uaminifu, wawe na uelewa hapo awali kuwa wanakabiliana na kitu kikubwa mno. Sio mafundisho tu kati ya mengine. Sio ahadi tu ambayo itawapa kile wanachotaka maishani. Ni wa eneo tofauti kabisa. Ndio maana ni Ufunuo Mpya kutoka kwa Mungu, Ufunuo peke yake kutoka kwa Mungu duniani kwa sasa.

Hii haimaanishi kuwa Ujumbe Mpya kutoka kwa Mungu utajenga maisha mapya kwako na ikupatie juhudi ya kufanya, kwa kuwa hii lazima itoke ndani yako – kati yako wewe mwenyewe, kati yako na ushiriki wako na maisha.

Watu wengi watahitaji Ujumbe Mpya uwe msingi wa mazoezi na focus yao, na watu wengine wataitwa kutumikita Ujumbe Mpya kwa sababu ni wito wao. Lakini kwa wengine, utawapatia nguvu ya kutambua mwelekeo mkubwa na kuwapatia nguvu na uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi yalio muhimu na kupiga kona ambazo lazima zipitiwe ili wasonge katika mwelekeo chanya na wa maana.

Kuna watu wengi duniani leo ambao wanajua kuwa lazima wajitayarishe kufanya kitu, ambao wanahisi wito wa ushiriki mkubwa, ambao wanahisi kuwa maisha yao ni muhimu kuliko shughuli za kawaida za kila siku. Baadh yao hawatapata njia katika duni za kitamaduni za dunia kwa sababu wanatayarishwa na wanaitwa kufanya kitu duniani. Wana muungano mkubwa wa mustakabali kuliko siku zilizopita, na mustakabali unawaita na unawavuta waende mbele.

Kuna watu ambao wana hatima ya kupokea Ufunuo wa Mungu kuusoma na kufanya mazoezi yake. Hawatapata njia yao popote pengine. Kama una hatima ya kitu cha ukubwa huu, hutapata uridhika ama utimizo popote pengine – ukijaribu kiwezekanacho, ukiamini kikamilifu iwezekanavyo. Ukijaribu kubadilisha maisha yako kama dikteta, bado hutaweza kufanya ushiriki wa msingi ila maisha yako inaelekea katika mwelekeo sahihi na asili ya ushiriki ambao unafaa kuwa wako unaweza kutambuliwa kabisa na kukubaliwa.

Ni kwa watu hawa ambao Ufunuo utatoa maisha mapya, sio tu kufanya maisha yao ya zamani iwe bora, sio tu kuhalalisha yale ambao wameyafanya ama hawajafanya hapo awali. Sio to kuwatia moyo na kuwaambia, „Basi, uko sawa. Kile umakifanya ni sawa. Ni kizuri.“

Hapana, Ufunuo utafanya makosa yako yawe wazi,dissapointments zako ziwe wazi, uhisi ukosefu wa mwelekeo kwa kiasi kikubwa. Labda utafanya mateso yako yazidi hapo mwanzoni hadi uweze kutambua zawadi ya kweli ya Ufunuo na utambue kuwa unaanza safari kubwa sana, labda safari ambayo umefunga kwa muda fulani ambayo sasa inaaza kuenda haraka.

Hapa hakuna mahali pa maafikano. Huwezi kujadili na Mungu. Huwezi kujadili na dhamira na hatima yako, kwa kuwa huwezi kuyabadilisha. Unaweza kuyaepuka, kuyakana ama kupitia njia ya kuyakubali na kuyadai.

Jinsi dhamira yako itaelezwa itategemea na hali ya dunia intakavyobadilika. Kwa hivyo kila kitu hakikuamuliwa hapo awali, bila shaka. Mafanikio au kushindwa kwako hakutalingana tu na ushiriki wako, lakini pia kwa ushiriki na utayari wa wengina ambao wana hatima ya kuwa na jukumi kubwa katika maisha yako. Wakishindwa hapa, itaathiri matokeo kwako, kwa kuwa maendeleo yako yanategemea maendeleo ya watu wengine maalum.

Utekeleza huu wa azma sio wa mtu binafsi ambapo unajaribu kujierevusha mwenyewe. Ni kujiunganisha na uungano na wenginw kwa dhamira kubwa. Wakishindwa, itaathiri matokeo kwako. Ukishindwa itaathiri matokeo kwao. Hii ndio maana kushindwa hapa kuna matokeo makubwa. Unafikiri kama bado unaishi katika utenganisho, kwa hivyo huwezi kuona hatima yako imeunganishwa na wengine.

Hawa ndio wale wengine ambao ni lazima uwapate maishani. Labda utu wao hautakuwa wa haiba ama kuwa na nyuso nzuri na tabia neema za jamii ambazo huvutia watu wengi. Labda hawatakuwa watu ambao ungewapenda ama una ushirika nao katika wakati uliopita. Wengi wao hawatashiriki maisha yako ya mustakabali nawe hata kama ulikwa na ushiriki nao katika wakati uliopita. Utahitaji Knowledge sasa. Kwa kuwa hiyo peke yake ndani yako ndio itajua. Itaona. Na itajibu.

Kama mtu mwengine bado hayuko tayari, basi, itakuwa janga kubwa kwako. Hii haimaanishi kuwa maisha yako yameisha. Inamaanisha kuwa itabidi mpango mwengine utengenezwe kwako. Na matokeo ni safari yako itakuwa ndefu na haitakuwa ya uhakika.

Kuna mengi hapa ya kutupa. Kuna ushawishi mingi ambao hautoi matokeo na ambao unaharibu mtu binafsi. Kuna matarajio mengi ambayo yanakuongoza ujitolee kwa kitu kabla haujajua kile ambacho unakifanya maishani, kabla haujaunda uhusiano na Knowledge, ambayo peke yake inashikilia dhamira yako na hatima yako kubwa.

Daima Mungu hatafunua yoyote kwa akili yako, sehemu ya akili yako ambayo imeshawishiwa na dunia na haiwezi kutegemewa na ni dhaifu na inaweza kushawishiwa kwa urahisi na nguvu zengine. Hapana, zawadi inapewa kwa sehemu yako ya ndani ambayo haiwezi kushawishiwa na dunia, haiwezi kushawishiwa na hisia na tabia zako ambazo zinabadilika, matumaini yako, hofu yako, furaha yako, janga yako – haiwezi kushawishiwa na haya yote. Inaishi katika kina cha bahari, sio katika ubapa wa mtikisiko.

Kuchukua hatua kwa Knowledge basi kunakuwa ni muhimu, ama maisha yako itakuwa maisha tupu – ukikimbilia watu, ukikimbilia ahadi, ukikimbilia tamaa zako, ukikimbilia ndoto, ukikimbilia matumaini, ukikimbia hofu, ukiogopa kuwa labda umepotea na uko peke yako, ukiogopa kuwa maisha yako hayatawahi kuwa sawa.

Knowledge inaishi zaidi ya eneo la tamaa na hofu, na hii ndio maana kuwa ina utulivu. Hii ndio maana ina nguvu. Hii ndio maana haibadiliki, na hauwezi kuibadilisha. Hii, hata hivyo, inawakilisha ukombozi wako. Licha ya kile unafikiria ama unafanya ama umefanya ama hujafanya, nguvu ya ukombozi inaishi ndani yako.

Sio lazima Mungu achambue hali yako. Mungu wa ulimwengu hajishughulishi na maisha yako. Lakini Mungu ameweka Knowledge ndani yako, inabeba ahadi yako na mwelekeo wako. Itawapata wale watu unafaa kuwapata. Italeta masahihisho, maelewano na balance katika maisha yako kama utaweza kuitambua na kuifuata na kuitimiza, pale ambapo inahitajika.

Hii ndio inajenga maisha mapya – sio maisha ya zamani ambayo yamerekebishwa, sio maisha ya zamani na mfumo mpya wa imani, sio maisha ya zamani na seti mpya ya nguo ama ufafanuzi wa dini wa kuvutia ambao sasa umekubaliwa katika jamii kwa sababu unasema na unafanya yale yote yalio sahihi.

Wewe sio aina ya mtangazo wa imani ya mtu mwengine. Kuna ahadi kubwa yako. Mungu anajali maisha yako kwa sababu Mungu anakupatia maisha mapya. Vinginevyo, Mungu angewacha kila mtu ashindwe na hangeshughulika nao. Hii ndio watu kwa ukweli wanaamini kwa sababu ukifikiri Ufunuo zote za Mungu zilipewa karne iliyopita na Mungu hana chochote cha kusema kwa binadamu, basi lazima uhitimishe kuwa Mungu hajali binadamu na hana chochote cha kusema binadamu akikabiliwa na vizingiti sasa, zote, ambazo binadamu hajawahi kukabiliwa nazo.

Mutakabiliana aje na dunia ya upungufu? Mutakabiliana aje na maingilio kutoka mataifa ya unyama kutoka ulimwengu ambayo yako hapa kupata faida kutokana na udhaifu na utenganisho wa binadamu? Mutakabiliana aje na mageuzi ya kisiasa na kiuchumi cha kiwango ambacho hakijaonekana hapa duniani?

Kama wewe ni mwaminifu, lazima uone kuwa hata hauna kidokezo. Lakini hii ndio hali ya dunia na kile lazima wewe na wengine pia mukabiliane nayo.

Mungu ametuma maandalizi ya Dunia Mpya kama sehemu ya Ujumbe Mpya. Mungu anatuma mipango ya maandalizi ya kuanza kuimarisha maisha mapya. Kuna Ujumbe wa dunia na kila mtu ndani ya dunia. Tena kuna Ujumbe wa mtu binafsi ambye anahisi kuwa ana dhamira kubwa na hatima duniani. Lazima kuwa uamue kama hii inakuzungumzia.

Mungu hakuvumbua dhana na imani yako. Mungu hakuvumbua mapendeleo yako na hofu yako. Mungu hakuvumbua dunia ambayo ni bidhaa ya mapendeleo na hofu ya kila mtu. Huwezi kulaumu Mungu kwa sababu ya hali ya kijamii ya binadamu. Huwezi kulaumu Mungu kwa sababu ya vita na ukatili, unyonyaji, utumwa na umaskini. Haya yote ni uvumbuzi wa binadamu yalio na msingi katika uchoyo na ujinga, yalio na msingi katita uchangiaji wa watu wachache tu duniani.

Lakini Mungu alivumbua uwepo wa Knowledge ndani yako, na ni Ufunuo Mpya wa Mungu ambao unafanya hii iwe wazi, bila kufunikwa na historia ama utafsiri wa binadamu na kuchanganya uelewa wako. Mfulilizo uko wazi. Ujumbe ni safi. Unaupokea kutoka chanzo chake, badala ya utafsiri ambao ulitolewa karne iliyopita kwa matumizi ya binadamu.

Kuwa na maisha mapya, lazima ufanye kazi. Sio uchawi unaowekwa kwako. Sio kuchukua maji ya uchawi na kufanya kila kitu kiwe tofauti. Sio aina ya addiction ama intoxication.

Lazima ufanye kazi. Lazima uchukue hatari, Lazima ufanya maamuzi. Lazima ukose kutimiza matarajio ya watu wengne. Lazima ukose kutimiza matarajio ya malengo na tamaa yako. Lazima ubadilishe mipango yako.

Hapa ndipo unapata nguvu. Hapa ndipo unaungana na wewe mwenyewe. Hapa ndipo ushirika wako wa kweli unaibuka kati ya uazimaji na wajibu wako kwa wengine. Hapa ndipo unapata nguvu yako na unaweza kujiamini. Hapa ndipi unawacha kuwa na tabia ya ujinga, ukitoa maisha yako kwa mambo ya ujinga na yasio na maana. Hapa ndipo unajua wale wa kuchagua kuwa nawe na jinsi ya kuepuka majaribu ambayo yatakuongoza pengine.

Unapata nguvu kwa sababu Knowledge iko ndani yako. Unavumilia matatizo kwa sababu Knowledge iko ndani yako. Unaweza kukabiliana na uchungo na upotevu, ugonjwa na hata kukataliwa na wengine ambao wanakujali kwa sababu nguvu ya Knowledge iko ndani yako. Na ukikutana na mwengine ambao ameendesha nguvu hii, uhusiano wako utakuwa katika eneo ingine – ya ajabu duniani, ukiwa na uwezo wa kutengeneza vitu vikubwa kuliko vile wewe peke yako unaweza kutengeneza.

Mungu anakupatia chanzo cha nguvu, lakini lazima ufanye mazoezi ya uongozi wake, na lazima uendeshe ujuzi wa kibinafsi ambao unakuwezesha uwe chombo cha Knowledge – mtu wa nguvu na uadilifu, mtu ambaye anayeweza kusisimua wengine na anaweza kuleta uwezo wa kujiamini, faraja na mwelekeo kwa wengine.

Huu ndio Ufunuo Mpya wa Mungu. Hii ndio inafaa kuzalisha. Lazima kuwe na wachagiaji walio na nguvu duniani sasa, ama binadamu atakabiliwa na upungufu mkubwa mno.

Uwache huu uwe uelewa wako.

Kuingia katika Jumuiya Kubwa

Ufunuo mpya kutoka kwa Mungu unafungua milango ya ulimwengu wa waangavu, ukitoa mtazamo, ufahamu na uelewa ambao hujawahi kutolewa hapo awali.

Familia ya binadamu haitambui kuwa iko dhaifu katika Jumuiya hii Kubwa ama katika uhusiano wake na Jumuiya hii Kubwa.

Imeishi katika upweke kwa muda mrefu, mtazamo wake mwenyewe, mtazamo wa Uumbaji na Uungu, unahusisha dunia hii moja peke yake. Lakini kuna watu wengi katika dunia leo ambao walio na mizizi katika Jumuiya Kubwa, kwa kuwa ufarisi wao wa zamani ulitokea hapo kabla waje dunia hii katika maisha haya.

Nyinyi ni kama kabila iliyotengwa ambayo haijawahi kugunduliwa na dunia ya nje, ambayo haijui kuwa kuna nguvu kubwa ambazo zinaishi karibu nayo na ambayo haijatayarishwa kukabiliana na ile siku ambayo uwepo wake utagunduliwa na walio nje.

Binadamu ameshinda akitangaza huko angani, bila shaka kama mjinga, na kwa hivyo uwepo wake umejulikana na majirani wake na vikundi vingine ambavyo vinachungilia dunia kwa makini.

Kwa wengine, mumekuwa mukichunguzwa kwa muda mrefu sana. Na hata kama wameona kuwa asili yenyu ya ndani haieleweki, tabia zenyu za nje zinaweza kutambuliwa na kutabiriwa kwa urahisi.

Munasimama katika kizingiti cha mazingira tofauti kabisa, ulimwengu ambapo viumbe havifanani na binadamu – ulimwengu ambapo maadili ya binadamu, matarajio ya binadamu hayathaminiwi na wengine, ulimwengu ambapo uwepo wenyu una muhimu au thamani ndogo, ila tu kwa mataifa ambayo yanataka kusaidia uhuru wa binadamu katika dunia ama kwa mataifa ambayo yanataka kuwanyanganya uhuru wenyu.

Jumuiya Kubwa itageuza jinisi mnajiona, na jinsi mataifa yanajadiliana hapa na ingine na vipaumbele vya binadamu. Athari yake inaweza kuwa ya faida kubwa mkiielewa vizuri.

Kwa kuwa ni Jumuiya Kubwa ambayo itashawishi mataifa yenyu yashiriki, yaungane kwa uhifadhi wa dunia na kwa ulinzi wa familia ya binadamu.

Ni Jumuiya Kubwa ambayo itawaonyesha kuwa hamuwezi kuendelea na migogoro yenyu ambayo haiihsi hapa duniani, na kuwa rasilimali yenyu ni ya thamani kubwa, na uwezo wenyu wa kujilisha hapa ni wa umuhimu mkubwa mno.

Na ufahamu huu, hamutaendelea kunyonya dunia kwa kiasi kile ambacho munafanya sasa. Hamutafikiri kama wajinga kuwa mtaweza kuchukua kile kilicho ulimwenguni mkimaliza mali ya dunia hii. Mtaelewa kuwa dunia hii tu ndio kile mlicho nacho. Dunia hii, mfumo huu wa Jua na Sayari zake, ndio kile mlicho nacho.

Nje ya hii, mnaingia mazingira ambayo yanamilikiwa na yanathibitiwa na wengine, na hamuwezi kuwanyanganya walio nacho. Hamujui sheria za ushiriki katikia ulimwengu ama mahusiano kati ya mataifa ama kile ambacho kinakubaliwa na kile ambacho hakikubaliwi katika Jumuiya hii Kubwa ya waangavu.

Nyinyi ni kama mtoto anayeingia katika mji mkubwa – bila makosa, bila kujua, bila ufahamu.

Watu wanataka mengi kutoka kwa wageni hapa. Wanatarajia mengi. Watu wanajiona kuwa hao ni muhimu katika ulimwengu na kuwa wengine bila shaka watakuja hapa kuwasaidia na kuwapa kile wanataka na kile wanahitaji. Watu wanafikiri kuwa Mawasiliano ni aina ya tukio la kusisimua, likizo kutoka mambo ya kawaida ya maisha ya binadamu. Wanataka kufikiri kuwa Mawasiliano haya yatakuwa mazuri sana na ya manufaa kwa sababu hawana nguvu, ujasiri au maandalizi ya kufikiria kwa njia yoyote ingine.

Ufunuo Mpya wa Mungu unawatolea dirisha ya kuangalia Jumuiya Kubwa, dirisha ambayo Mungu peke yake anaweza kutoa. Kwa kuwa hakuna lolote ulimwenguni ambalo Mungu halifahamu. Hakuna taifa ambayo inaweza kudai hivyo. Hatika taifa ambayo ina uelewa wa galaxy hii. Hakuna taifa ambayo ina uelewa wa asili ya ndani ya ubinadamu.

Hata yale mataifa katika sehemu hii ya anga ambayo yana uhuru na yanajitawala, hata hao hawawezi kuelewa maana kamili ya asili ya ndani ya binadamu.

Kila mtu ulimwenguni anatafuta rasilimali, na yale mataifa yameendelea kiteknolojia yanategemea rasilimali kabisa. Kamwe hamutawahi kufika mahali ambapo hitaji hili litaisha kwa sababu mukizidi kuendelea kiteknolojia, basi hitaji la rasilimali linazidi.

Binadamu haijui kuwa iko katika kizingiti kikubwa, pointi kubwa ya mageuko, pointi ambayo itatengeza mustakabali ambao ulio tofauti na siku za zamani. Ikiishi katika dunia ya upungufu. dunia ya rasilimali zinazopunguka na fursa ambazo zinapunguka. Serikali zenyu zimetumbukia katika shida zao za ndani na shida na serikali za taifa ziingine.

Dunia ni mahali pazuri sana, pakiwa na utajiri wa kibiolojia, pakiwa na rasilimali mingi ya muhimu ambazo hazipatikani kwa urahisi katika ulimwenngu ya dunia zilizo tasa.

Ufunuo wa Mungu lazima uwaamushe kwa ukweli, ugumu na fursa za kuibuka katika Jumuiya ya waangavu. Hakuna ufunuo yoyote ya zamani kutoka kwa Mungu ambayo ilihitaji kufanya hivi kwa sababi hitaji haikuwa hapo. Ubinadamu haukuwa umeendelea sana.

Lakini sasa muna tamaduni ya kidunia – iliyotenganishwa, iliyo katika migogoro, inayoharibu, isiyo na ufahamu na isiyowajibika, lakini hata hivyo ni jamii ya kidunia. Muna mawasiliano ya kidunia. Muna uchumi ya kidunia. Na kwa watu wengi, ufahamu wa kidunia. Ni katika pointi hii ambapo maingilio yatajaribiwa. Ni katika pointi hii ambapo binadamu itakuwa kama nyara ya kumilikiwa.

Wale ambao watakuja hapa na tayari wako hapa hawawezi kuishi katika mazingira ya kibiolojia kama mnayoishi na mumejifunza kuishi. Wanahitaji usaidizi kutoka kwa binadamu. Wanahitaji utii kutoka kwa binadamu. Wanahitaji ushiriki kutoka kwa binadamu ndio waweze kupata uwezo wa kutawala na kudhibiti hapa. Na watachukua faida kutoka kwa matarajio yenyu, tamaa yenyu, fantasies zenyu, na malalamiko yenyu ndio waweze kujiimarisha hapa.

Angalieni historia yenyu ya maingilio duniani. Angalieni vile watu wa kitamaduni walivyoshindwa katika uwepo wa maingilio ya kigeni. Hii sio lazima iwe hatima yenyu.

Mukianza kufikiri katika mazingira haya makubwa ya maisha. mutaanza kuona mambo ambayo hapo awali hamukuweza kuyaona. na mutaona kuwa umoja wa binadamu na ushiriki wa binadamu sio tu lengo ambalo linahitajika katika mustakabali au chaguo nzuri, ila ni muhimu kwa kuhakikisha uhuru na mustakabali wa familia ya binadamu.

Maingilio hayataki kuwaangamiza, lakini yanataka kuwatumia, kwa malengi yao wenyewe. Huu ni ukweli ambao hamuwezi kuepuka, na uongo ambao utatolewa kwa familia ya binadamu na pacification ambayo itatolewa kwa familia ya binadamu kusujudia na kutii ni mkubwa mno.

Watu wakipozeza imani kwa utawala na taasisi za binadamu, wataangalia nguvu ziingine kutoka ulimwenguni ziwaongoze, wakiamini kwa dhati kuwa nguvu ambazo zitakuwa za faida zitakuja hapa kurejesha na kuokoa binadamu. Ni tarajio hii, hamu hii, ingawa haitambuliwi, ambayo itatumiwa na Maingilio kwa malengo yao wenyewe.

Uhuru wenyu ni wa thamani kubwa, kwa kiasi chochote ambacho imeimarishwa duniani. Imepatikaka kutokana kwa njia ya juhudi kubwa na kwa kutolewa dhabihu kutoka kwa binadamu. Lazima ilinzwe kwa makini makubwa mno.

Mnashughilika na wengine katika mtazamo huu, lakini sasa mumepata shughuli kubwa, na shughuli hizo zimeleta hitaji kubwa ya kuwa na elimu kuhusu maisha katika ulimwengu na maandalizi ya ushiriki huu ulio mgumu na wa hatari kubwa mno.

Wale ambao ni washirika wa binadamu, mataifa yalio huru, hayataingilia shughuli za binadamu, kwa kuwa maingilio kwao ni ukiukaji. Wanatambuwa kuwa hata wakipata uaminifu wenyu, lazima waimarishe uwepo wa uthibiti hapa ndio waweze kuwaongoza katika Jumuiya Kubwa. Na hii, hawawezi kuifanya. Wanatambua kuwa binadamu lazima ipambane na iteseke, kufika katika pointi ya utambuzi na uwajibika kuhusu mustakabali wake na hatima yake hapa.

Wanaweza tu kutoa ushauri. Watatuma Maagizo, Maagizo kutoka Washirika wa Binadamu. Haya wameyafanya kama sehemu ya Ufunuo Mpya kutoka kwa Mungu, kwa kuwa Muumba anajua lazima mtambue kuwa hamuko peke yenyu katika ulimwemgu na uhuru na uwezo wa kujitawala upo na umepatikana na wengine. Lakini mafanikio haya hayakuwa rahisi kupata. Yana mahitaji ya msingi.

Watu hushtushwa na haya, sio kwa sabau ni ya uongo ama yanaonekana kuwa ni ya kusisimua, lakini kwa sababu hawajawahi kuyawaza, na hata hawataki kuyawaza, ni makubwa, ya ugumu na ya changamoto.

Lakini hii ni dunia yenyu. Hii ndio sababu umekuja. haukukuja kulala katika dunia iliyo nzuri, lakini kusaidi kuihifadhi na kulinda familia ya binadamu kutoka kwa upungufu na utawala wa kugeni.

Migogoro ya binadamu inawapoteza. Ujinga, upumbavu na ukosefu wa ufahamu kuhusu yale ambayo yanaishi katika mipaka yenyu, migogoro ya binadamu inawapoteza.

Huu ndio wakati wa ubunadamu upevuke, ukue wakubwa, utambue kuwa unaishi katika Jumuiya Kubwa ya waangavu – Jumuiya Kubwa ambayo hamuwezi kudhibiti, Jumuiya Kubwa ambayo iko zaidi ya juhudu yenyu, teknolojia yenyu na hata uelewa wenyu.

Hii ndio maana Muumba wa maisha yote analeta ufunuo kuhusu Jumuiya Kubwa katika dunia. Huu ndio wakati – kama binadamu anasimama katika ukingo wa dunia ya upungufu, dunia ya rasilimali zinazopunguka na dunia ya ukosefu wa utulivu wa kuichumi na siasa, wakati ambapo dini za dunia zinashiriki katika mgogoro na ushidnani unaoendelea kuhusu kukubalika na uongozi wa binadamu, wakati ambapo mataifa maskini hayana rasilimali za kutosha na mataifa tajiri yanaanguka katika madeni makubwa.

Huu ni wakati kamilifu wa maingilio. Ni wakati muhimu wa ufahamu mkubwa wa binadamu uibuke na kwa uwajibika mkubwa duniani – sio tu kwa taifa yake moja ama kikundi chake kimoja ama kwa dini yake, lakini kwa binadamu wote. Kwa kuwa taifa zikishindwa, basi dunia nzima itashindwa. Kama Maingilio yatafaulu katika sehemu moja ya dunia, hii itatia katika hatari mustakabali wa kila mtu hapa.

Watu wana manunguniko, wana mahitaji, wana, katika kesi fulani, mahitaji makubwa mno – umaskini na ukandamizaji. Viongozi wa dunia ni aidha vipofu ama hawawezi kushiriki yale waliomabiwa, wanaoona na wanajua. Kwa hivyo watu wa mataifa wanabaki wajinga kuhusu matukio haya makubwa ya historia ya binadamu, changamoto kubwa kwa uhuru wa binadamu na uwezo wake wa kujitawala na fursa kubwa ya umoja na ushirika wa binadamu.

Kwa kuwa hamutaweza kushiriki katika Jumuiya Kubwa ya waangavu kama muna vita na migogoro kati ya makabila na mataifa yenyu. Hamutakuwa na nguvu au ufanisi hapo, na udhaifu wenyu utakuwa wazi kwa wengine.

Ubinadamu unaharibu mali ya dunia, na hii pia imeleta maingilio.

Kuna mengi ya kujifunza. Haiwezi kuwasilishwa na maneno machache tu, lakini kwa mfumo mkubwa wa mafundisho, ambao ni sehemu ya Ufunuo wa Mungu.

Hapa mkristo lazima awe mkristo na ufahamu wa Jumuiya Kubwa. Muislamu lazima awe muislamu na ufahamu wa Jumuiya Kubwa. Buddhist ama Myahudi anapata panorama kubwa ya maisha ambapo mafundisho yake ya kidini lazima yawe ya muhimu. Kama dini duniani itakuwa ya kufunza na kuerevusha, lazima iwe na uwezo na ufahamu huu.

Hamuwezi kuwa wajinga mukikabiliana na Jumuiya Kubwa ama mukikabiliana na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko ambayo yanatokea duniani. Ni wakati wa kupevuka.

Binadamu ana nguvu yake. Hamujapoteza uhusiano na Knowledge ya ndani ambayo inaishi ndani ya kila mtu. Hamujakuwa jamii ya kijeshi, ya kidunia, ya kiteknolojia, ambayo ni kama kawaida ulimwenguni. Hamujapoteza uhuru wenyu ama hisia zenyu kubwa ingawa haya yote yanatokea kila siku.

Mahitaji ya maisha ni muhimu kila mahali. Teknolojia ya juu haitafanya muepuke mahitaji haya kikamilifu na kwa kweli inaweza kuyasambaza kwa kiasi kikubwa. Kweli munafikiri kuwa jamii kubwa ya kiteknolojia kutoka Jumuiya Kubwa haihitiaji rasilimali, rasilimali ambayo sasa haiwezi kutengeneza na ni lazima wafanye biashara na wayatafute, kutoka mmbali na dunia yao? Wamepoteza uwezo wao wa kujitawala. Wanadhibitiwa sasa na mitando ya biashara ambayo sasa wanaitegemea.

Kuwa na uhuru ulimwenguni lazima muwe na uwezo wa kujitawala, lazima muwe na umoja na lazima muwe na siri. Haya ndio mahitaji ambayo kila taifa inahitaji, kila taifa lazima iimarishe katika Jumuiya Kubwa ya waangavu.

Hapa munaona hatari na mvuto wa binadamu akipokea teknolojia na rasilimali kutoka nje ya dunia. Huu utakuwa mvuto mkubwa mno!

Mukipoteza uwezo wenyu wa kujilisha, kila kitu ambacho munathamini kitapotea, kwa sababu hamutaweza kuimarisha masharti ya kushiriki ili muweze kupata vitu vyote ambavyo sasa mnavyovitegemea. Mataifa ingine yataamua tabia yenyu na ushiriki wenyu. Hii ni ukweli wa maisha.

Hamuwezi kujaribu kutawala ulimwengu wenyu wa karibu mtapingwa na kila mtu. Hii ni picha tofauti kuliko ile picha ya filamu zenyu na science fiction zenyu na fantasies zenyu, matumaini yenyu, matarajio yenyu yasiotajwa. Hii inatoa picha tofauti na umuhimu wa umoja na ushiriki wa binadamu hapa duniani, umuhimi wa kulinda na kujenga uhuru wa binadamu na nguvu na uwepo wa Knowledge ambayo Mungu ameweka ndani ya kila mtu.

Hapa uhuru sio tu kujitumbukiza kwa mambo na kukosa kuwajibika kwa mtu yeyote au kitu chochote. Inakuwa kitu cha muhimu katika ushiriki wa maisha yako. Hapa vipawa vyako vikubwa vinaweza kutoka mbele, kwa kuwa unatambuwa uko hapa kutoa huduma katika hitaji na hatari kubwa ya binadamu. Hapa kila kitu ndani yako kilicho cha kweli na asili kinaanzishwa na kinaitwa. Hapa mataifa yanawacha mogogoro yao yasioisha na yanajaribu kujenga uimara kwao wenyewe na kwa majirani wao ndio wahakikishe usalama wao wakati wa mustakabali na kujilinda kutoka maingilio kutoka nje.

Dunia haitachukuliwa kwa nguvu, kwa sababu hii hauruhusiwi katika sehemu hii ya ulimwengu. Itachukuliwa kupitia mvuto na ushawishi, kupitia kupata faida kutoka kwa udhaifu na migogoro ya binadamu, ushirikina wa binadamu na mahitaji ya binadamu ambayo hayajatimizwa.

Kushambuliwa kwa kutumia nguvu hakutumiwi katika sehemu hii ya ulimwengu. Njia ya hila ndogo lakini ilio na matokeo makubwa inatumiwa ndio rasilimali za dunia zihifadhiwe na uwezo wa kutawala upatikane kwa kutumia ushawishi, oungo na siri. Ubinadamu ni taifa ambayo iliyo clumsy na iliyo na vurugu katika mtazamo huu, lakini hata hii inabadilika hapa Duniani.

Tunawapa mtazamo huu kwa sababu hii inawakilisha upendo wa Muumba. Ingawa itakuwa ni kubwa na ya kutisha mara ya kwanza, ni ukweli ambao lazima muwe na ufahamu wake na muuzoee. Sasa ni lazima mufikiri sio tu kwa kujitazama wenyewe ama jamii yenyu ama taifa yenyu, lakini kwa dunia nzima kwa sababu hii itaamua hatima yenyu na usalama wa watoto wenyu na watoto wa dunia.

Huu ni mgeuko mubwa wa ufahamu, mgeuko ambao ni mkubwa na wa muhimu. Watu watapinga haya, bila shaka. Watakimbilia dini yao. Watakimbilia ideolojia yao ya siasa. Watakimbilia fikira za binadamu. Lakini maisha katika ulimwengi haitegemei haya. Sio swala la mtazamo. Sio swala la ideolojia. Ni swala la kuwa makini, kujiangalia, kujiona bila hukumu na kuwa mwaminifu kwako mwenyewe.

Hii ni changamoto kubwa, lakini ni changamoto inayohitajika, changamoto inayokomboa kama inaweza kukabiliwa kwa uaminifu na kwa dhati. Muna macho ya kuona na masikio ya kusikia, lakini hamuangalii na hamusikilizi. Kila mtu karibu na wewe anaonekana kuwa yuko obsessed, na shughuli ama anakandamizwa. Ni nani atazungumza na hao? Labda hawatasikia maneno yetu. Ni nani atazungumza na hao?

Unahitaji tu kupointi kwa Ufunuo, kwa sababu Ufunuo ni mkubwa mno kiasi mtu moja peke yake hawezi kuielewa. Pointi kwa Ufunuo, kwa kuwa hii peke yake inashikilia maandalizi kwa mustakabali na hatima ya binadamu kaitka dunia inayoibuka.

Mungu anapatia binadamu kile ambacho binadamu hawezi kujipatia mwenyewe. Mungu anaagiza binadamu ndio awe macho kwa hatari na fursa akisimama katika kizingiti cha anga. Mungu anaagiza binadamu awe macho kwa hatari na fursa na umuhimu wa kuishi katika dunia ya upungufu. Mungu analeta duniani ufafanuzi wa asili na dhamira ya kiroho cha binadamu, asili na dhamira ambayo imepotea na imevikwa katika Ufunuo kutoka kwa Mungu za hapo awali.

Ufunuo ni mkubwa mno. Unazungumzia mambo mengi. Hamuwezi kufanya iishe, na lazima muitumie na mushiriki ukweli wake na wengine. Ni hapo tu ambapo mutaona maana yake halisi na kwa nini ni muhimu na kwa nini inashikilia ahadi kubwa ya mustakabali na uhuru wa watu wa dunia.

Kwa kuwa hakuna uhakika wa mafanikio. Watu wengi katika ulimwengu wameanguka kwa ushawishi na utawala. Imefanyika mara isiyohesabika. Ni tukio lisilozuika kwa watu ambao hawajaonywa na kutayarishwa kushiriki na mazingira makubwa ya waangavu.

Tahadharini fantasies na matarajio yenyu. Yajadili. Yafikirie katika mwangaza wa ukweli wa asili na historia ya binadamu.

Ukiwa mwaminifu kwako mwenyewe, lazima ukuje kuona kuwa hujui kile kilichi zaidi ya mipaka ya dunia hii, na matarajio ya matumaini yanaweza kukuvika. Lazima utayarishwe kwa kitu chochote, kama vile lazima utayarishwa kwa kitu chochote kinachofanya kazi hapa duniani – katika mahusiano ya binadamu na katika shughuli za maisha yenyewe.

Kuwa na uhuru lazima uwe na nguvu. Kuwa na nguvu lazima uwe wazi. Lazima uone wazi. Lazima usikie ukweli. Lazima uwe na mtazamo usio na hukumu kuhusu maisha yako na hali yako. Lazima uangalie dunia sio kwa kunungunika au kuepuka, lakini kwa huruma, uvumilivu na uamuzi. Kama lazima mujenge msingi wa mustakabali mpya hapa, kuchangia sehemu yako ndogo lakini muhimu hapa, lazima muwe na mtazamo huu.

Pokea zawadi hii ya upendo na Ufunuo. Inakuja na uwajibika mkubwa, lakini pia na nguvu kubwa na ahadi kubwa.

Bado hauishi ile maisha unafaa kuishi kwa sababu maisha yako haiko kaitka ushiriki na Ukweli Mkubwa ambao unaishi ndani yako na karibu na wewe. Kwa binadamu, hii ni pointi kubwa ya mageuko. Na kwako wewe, hii ni pointi kubwa ya mageuko.

Watu wa dunia lazima waamuke kwa Jumuiya Kubwa na kwa hali ya dunia ambayo wanaishi. Lazima mujifunze kuhusu nguvu yenyu kubwa na hekima yenyu kubwa ambayo Mungu ameweka ndani yenyu iwaongoze, iwatayarishe na iwalinde.

Mungu amezungumza tena. Ni kwa dhamira kubwa ya kukabiliana na seti kubwa ya mahitaji.

 

Maandalizi ya kukabiliana na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko.


Mabadiliko Makubwa yanakuja duniani, mabadiliko tofauti na kitu chochote ambacho binadamu kwa ujumla amewahi kuona hapo awali – Mawimbi Makubwa ambayo yanakusanya kwa wakati huu. Kwa kuwa binadamu ameathiri dunia kwa njia nyingi, na matokeo ya athari hiyo inakusanyika sasa – nguvu yake inakusanyika sasa, inakusanyika katika wakati binadami kwa kiasi kikubwa hajui kuihusu na hajajiandaa.

Mawimbi haya Makubwa sio tukio moja peke yake. Sio kitu kimoja kidogo ambacho kinatokea wakati moja peke yake, kwa kuwa binadamu ameweka katika mageuzi nguvu za mabdasiliko ambazo sasa lazima akabiliane nazo kwa muda unaoendelea. Kwa kuwa sasa munaishi katika dunia ya rasilimali ambazo zinapunguka, dunia ambapo hali ya hewa imeathiriwa kwa kiasi kikubwa, dunia ambayo hali ya ikolojia inazorota, dunia ambayo binadamu lazima akabiliane na tarajio ya upungufu mkubwa wa chakula na maji na hatari ya magonjwa katika eneo kubwa, hata ikiathiri mataifa yalio tajiri ya dunia. Mizani sasa imebadilishwa, na fanilia ya binadamu kwa jumla lazima iungane na ikusanyike kukabiliana na mabadiliko haya makubwa.

Katika dunia ambapo idadi ya watu inaongezeka na rasilimali zinapunguka, ubinadamu utakabiliana na uamuzi mkubwa, uamuzi wa msingi ya njia ya kuelekea. Je, mataifa yatashindana na kuwa katika migogoro kwa kupata rasilimali zilizobaki? Watafanya vita na migogoro kuhusu nani ambaye atadhibiti rasilimali hizi na ni nani atamiliki rasilimali hizi? Kwa kweli, vita vyote vikubwa vya historia ya binadamu, vimekuwa mapambano, kwa msingi, juu ya kupata na kudhibiti rasilimali.

Je, mataifa yalio tajiri katika dunia yatasisitiza kuwa staili ya maisha yao lazima ihifadhiwe na hivyo kuingia katika ushindani na migogoro na mataifa ingine, wakizidi kuaziri dunia, wakiiba kutoka kwa maskini wa dunia uwezo wao wa kujilisha ndio staili ya maisha makubwa na ya ustarehe iendelezwe katika mataifa tajiri?

Binadamu ikichagua njia hii, itaingia katika hali ya migogoro ya muda mrefu na hali ya upungufu wa kudumu. Badala ya kuhifadhi na kusambaza rasilimali zilizobaki na kujenga uwezo wa kuishi katika hali ya dunia mpya, binadamu itaharibu kile kilichobaki, na itajiweka katika hali ya umaskini na upungufu, na upotevu mkubwa mno wa maisha ya binadamu na matarajio ya mustakabali usio na matumaini.

Lakini bunadamu ikichangua njia tofauti, kwa kutambuwa hatari kubwa inayohusika kwa kukabiliana na Mawimbi haya Makubwa ya Mabadiliko, ikitambua ukubwa wa ukweli na matukio makubwa ambayo yanaweza kutokoea kwa usalama na mustakabali wa binadamu, basi watu na viongozi wa mataifa na dini walio na hekima wanaweza kutambuwa kuwa ubinadamu ulio tenganishwa utashindwa ukikabiliana na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko. Lakini katika umoja, ubinadamu unaweza kujenga njia mpya, kujitayarisha kwa athari za Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko na kuanzisha ushiriki mkubwa na umoja mkubwa kuliko ule binadamu amewahi kuwa na ufarisi wake hapo awali. Hii itaanzishwa sasa, sio kwa sababu ya kanuni za dini ama maadili ya juu, lakini kwa sababu ya hitaji kubwa yenyewe.

Kwa kuwa ni nini taifa moja inatarajia kutimiza kama dunia inatumbukia katika migogoro na upungufu? Mataifa ya dunia yanategemea mataifa ingine kwa kiasi sasa hakuna anayeweza kuchagua njia ya vita na migogoro bila kuleta janga na upungufu kwa kila mtu.

Pamoja, mutakuwa na fursa kubwa. Mukigawanywa, mutashindwa. Na kushindwa kwenyu kutadumu, na kutaleta hasara kubwa mno – hasara kubwa kuliko vita vyovyote ambavyo vimewahi kutokea hapa duniani, vya hasara kubwa kuliko mgogoro wowote wa binadamu ambao binadamu amewahi kujua.

Maamuzi ni machache, lakini ni ya msingi. Na maamuzi hayo sio tu ya viongozi wa mataifa na taasisi ya dini, ila ya raia wote. Kila mtu lazima achague kama atapigana na kushindana, kama atapinga Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko, kama atapambana na mwengne ili aweze kuimarisha staili ya maisha ambayo anashikilia. Ama atatambua hatari kubwa, na ataungana na mwengine na kuanza kujiandaa kwa athari ya mabadiliko na kujenga aina ya mustakabali iliyo mpya na tofauti?

Kwa kuwa hamuwezi kuimarisha vile munaishi sasa. Hayo mataifa yalio tajiri, wale watu walio tajiri, wale watu ambao wamezoea ustaarabu, wakiona kuwa ni haki yao kutoka kwa Mungu na kutoka kwa maisha – lazima wakuwe tayari kubadilisha vile wanaishi, na kuishi maisha ile siyo ya utajiri, kuishi maisha ya kugawa na wengine, kwa kuwa kushiriki rasilimali zilizobaki itahitaji wafanye hivi.

Matajiri lazima watunze maskini, na maskini lazima wajitunze wenziwe, ama kila mtu atashindwa, tajiri na maskini. Hakutakuwa na washindi jamii ya binadamu ikishindwa. Hakutakuwa na taifa kuu. Hakutakuwa na kabila ama kikundi ama taasisi ya kidini kuu tamaduni ya binadamu ikishindwa. Na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko yana nguvu ya kuangamiza tamaduni ya binadamu. Huu ndio ukubwa wake. Hivi ndivyo athari yake itakuwa kubwa na itadumu.

Kwa hivyo, changamoto ya kwanza na inayowakabili ni kukabiliana na changamoto hii – bila kusisitiza kupata suluhisho, bila kupinga ukweli wa kile unajua na kile unaona, bila kulaumu watu wengine ama kutarajia mtu mwengine atafute suluhisho badala yako. Kila mtu lazima awajibike kwa vile anaishi, kwa vile anafikiri, kwa kile anafanya, kwa maamuzi yalio mbele yake sasa, na kwa maamuzi ambayo itabidi akabiliane nayo siku za baadaye. Kila mtu, haswa wale wa mataifa yalio tajiri, lazima wafikirie upya pale wanaishi, jinsi wanaishi na aina ya kazi ambayo wanafanya, vile wanajilisha, na vile wanatumia rasilimali za dunia, vile wanatumia nishati – haya yote.

Huu sio wakati wa kutokuwa na uamuzi kuhusu maamuzi yako ama kujilaumu. Kwa hakika sio wakati wa kufikiri kuwa viongozi wa serikali lazima watatue tatizo kwako, kwa kuwa lazima sasa uangalie maisha yako na hali yako.

Ni kama bili imetolewa kwa binadamu. Binadamu amekuwa akitumia na kukopa kutoka kwa urithi wake wa asili kwa muda mrefu, akiweka kando malipo ya matukiio yake kwa muda mrefu, na sasa bili imetolewa. Sasa matukiio yanaibuka kikamilifu, na matukio ni mengi.

Sasa lazima mukabiliane na yale mumejenga. Lazima mukabiliane na hali yenyu. Lazima mukabiliane na dunia ambayo munaijenga kwenyu wenyewe. Kwa kuwa binadamu amepatanya urithi wake wa asili. Hii dunia iliojaa kibiolojia na iliyo nzuri ambayo Muumba wa maisha yote amewapa binadamu kama dunia yake yenyewe, imenyonywa na kupatanywa na kupotezwa – kupitia uchoyo, kupitia ufisadi, kupitia vita na migogoro, kupitia kutowajibika, kupitia kutojua na ujinga – na sasa matokeo yanaanza kujitokeza. Sio tu uwezekano wa mbali ama tatizo la kizazi cha baadaye.

Hii ndio dunia umekuja kutumikia. Hii ndio dunia umetengeneza. Hii ndio hali ambayo unakabiliana nayo sasa. Lazima ukabiliane nayo. Lazima uwajibike kuwa umechanga sehemu yako ndogo kwa kuijenga. Lazima uitikie uwajibika huu bila aibu, lakini hata hivyo uwajibike. Kwa kuwa katika makabiliano na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko, hakuna mahali pa kukimbia na kujificha. Huwezi tu kufunga virago vyako na uhame ushambani ama kutafuta mahali pa kujificha hadi dhoruba hii ipite, kwa kuwa dhoruba hii itadumu muda mrefu, na hakuna pa kujificha.

Ni Knowledge peke yake ndani yako, akili kubwa ile Mungu ameiweka ndani yako, itakayojua namna ya kukabiliana na hali hii na mabadiliko makubwa ambayo yanatokea kwa binadamu. Ni Knowledge hii ya ndani, hii Knowledge takatifu, ambayo itajua jinsi ya kusafiri katia siku ngumu mbele yako, ndio itajua jinsi ya kupandisha tanga katika maji isiyotulia, kwa kuwa kutakuwa na maji ambayo hayatulii.

Labda mezoea kuishi bila kusumbuliwa na shida kubwa za dunia. Labda umejizuia kwa kiasi fulani ambapo zinaonekana kuwa ni za mbali, ambapo hazionekani kuwa ni shida kwako. Zinaokenaka kuwa ni tatizo la mtu mwengine, tatizo la taifa ingine, tatizo ambayo watu wengine lazima wakabiliane nayo. Lakini insulation hii imeisha. Haiwezekani kuwa hutaathiriwa kwa kiasi kikubwa na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko. Haiwezekani kuwa hayatabadilisha hali yako, labda pia kwa kiasi kikubwa mno.

Kwa asili huwezi badilisha kile kinakuja sasa, lakini unaweza kujitayarisha kukabiliana nacho. Unaweza kubadilisha maisha yako ili uweze kuishi. Unaweza kuitumia ili kuchangia kwa usalama wa watu, kwa kuwa hii ndio sababu umekuja duniani. Katika eneo kubwa, zaidi ya mawazo na imani, kuna ukweli ambao umekuja duniani kwa misioni, kwa kuwa uko hapa kwa dhamira na kuwa Mungu amekutuma hapa duniani kuchangia duniani, katika hali hii ambayo inatokea.

Kwa hivyo, akili yako ikijibu kwa hofu na wasiwasi, kwa hasira – labda unaweza kuchanganyikiwa na kushangaa, labda utahisi kuwa huna nguvu na uwezo kaitka uso wa changamoto hii kubwa – lakini ndani yako, katika eneo ya Knowledge, huu, kwa kweli, ndio wakati wako. Huu ndio wakati ambao wito mkubwa utatoa sauti kwako. Huu ndio wakati ambapo vipawa vyako vikubwa vitatoka mbele, kwa kuwa wewe mwenyewe huwezi kuvifanya vitoke mbele. Lazima viitwe kutoka kwako. Na wito lazima utoke kwa dunia, kwa sababu huwezi kujiita mwenyewe kama wito wenyewe utakuwa halisi. Huwezi kujisisimua kwa maisha makubwa. Kwa kuwa wito lazima utoke nje yako – ukiita vipawa vyako kutoka kwako, ukikuita kwa hali kubwa ya akili na ufahamu na kwa sehemu kubwa ya kuwajibika.

Bila wito huu, utakana na kujaribu kusahau na kubaki mjinga na mpumbavu, ama utapigana na kupambana ili kuhifadhi zile haki ambazo unahisi unazo ama lazima uwe nazo. Utatenda kutokana na hofu na hasira. Utakasirikia wengime. Utakuwa na hofu kubwa mno na utachanganyikiwa kabisa. Utaamini kuwa kitu kitakukomboa, kuwa kuna suluhisho katika upeo wa macho ambayo itafanya shida zote ziende. Hautaona na hautajua na hautajiandaa. Na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko yakija, hutakuwa tayari, na utakuwa mdhaifu.

Kwa kweli umeona kuwa asili haina huruma kwa wale ambao hawajajitayarisha. Asili haionyeshi huruma kwa wale ambao hawajajitayarisha wa matukio. Mungu anapenda kukuokoa kutoka kushindwa, migogoro na ugomvi. Hio ndio maana Knowledge imewekwa ndani yako. Mungu anajua kile ambacho kinakuja kwa binadamu. Lakini watu wanabaki vipofu na wajinga na wanajitumbukiza kwao wenyewe. Mungu anajua kuwa ukikosa kujiandaa, ukikosa kuwa na nguvu ya Knowledge, ukikosa kuruhusu vipawa vyako viitwe mbele, ukikataa kuwacha maisha yako ya zamani, na seti ya mawazo na dhana, basi utashindwa. Na kushindwa kwako kutakuwa kubwa mno.

Lakini Knowledge ndani yako iko tayari kujibu. Haiogopi Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko. Kwa kweli, imejitayarisha kwa Mawimbi haya wakati huu wote, kwa kuwa hii ndio hatima yako. Haukukuja duniani tu kuwa mlaji, ama tu kujaza nafasi, kuharibu dunia na kutumia rasilimali zake. Haya sio yale yalikuleta hapa, na kwa roho yako unajua kuwa hii ni ukweli. Lakini kile unajua ni ukweli na kile unafikiri bado sio kitu kimoja. Na ni lazima uzilinganishe na Knowledge na ujifunze Njia ya Knowledge na uchukue Hatua kwa Knowledge ndio iwe mwongozi na mshauri wako.

Utahitaji uhakika huu wa ndani, kwa sababu kutakuwa na mchanganyiko, hasira na migogoro wakati watu wakinyimwa, watu wakihisi kuwa wanatishwa na ulinzi wa wao kila mahali ukiwekwa katika changamoto. Utaona watu na vikundi vikijibu kwa hasira. Utaona mataifa yakitisha ingine, na hii tayari inatokea. Na migogoro mikubwa ambayo yatatokea na hatari kubwa ya vita yatavikwa barakoa ya siasa na dini, lakini kwa kweli migogoro ni ya rasilimali. Ni nani atabaki na rasilimali hizi? Ni nani atadhibiti rasilimali hizi?

Migogoro hii tayari imeanza na inaendelea. Na hatari ya migogoro mikubwa, ya vita kubwa, inakuwa kubwa kila siku. Tayari kuna moto ambao unachomeka duniani, na makaa ya migogoro mikubwa yanawashwa, na hali ya matukio yake imekomaa.

Kwa kweli, ukitaka kulindwa na kupata faida kutokana na mabadiliko ambayo yanatokea, huwezi kubaki katika hali yako ya sasa, katika mawazo yako ya sasa, katika dhana zako za sasa. Lazima kuwe na badiliko kubwa ndani yako, na badiliko hii italetwa na hali ya dunia na kuibuka kwa Knowledge ndani yako. Huwezi kubaki mahali upo kiakili, kisaikolojia na kihisia na kuwa na imani ya kweli ya kuishi na kupata faida kutoka mabadiliko makubwa ambayo yanakuja.

Hii ndio onyo kubwa ambayo Ujumbe Mpya inaeleza. Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko yanakuja duniani, na binadamu sasa anakabiliwa na ushindani kutoka nje ya dunia – maingilio kutoka mataifa nje ya dunia ambayo yanataka kupata faida kutoka kwa binadamu iliyo dhaifu na isiyo na umoja, ambao wanataka kupata faida kutoka kwa upungufu wa tamaduni ya binadamu.

Mafundishi ya Ujumbe Mpya yanaeleza ukweli hii kikamilifu. Na sio vigumu kuelewa wakati ambao utawacha ulinzi wako, utaweka kando mapendeleo yako, wakati ambapo utaangalia na macho yalio wazi na utasikiza dunia ndio uweze kuona na kujua.

Lakini, kwa kushangaza, akili ya kawaida sio ya kawaida. Labda watu wamepotea kwa yale wanataka ama yale wanaogopa kupoteza. Wamepotea kwa migogoro yao, malalamiko yao, mapambano yao na hao wenyewe na wengine. Kwa hivyo yale ambayo yako wazi na ya kawaida kuona, kusikia, kujua na kufanya yanapotea – yakishindwa na shughuli za binadamu, tamaa ya binadamu na migogoro ya binadamu.

Bila shaka, binadamu inafika katika kizingiti kikubwa sasa ambayo itaamua hatima yake na mustakabai wake. Ushahidi wa hii uko karibu na wewe, na unawza kuuhisi ndani yako – hisia ya wasiwasi, hisia ya ukosefu wa utulivu, mchanganyiko, matarajio ya hofu. Ishara za dunia zinazungumza na wewe – zinakuambia kuwa mabadiliko makubwa yanakuja, kuwa yako katika mlango wenyu.

Unaweza kuyahisi haya, ukijiruhusu kuyahisi – bila kujaribu kujificha ama kuyatoroka, bila kusisitiza kuwa uwe na furaha na bila shughuli, bila kutafuta mambo yasio na faida ndio akili yako ijae shughuli mingi na iwe distracted ndio usisikie ishara za dunia, wito wa dunia na harakati ya Knowledge ndani yako.

Huu ndio wakati wako. Hii ndio sababu umekuja. Haya ndio matukio makubwa ya wakati wako. Hiki ndicho kizingiti kikubwa ambacho binadamu anakabiliana nacho, kwa kuwa sasa lazima mukabiliane na mustakabali ambao utakuwa tofauti na siku za zamani. Maisha haitaendelea kama vile munavyoijua, bila kupingwa. Binadamu haitapata tu chanzo kiingine cha nishati ama suluhisho la uchawi ili kuimarisha mapendeleo ya wachache.

Kwa kuwa munaishi katika dunia ya upungufu. Yale rasilimali ambayo yanapatia mataifa mali, ulinzi na utulivu yanapungua. Mazingira ambayo munaishi yako katika hali ya shinikizo ambayo inaongezeka kupitia uharibifu wa mazingira, kupitia mabadiliko ya hali ya hewa na kupitia athari mingi ambazo zimetokea kwa muda mrefu ndani ya dunia.

Kwa hivyo, munasimama katika poromoko. Je mutaamua kubaki wajinga na mutapigana na kupambana wakati ujinga wenyu na kukana kwenyu kumeshindwa? Ama mutaamua njia ya ujasiri na hekima kwa kujiandaa na kuruhusu zawadi kubwa kutoka kwa Mungu ya Knowledge iwaongoze?

Kujua maana ya zawadi kubwa ya Mungu, lazima muone ukubwa na kina ya changamoto inayokabili binadamu. Lazima muhisi hitaji ndani yenyu, mukitambua kuwa nyinyu wenyewe hamuna majibu na hata mataifa yenyu na wasomi wenyu na wanasayansi wenyu kwa kweli hawana majibu. Wana majibu ya baadhi ya matatizo. Wanafanya kazi kwa kuandaa binadamu, lakini binadamu yuko nyuma sana kwa kujiandaa kukabiliana na Mawimbi Makubwa ya mabadiliko. Hakuna wakati wa kutosha, na hamuko tayari.

Kwa hivyo lazima muhisi hitaji halisi ndani yenyu kujibu zawadi kubwa ile Mungu amewapa – zawadi tofauti kuliko kitu chochote ambacho binadamu amewahi kupokea hapo awali – kwa kuwa binadamu anakabiliwa na changamoto na tatizo tofauti kuliko kitu chochote ambacho binadamu amewahi kukabiliwa nacho.

Kuona suluhisho, lazima muhisi hitaji. Lazima mutambue hitaji. Lazima mukabiliane na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko. Lazima muanze kuweka pamoja sehemu na ishara ili muweze kuona ile picha ambayo inawaonyesha. Picha hii iko wazi na dhahiri, lakini sio dhahiri kwa wale ambao hawaangali, ambao hawafikirii, ambao hawafanyi ushirika wa msingi ambayo inafaa kufanywa kama unaweza kuona picha kwa uwazi.

Tukio lolote la ujasiri ambalo ni la kubadilisha malengo yako na nguvu yako daima lazima liwe na msingi katika hitaji na shinikizo ya ndani. Katika mazingira ya utilivi ni nadra kwa watu kuendelea katika eneo lolote la maisha. Maendeleo ya kweli lazima iendeshwe na hitaji kubwa mno ya ndani – shinikizo kutoka kwa mazingira na kutoka kwa mahitaji ya dunia na pia kutoka kwa Knowledge ndani yako. Knowledge inakuongoza uwe na ufahamu. Inakuongoza ujitayarishe kisaikolojia, kihisia na kwa matendo kukabiliana na changamoto kubwa ambayo yanakuja sasa, kwa matukio makubwa ya maisha yako na kwa mahusiano makubwa ambayo unafaa kuwa nayo. Lakini mahusiano haya yatatokea tu ukikabiliana na changamoto kubwa ya maisha.

Usijali kuwa wengine hawajibu. Usijali kuwa binadamu inabaki katika hali ya ujinga na upumbavu katika ushindi na migogoro yake. Kwa kuwa wito ni wako. Lazima uwajibike kwa maisha yako na dhamira yako ya kuwa hapa. Wito ni wako. Hauhitaji makubaliano na wengine ili uweze kujibu. Hata kama hii ndio kesi, lazima ujibu. Huwezi kusubiri wengine wakupatie uthibiti kuwa unafaa kujibu, kwa kuwa wakati kila mtu atajibu, kutakuwa na hofu na ugomvi. Kutakuwa na dhiki na migogoro. Hutaki kusubiri hadi wakati ambapo kila mtu anajibu, kwa kuwa kutakuwa na ukosefu wa utulivu.

Lazima ujitayarishe na utayarishe maisha yako. Lazima uimarishe mahusiano yako. Lazima ufunze watu walio karibu nawe- wale ambao wanaweza kusikia na wanaweza kujibu. Lazima uweke kando malengo yako na mapendeleo yako ndio uweze kujibu dunia. Lazima ufikirie upya mahali ambapo unaishi, jinsi unavyoishi na wale ambao uko nao katika swala la ni nani anaweza kusafiri na wewe, ni nani anaweza kujiandaa na wewe na ni nani hawezi. Lazima ufikiri upya kazi yako na umuhimu wake katika mustakabali. Na lazima uyafanye haya yote bila kutiwa moyo na wale walio karibu na wewe ama wakubali na wewe, kwa kuwa hii labda haitawezekana.

Akili yako haitataka kukabiliana na siku za baadaye. Akili yako haitataka vitu vingine kwa sababu akili ni dhaifu mno. Inaendeshwa na hofu na mapendeleo. Lakini kuna akili kubwa ndani yako, akili ya Knowledge. Haiko distracted. Haiko katika hali ya mgogoro. Haiwezi kushawishiwa na dunia ama nguvu yoyote, kwa kuwa inawajibika kwa Mungu peke yake. Hio ndio sehemu yako peke yake ambayo ndio safi na inaweza kutegemewa, ni sehemu yako peke yake ambayo ina hekima. Ina dhamira yako kubwa ya kukuja duniani, na inawakilisha uhusiani wako wa msingi na Mungu, ambao haujapotea katika utenganisho.

Licha ya maono ya dunia hii, licha ya shughuli na mlimbiko na majanga ya dunia hii, bado umeshikamana na Mungu. Mungu amekutuma duniani kutumikia dunia katika wakati wake wa haja kubwa. Hiyo ndio maana wewe uko vile ulivyo. Hiyo ndio maana una asili ya kipekee. Hiyo ndio maana una uwezo fulani ambao lazima utumiwe na udhaifu ambao lazima utambuliwe na udhibitiwe kwa hekima. Kwa kuwa huwezi kuwa mdhaifu na ambivalent ukikabiliana na Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko. Yatatoa wito wa nguvu yako ya msingi, na utahitaji nguvu hii ya msingi sasa. Huwezi kuwa mjinga sasa ukikabiliana na ugumu na changamoto ya ukubwa kama huu.

Kwa kweli, Mawimbi Makubwa yanakusanya sasa. Hamuwezi kuyaepuka. Ni makubwa mno na yatadumu muda mrefu sana. Je, una uwazi, unyenyekevu na uaminifu wa kuyaona kikamilifu, kujiandaa kukabiliana nazo kwa kihisia, kisaikilojia na kuanza kujenga msingi wako mwenyewe – msingi ambao umejengwa na Knowledge ndani yako, msingi wa mahusiano, msingi wa shughuli na msingi wa hekima? Unajenga msingi huu sio tu kuweza kusafiri mabadiliko haya makubwa, lakini kuweza kusaidia na kutimikia wengine.

Kwa kuwa lazima ujue kuwa mahitaji ya binadamu yatakuwa makubwa mno katika mustakabali. Kila mtu atakua maskini, na wengi watakuwa katika hali ya umaskini mkubwa mno. Lazima uwe na nguvu hapa sio tu wa kujichunga lakini kuwachunga wengine – kuwachunga wazee, kuwachunga watoto. Kwa kweli wewe mwenyewe hutachunga kila mtu, lakini itakuwa wazi ni nani miongoni mwa majirani wako ama mahusiano yako haswa walio wadhaifu. Lazima uwe na nguvu ya kutosha ya kuwachunga pia hao.

Ingawa hii inaonekana kuwa ni kubwa, ingawa hii sio ile ambayo ungependa kufanya, hii kwa kweli ndio itakukomboa, kwa kuwa hii itakutoa kwa migogoro yako, addictions zako, kutojiamini, majuto yako, kumbukumbu za uchungu. Hii itakulazimisha uimarishe mahusiano ya kweli nawe mwenyewe na wengine na dunia.

Kwa hivyo usiangalie Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko kama tu janga ama hatari kubwa, lakini kama wito, kama hitaji – wito na hitaji ambayo inaweza kukurejesha na kukukomboa, ambayo itaiita mbele Knowledge ndani yako na vipawa vikubwa ambavyo umekuja kuvitoa, vipawa ambavyo vitaamuliwa na hali ambayo sasa inaibuka.

Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko yataleta uwazi kwa maisha yako, na yatakuonyesha udhaifu na nguvu zako. Yatakutoa kutoka ndoto zako za utimizo na janga. Yatakuleta kwa hisia zako, na yatakuleta kwa Knowledge ndani yako. Kwa hivyo, usiyakane. Usiyakatae. Usifikiri kuwa hayana maana ama kuwa watu watakuwa na suluhisho rahisi kwao, kwa kufanya hivyo ni kujikana wito na nguvu ya wakati wako na ukombozi ambao unafaa kukuleta kwa wale waliotumwa duniani kwa sababu ya hali hii.

Hii itakuunganisha na nguvu yako, na itavunja muungano wako na udhaifu wako, kwa kuwa ni wewe ambaye lazima aitwe mbele sasa. Hili sio tatizo la wengine la kurekebisha, kwa kuwa kila mtu lazima achangie sehemu yake. Na wengi wakiitwa katika dhamira kubwa hapa, basi nafasi ya binadamu kufaulu itakuwa kubwa, na ahadi ya binadamu itakuwa kubwa na uwezekano wa binadamu kuishi katika Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko na kuanzisha njia mpya na mwelekeo mpya na umoja na ushiriki mkubwa itakuwa kubwa.

Lakini inategemea ile nguvu ulizaliwa nayo, nguvu ambayo sasa lazima itoke mbele kwa Knowledge ambayo Mungu ameweka ndani yako, ambayo peke yake inajua njia mbele.

Kwa kwa nyakati kubwa ziko nayni. Huu ndio wakati wenyu. Huu ndio wito wenyu. Hapa ndipo nguvu yenyu halisi itapatikana. Nguvu halisi kamwe haipatikani kama watu hawajali na wanalala. Hupatikana tu wakati watu wanajibu na wanafanya kazi kwa kupitia mwelekeo halisi na nia halisi.

Na katika Mafundisho ya Ujumbe Mpya, binadamu sasa ina matumaini makubwa. Kwa mara ya kwanza, kiroho kinafundishwa katika eneo ya Knowledge. Ni wito mkubwa. Ni zawadi kubwa. Inaleta nayo hekima zaidi kuliko ile binadamu amewahi kuimarisha. Inaita watu nje ya vivuli – nje ya migogoro, nje ya vigambo, nje ya addictions, nje ya janga – kujibu kwa dunia iliyo na mahitaji.

Kwa kuwa Ujumbe Mpya unazungumzia hitaji kubwa ya dunia – Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko na Giza Kubwa ya maingilio ambayo iko duniani. Unazungumzia dhamira kubwa ambayo imeita kila mtu hapa. Unazungumzia nguvu ya Knowledge na unafunua jinsi Knowledge inaweza kutambuliwa na kuwa na ufarisi wake. Unazungumzia eneo la mahusiano ambayo watu lazima wafikie kama wanataka kupata muungano wa kweli na nguvu na wengine. Unazungumzia mustakabali wa binadamu katika Jumuiya Kubwa ya waangavu ulimwenguni na kizingiti kukibwa ambacho binadamu lazima apitie kupata hatima na utimizo wake mkubwa.

Umebarikiwa, basi, kupokea Ujumbe huu, kufahamishwa kuhusu Mawimbi Makubwa ya Mabadiliko na kuhusu Giza Kubwa ambayo iko duniani. Kwa kuwa una wakati wa kuwa na ufahamu, kujiandaa na kuandaa maisha yako na kupokea uongozi ambao Mungu amekupatia kupitia Knowledge ambayo ulizaliwa nayo, ambayo ni kipaji kikubwa kutoka kwa Mungu kwako na kwa dunia.